Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,045
- 20,408
ANAANDIKA MH. BENARD KAMILLIUS MEMBE, SIMBA WA RONDO.
Watanzania Wenzangu! Nawasalimia! Kwa siku tatu mfululizo magazeti ya makuhani wa fitina na
unafiki Musiba na Mchange na wenzao wamekuwa wakinishambulia kwa uchochezi wa sintofahamu
iliyotokea kuanzia Alhamisi tarehe 17 Octoba siku ambayo Mhe Rais ameondoka Lindi kuelekea Dar hadi Jumapili ya tarehe 20.
Mimi nipo Kijijini kwangu Rondo kwa mwezi mmoja sasa. Ni nini hicho nilichokisema au
kukiandika kwenye mitandao ya kijamii? Kwa kuwa mawasiliano yangu yote nayafanya kwa simu
yangu ambayo inasikilizwa na kudukuliwa, naviomba vyombo vinavyohusika vitoe hadharani
mazungumzo na maandishi yangu ili watu wasikie, wasome na wanihukumu.
Napenda niuhakikishie umma kuwa Mimi sikuwa mjinga! Nilijua kuwa nikisema au kuandika vibaya, wabaya wangu wataninyooshea vidole. Sikuingia kwenye mitego yao hiyo. Mimi kama Watanzania wote wenye akili za kawaida nilishangazwa sana na ukimya wa Serikali huku damage na rumours zikiwa zimetanda kote nchini bila kuzitolea maelezo kwa siku 3 mfululizo!
Mhe. Rais ni kiongozi wa Umma.
Inapotokea sintofahamu au upotoshaji wowote ule, ulikuwa ni wajibu wa Msemaji wa Ikulu au wa Serikali kukanusha na kuweka mambo sawa kama wanavyofanya siku zote. Vinginevyo wale wenye akili za mbilikimo na makuhani wa unafiki wanachukua mwanya huo kutunga ya kwao ili kumfurahisha Mhe. Rais.
Good governance requires quick response to rumours. Rumours left unattended damages governance! Narudia! Naviomba vyombo husika vitoe hadharani nilichokisema au kupost kwenye mitandao ili nihukumiwe na Wananchi wenyewe na sio na Wabwekaji wa Taifa. Ben Membe. Rondo- Lindi.
#NiguseNinuke2020
Watanzania Wenzangu! Nawasalimia! Kwa siku tatu mfululizo magazeti ya makuhani wa fitina na
unafiki Musiba na Mchange na wenzao wamekuwa wakinishambulia kwa uchochezi wa sintofahamu
iliyotokea kuanzia Alhamisi tarehe 17 Octoba siku ambayo Mhe Rais ameondoka Lindi kuelekea Dar hadi Jumapili ya tarehe 20.
Mimi nipo Kijijini kwangu Rondo kwa mwezi mmoja sasa. Ni nini hicho nilichokisema au
kukiandika kwenye mitandao ya kijamii? Kwa kuwa mawasiliano yangu yote nayafanya kwa simu
yangu ambayo inasikilizwa na kudukuliwa, naviomba vyombo vinavyohusika vitoe hadharani
mazungumzo na maandishi yangu ili watu wasikie, wasome na wanihukumu.
Napenda niuhakikishie umma kuwa Mimi sikuwa mjinga! Nilijua kuwa nikisema au kuandika vibaya, wabaya wangu wataninyooshea vidole. Sikuingia kwenye mitego yao hiyo. Mimi kama Watanzania wote wenye akili za kawaida nilishangazwa sana na ukimya wa Serikali huku damage na rumours zikiwa zimetanda kote nchini bila kuzitolea maelezo kwa siku 3 mfululizo!
Mhe. Rais ni kiongozi wa Umma.
Inapotokea sintofahamu au upotoshaji wowote ule, ulikuwa ni wajibu wa Msemaji wa Ikulu au wa Serikali kukanusha na kuweka mambo sawa kama wanavyofanya siku zote. Vinginevyo wale wenye akili za mbilikimo na makuhani wa unafiki wanachukua mwanya huo kutunga ya kwao ili kumfurahisha Mhe. Rais.
Good governance requires quick response to rumours. Rumours left unattended damages governance! Narudia! Naviomba vyombo husika vitoe hadharani nilichokisema au kupost kwenye mitandao ili nihukumiwe na Wananchi wenyewe na sio na Wabwekaji wa Taifa. Ben Membe. Rondo- Lindi.
#NiguseNinuke2020