Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,477
- 30,130
Tumemsikia wenyewe aliyekuwa mwanachama wa CCM, Bernard Membe akidai kuwa katika kufukuzwa kwake CCM, Katiba ya chama chake haikuzingatiwa
Kwa maelezo yake, kikao pekee chenye uwezo wa kumfukuza mwanachama yeyote wa CCM, ni Halmashauri Kuu ya CCM, jambo ambalo haliikufanyika, badala yake ni kikao cha Kamati Kuu (CC) ya CCM kilichojitwalia mamlaka hayo ya kumfukuza yeye uanachama, jambo ambalo aliliita ni la kuvunja Katiba ya chama chao waziwazi
Kutokana na maelezo yake mwenyewe, Bernard Membe, alieleza kuwa mchakato wa kumfukuza kwenye chama hiko cha CCM, bado haujakamilika, kwa vile kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) bado hakijaketi ili kubariki uamuzi huo wa Kamati Kuu ya CCM.
Maswali ya kuwauliza wajumbe wa kikao hicho cha Kamati Kuu ni haya, je ni kweli madai ya Membe kuwa alifukuzwa uanachama wa CCM na kikao ambacho hakina mamlaka hayo kikatiba?
Kama ni kweli, ni kwanini kikao hicho cha chama kikongwe barani Afrika, kifanye kitendo hicho cha kuvunja Katiba yake yenyewe?
Je chama hicho kimeanza kuvunja Katiba ya Chama chake, kama "walivyozoea" kuvunja Katiba ya nchi waziwazi?
Baba wa Taifa hili, Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka wakati akiwa hai kuwa mtu anayeanza kula nyama ya mtu hataacha kamwe!
Je ni kweli baada ya CCM kuanza "kuisigina" waziwazi Katiba ya nchi, sasa wameamua kuanza "kuisigina" Katiba ya Chama chao cha CCM?
Ningependa nijibiwe hayo maswali yangu machache.
Kwa maelezo yake, kikao pekee chenye uwezo wa kumfukuza mwanachama yeyote wa CCM, ni Halmashauri Kuu ya CCM, jambo ambalo haliikufanyika, badala yake ni kikao cha Kamati Kuu (CC) ya CCM kilichojitwalia mamlaka hayo ya kumfukuza yeye uanachama, jambo ambalo aliliita ni la kuvunja Katiba ya chama chao waziwazi
Kutokana na maelezo yake mwenyewe, Bernard Membe, alieleza kuwa mchakato wa kumfukuza kwenye chama hiko cha CCM, bado haujakamilika, kwa vile kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) bado hakijaketi ili kubariki uamuzi huo wa Kamati Kuu ya CCM.
Maswali ya kuwauliza wajumbe wa kikao hicho cha Kamati Kuu ni haya, je ni kweli madai ya Membe kuwa alifukuzwa uanachama wa CCM na kikao ambacho hakina mamlaka hayo kikatiba?
Kama ni kweli, ni kwanini kikao hicho cha chama kikongwe barani Afrika, kifanye kitendo hicho cha kuvunja Katiba yake yenyewe?
Je chama hicho kimeanza kuvunja Katiba ya Chama chake, kama "walivyozoea" kuvunja Katiba ya nchi waziwazi?
Baba wa Taifa hili, Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka wakati akiwa hai kuwa mtu anayeanza kula nyama ya mtu hataacha kamwe!
Je ni kweli baada ya CCM kuanza "kuisigina" waziwazi Katiba ya nchi, sasa wameamua kuanza "kuisigina" Katiba ya Chama chao cha CCM?
Ningependa nijibiwe hayo maswali yangu machache.