Membe ni muongo, Kikwete hakuvunja Baraza la Mawaziri: Raia Mwema 12-18/10

Hossam

JF-Expert Member
Feb 10, 2011
3,536
2,153
Nimesoma na kusikitika sana kauli ya membe kwenye gazeti la raia mwema la jana 12-18/10 kwamba eti namnukuu 'Unajua ili uweze kujibu swali hili lazima uangalie matukio ya mwaka 2008. Mwaka 2008 Rais Alivunja Baraza la Mawaziri, hadi Waziri mkuu, Lowassa, akaondolewa. Hakuna huruma hapo. Ameondoa mawaziri na waziri mkuu'. Hivi huyu ndio eti na yeye yuko mbioni kuusakanya urais wa Tanzania, kweli nchi hii ni ya vilaza kabisa.

Mwaka huo huo, 2008 Lowassa alisema, 'Nimetafakari kwa makini suala hili na kwa niaba ya chama changu, nimemuandikia rais barua ya kuachia ngazi (kujiuzuru)'. Membe labda alikuwa kauchapa usingizi hapo.

Kwa nchi kama Tanzania (URT) waziri mkuu akijiuzuru, cabinet nzima inakuwa imefikia tamati bila hata rais kupenda ama asipende. Kwa mujibu wa maneno potofu ya nachelea kusema huyo matamshi ya Membe yanadhihilisha ama Lowassa alilazimishwa kujiuzuru, ama aliambiwa afanye usanii kwa makubaliano fulani, ama wote hawaelewi nini kiliendelea.

Nina wasiwasi ukimuuliza Membe hivi hii miaka 50 ya uhuru ni wa nchi gani, anaweza kukujibu harakaharaha 'Tanzania' badala ya Tanganyika.

Miaka 50 ya umaskini, Tanganyika ya leo hata wembe inaagiza nchi za nje, kweli tunahitaji kusherekea miaka 50 yetu.

Nafungua mjadala.
 
Membe ni CCM kwanza kama JK na CCM lao .Membe ni waziri wa Nje mambo ya ndani kuyajua si rahisi labda alikuwa nje wakati Lowasa anaamua kumeza kaa la moto .Tanganyika ni Nchi gani ? Iko bara gani ? Yaanu hata wazanzibar wanatucheka kwa uhuni huu .Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania mh mshangao mkubwa .Hawa jamaa wana pupa then Lissu akisema juu ya Tanganyika wanasema Chadema wanataka kuuvunja muungano.Upuuzi mtupu .
 
Mwana JF, naungana na hoja yako mia kwa mia; hofu yangu ni weledi mdogo wa waandishi wetu. Hivi walio/aliye kuwa anamuoji hakuona upotoshaji wa Membe? Au ndiyo bahasha za kaki zinatumiwa kubomoana!
 
Mhurumieni huyo Membe jamani si ajabu wakati Lowasa anajiuzulu alikuwa misele huko nje ya nchi..hivyo hakupata taarifa vizuri...teh teh heee
 
URAIS MTAMU!!! Mtu anaweza kusema lolote ili mradi asafishe njia kuelekea magogoni!! Hivi pale magogoni na ile harufu ya soko la feri kuna raha gani?
 
Jamani hebu kumbukeni vizuri, baada ya Mwakyembe kuwasilisha ripoti ya kamati ya richmond, kesho yake mtu wa kwanza kuchangia alikuwa Waziri Mkuu Lowasa, katika mchango wake akasema amemwandikia barua Rais ili ajiuzulu. Lakini kama kumbukumbu zenu zipo Rais hakumjibu Lowasa kumkubalia kujiuzulu na badala yake JK alivunja baraza la mawaziri na kubadilisha mawaziri. So ukweli ni kwamba Lowasa na mawaziri wengine walitimuliwa na JK wala sio kwamba alijiuzulu. Hata Karamagi aliyedai naye kaomba kujiuzulu ni kwamba walifutwa uwaziri. Membe yuko sahhi kabisa
 
Jamani hebu kumbukeni vizuri, baada ya Mwakyembe kuwasilisha ripoti ya kamati ya richmond, kesho yake mtu wa kwanza kuchangia alikuwa Waziri Mkuu Lowasa, katika mchango wake akasema amemwandikia barua Rais ili ajiuzulu. Lakini kama kumbukumbu zenu zipo Rais hakumjibu Lowasa kumkubalia kujiuzulu na badala yake JK alivunja baraza la mawaziri na kubadilisha mawaziri. So ukweli ni kwamba Lowasa na mawaziri wengine walitimuliwa na JK wala sio kwamba alijiuzulu. Hata Karamagi aliyedai naye kaomba kujiuzulu ni kwamba walifutwa uwaziri. Membe yuko sahhi kabisa
yale yale tu!!
katibu mkuu anakuwa na kashfa, anastaafu kwanza ndo anapelekwa mahakamani.
 
Nimesoma na kusikitika sana kauli ya membe kwenye gazeti la raia mwema la jana 12-18/10 kwamba eti namnukuu 'Unajua ili uweze kujibu swali hili lazima uangalie matukio ya mwaka 2008. Mwaka 2008 Rais Alivunja Baraza la Mawaziri, hadi Waziri mkuu, Lowassa, akaondolewa. Hakuna huruma hapo. Ameondoa mawaziri na waziri mkuu'. Hivi huyu ndio eti na yeye yuko mbioni kuusakanya urais wa Tanzania, kweli nchi hii ni ya vilaza kabisa.

Mwaka huo huo, 2008 Lowassa alisema, 'Nimetafakari kwa makini suala hili na kwa niaba ya chama changu, nimemuandikia rais barua ya kuachia ngazi (kujiuzuru)'. Membe labda alikuwa kauchapa usingizi hapo.

Kwa nchi kama Tanzania (URT) waziri mkuu akijiuzuru, cabinet nzima inakuwa imefikia tamati bila hata rais kupenda ama asipende. Kwa mujibu wa maneno potofu ya nachelea kusema huyo matamshi ya Membe yanadhihilisha ama Lowassa alilazimishwa kujiuzuru, ama aliambiwa afanye usanii kwa makubaliano fulani, ama wote hawaelewi nini kiliendelea.

Nina wasiwasi ukimuuliza Membe hivi hii miaka 50 ya uhuru ni wa nchi gani, anaweza kukujibu harakaharaha 'Tanzania' badala ya Tanganyika.

Miaka 50 ya umaskini, Tanganyika ya leo hata wembe inaagiza nchi za nje, kweli tunahitaji kusherekea miaka 50 yetu.

Nafungua mjadala.
rais anaweza kulivunja baraza lake la mawaziri endapo yafuatayo yatatokea:
Kujiuzuru kwa waziri mkuu na mengineyo. kwa hiyo rais alivunja baraza la mawaziri. IF A=B,B=C THEN A=C FINITO.
 
hizi ni siasa za kuchafuana tu na hazina mashiko yoyote. sasa mambo ya mwaka jana unatuletea leo?? hjata kama na sisi tukitaka kuona hiklo gazeti itakuwaje? ulikuwa wapi siku zote hizi kuyasema haya? au kwa sababu umetumwa kumchafua huyu? Je na mpuuzi mwingine akileta thread humu kwamba mwanahalisi la 2007 February, Lowassa alidanganya halmashauri ya Rungwe,, tuamini pia??acheni upuuzi nyie,, tuongee changamoto zilizopo na zinazokuja.
 
Nimesoma na kusikitika sana kauli ya membe kwenye gazeti la raia mwema la jana 12-18/10 kwamba eti namnukuu 'Unajua ili uweze kujibu swali hili lazima uangalie matukio ya mwaka 2008. Mwaka 2008 Rais Alivunja Baraza la Mawaziri, hadi Waziri mkuu, Lowassa, akaondolewa. Hakuna huruma hapo. Ameondoa mawaziri na waziri mkuu'. Hivi huyu ndio eti na yeye yuko mbioni kuusakanya urais wa Tanzania, kweli nchi hii ni ya vilaza kabisa.
Hiyo tarehe uloiweka hapo 12/18/10 naamini kwamba unamaanisha December 18 siyo? Na sote tunajua kwamba Raia mwema hutoka kila siku ya jumatano. Sasa tarehe hiyo uloweka wewe mbona haikuwa Jumatano? hii tarehe ilikuwa jumamosi, wewe umetoa wapi hilo gazeti la Raia mwema la Jumamosi? N hata kama ulimaanisha kusema tarehe 12,, nayi haikuwa jumatano,, sasa kama si uongo na uzushi humu ndani kwa njaa zenu ni nini? N gazeti lenyewe ulifungiwa maandazi niini maana toka December hadi leo umelipekua ili ulisome utuletee upuuzi kuhusu Membe uliliweka wapi? Sote tunajua Raia mwema walikuwa hawako online by that time. Wewe ni mzushi,, MODs please toa hii thread ya majungu.
 
sipendi viongozi wanafki like membe,,,,,thread za leo kweli zote kali naomba na magogoni wazipate, ikiwezekana wachukue hatua kwa mtu kama mkulo aaaaaaaaaaaaaaaaachie ngazi
Wee nawe mbona unaingia kimugongo mugongo bila data wala taarifa zozote? unashabikia tu hata upuuzi. Kafanye utafiti ndipo ulete majungu yako hapa. Chundu kama nyie ndiyo mnalishushia hadhi jukwaa hili
 
rais anaweza kulivunja baraza lake la mawaziri endapo yafuatayo yatatokea:
Kujiuzuru kwa waziri mkuu na mengineyo. kwa hiyo rais alivunja baraza la mawaziri. IF A=B,B=C THEN A=C FINITO.
Waelimishe wabangubangu hawa wasio na data na vilaza wa katiba na sheria
 
Mhurumieni huyo Membe jamani si ajabu wakati Lowasa anajiuzulu alikuwa misele huko nje ya nchi..hivyo hakupata taarifa vizuri...teh teh heee
Ya nini kumhurumia kama kuna hoja ya ukweli?? Tatizo ni kwamba hakuna hoja hapa zaidi ya ushambenga tu. Watu hata tarehe wanazitunga haziendani na siku husika, na ninyi mnaojiita Great thinkers mnaamini tu na kushabikia kila upupu humu!! shame
 
Hiyo tarehe uloiweka hapo 12/18/10 naamini kwamba unamaanisha December 18 siyo? Na sote tunajua kwamba Raia mwema hutoka kila siku ya jumatano. Sasa tarehe hiyo uloweka wewe mbona haikuwa Jumatano? hii tarehe ilikuwa jumamosi, wewe umetoa wapi hilo gazeti la Raia mwema la Jumamosi? N hata kama ulimaanisha kusema tarehe 12,, nayi haikuwa jumatano,, sasa kama si uongo na uzushi humu ndani kwa njaa zenu ni nini? N gazeti lenyewe ulifungiwa maandazi niini maana toka December hadi leo umelipekua ili ulisome utuletee upuuzi kuhusu Membe uliliweka wapi? Sote tunajua Raia mwema walikuwa hawako online by that time. Wewe ni mzushi,, MODs please toa hii thread ya majungu.

Mkuu unaangalia kalenda ipi? Yangu inaonuesha Jumatano. Jamaa yuko sahihi labda useme husomi sred sawasawa
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom