Hossam
JF-Expert Member
- Feb 10, 2011
- 3,536
- 2,153
Nimesoma na kusikitika sana kauli ya membe kwenye gazeti la raia mwema la jana 12-18/10 kwamba eti namnukuu 'Unajua ili uweze kujibu swali hili lazima uangalie matukio ya mwaka 2008. Mwaka 2008 Rais Alivunja Baraza la Mawaziri, hadi Waziri mkuu, Lowassa, akaondolewa. Hakuna huruma hapo. Ameondoa mawaziri na waziri mkuu'. Hivi huyu ndio eti na yeye yuko mbioni kuusakanya urais wa Tanzania, kweli nchi hii ni ya vilaza kabisa.
Mwaka huo huo, 2008 Lowassa alisema, 'Nimetafakari kwa makini suala hili na kwa niaba ya chama changu, nimemuandikia rais barua ya kuachia ngazi (kujiuzuru)'. Membe labda alikuwa kauchapa usingizi hapo.
Kwa nchi kama Tanzania (URT) waziri mkuu akijiuzuru, cabinet nzima inakuwa imefikia tamati bila hata rais kupenda ama asipende. Kwa mujibu wa maneno potofu ya nachelea kusema huyo matamshi ya Membe yanadhihilisha ama Lowassa alilazimishwa kujiuzuru, ama aliambiwa afanye usanii kwa makubaliano fulani, ama wote hawaelewi nini kiliendelea.
Nina wasiwasi ukimuuliza Membe hivi hii miaka 50 ya uhuru ni wa nchi gani, anaweza kukujibu harakaharaha 'Tanzania' badala ya Tanganyika.
Miaka 50 ya umaskini, Tanganyika ya leo hata wembe inaagiza nchi za nje, kweli tunahitaji kusherekea miaka 50 yetu.
Nafungua mjadala.
Mwaka huo huo, 2008 Lowassa alisema, 'Nimetafakari kwa makini suala hili na kwa niaba ya chama changu, nimemuandikia rais barua ya kuachia ngazi (kujiuzuru)'. Membe labda alikuwa kauchapa usingizi hapo.
Kwa nchi kama Tanzania (URT) waziri mkuu akijiuzuru, cabinet nzima inakuwa imefikia tamati bila hata rais kupenda ama asipende. Kwa mujibu wa maneno potofu ya nachelea kusema huyo matamshi ya Membe yanadhihilisha ama Lowassa alilazimishwa kujiuzuru, ama aliambiwa afanye usanii kwa makubaliano fulani, ama wote hawaelewi nini kiliendelea.
Nina wasiwasi ukimuuliza Membe hivi hii miaka 50 ya uhuru ni wa nchi gani, anaweza kukujibu harakaharaha 'Tanzania' badala ya Tanganyika.
Miaka 50 ya umaskini, Tanganyika ya leo hata wembe inaagiza nchi za nje, kweli tunahitaji kusherekea miaka 50 yetu.
Nafungua mjadala.