Membe & Kabaka: Lindi kuanzisha University!!

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,408
54,886
Tanzania Daima said:
WANANCHI mkoani hapa wamechanga sh 38,728,000, kwa ajili ya ujenzi wa chuo kikuu, ikiwa moja ya hatua ya kusogeza huduma hiyo muhimu inayolenga kuinua kiwango cha elimu.

Michango hiyo ni pesa taslimu na ahadi zilizotolewa katika harambee iliyofanyika kwenye ukumbi wa Oceanic Hotel, hapa, mwishoni mwa wiki. Harambee hiyo iliongozwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Gaudensia Kabaka.

Katika harambee hiyo, wananchi wa mkoa huo walichanga papo hapo kiasi cha sh 14,293,000 wakati sh 24,435,000 ni ahadi zilizotolewa na watu mbalimbali, mashirika na taasisi za umma na Serikali na wadau wengine wa maendeleo wa mkoa huo.

Katika uchangiaji huo, Kabaka na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, na marafi zake - Mbunge wa Lindi Mjini ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Abdulaziz - kila moja alichangia sh 1,000,000.

Wengine ni kampuni ya Bioshape Limited yenye makao yake wilayani Kilwa, inayojishughulisha na ulimaji wa mibono kwa ajili ya kutengeneza mafuta ya dizeli, kupitia taasisi yake ya Bioshape Benefits Foundation, Ruvuma Construction pamoja na Jamal Malinzi, kila moja wakichangia sh 1,000,000.

Ofisi za wakuu wa wilaya zote tano za Lindi, Nachingwea, Ruangwa, Kilwa na Liwale kila moja zilichangia kiasi sh 300,000, wakati ofisi tatu za wakurugenzi watendaji - Lindi Vijijini, Liwale na Ruangwa, zikitoa kiasi kama hicho kila moja, wakati Nachingwea na Kilwa zikitoa sh 200,000 na Lindi Mjini sh 100,000.

Vyama viwili vya siasa vya CCM na CUF vilijitokeza katika harambee hiyo. CCM ilichangia sh 300,000 na CUF sh 100,000.

Wachangiaji wengine - wabunge wawili wa Viti Maalumu Mkoa wa Lindi kwa tiketi ya CCM - Fatuma Mikidadi, Rulida Said - Oceanic Hotel, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kila mmoja akichangia sh 500,000. Kiasi kilichobaki kimechangiwa na taasisi za umma na watu binafsi.

Akizungumza mara baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, ambaye pia ni mkuu wa mkoa huo, Said Meck Sadiki, kutangaza mapato hayo, Kabaka aliwataka wananchi wa mkoa huo waendelee kuchangia ujenzi wa chuo hicho.

wandugu,

..wahenga walisema "safari ni hatua." naona wana-Lindi wameanza safari ya Ujenzi wa Chuo Kikuu.

..napendekeza wasikibatize chuo kikuu chao majina ya wanasiasa, badala yake wakipe jina rahisi, zuri, Lindi University.

..natoa hongera kwa wananchi na viongozi wa mkoa wa Lindi kwa kuleta wazo hili la maendeleo.

NB:

..ile University ya kule Bukoba inaendelea vipi? pia nakumbuka Nimrod Mkono naye ana project yake ya kujenga University karibu na Butiama.
 
Hii inaweza kuwa ni hatua mzuri kwa mkoa wa Lindi kukwea kwenye ramani ya Tanzania.

Hivi stats za wahadhiri bongo ziko vipi? Idadi yao inaongezeka au? Nafikiri kuna haja kubwa ya kufanya research (kama bado) ya idadi ya wanafunzi wanaofuatilia kazi ya uhadhiri kwa karibu. Hi itasaidia kufanya tathmini ya wapi tunakwenda katika suala la upanuaji na uongezaji wa vyuo nchini.
 
Tatizo ni kuwa kutokana na mwamko mdogo wa watu wa mkoa huo, kuna uwezekano michango ikachukua muda mrefu sana kufikia viwango vinavyotakiwa, hivyo zinazokusanywa kuwa hatarini kufisadiwa.
Labda shemeji (muungwana) awasaidie kupata mfadhili wa nguvu na kazi iende motomoto
 
Hata WAMA nao wanaweza kuchangia pia.

Hivi WAMA ina miradi Dar na Lindi tu ama iko kila mkoa? Mara kwa mara nikisikia shughuli ya WAMA basi itakuwa ni Lindi au Dar, sehemu nyingine hakuna wanawake?

Wakati Lowassa akiwa PM nilisikia pia WAMA wana mradi wa ujenzi wa sekondari kule Monduli, baada ya EL kuondoka sijasikia developments za hiyo project.
 
Si haba maana yerere aliwaadhibu sana mikoa hiyo ya kusini kama alivyowafanyia watu wa mikoa ya pwani

Kudos Membe hii ni hatua nzuri
 
Hizi University zinachomoka kila kukicha kama uyoga zitakuwa na wahadhiri wenye sifa zinazostahili au ndiyo sifa tu ya kwamba na sisi mkoa wetu una University lakini elimu inayotolewa hapo ni bomu kwa kuwa University haina wahadhiri wenye sifa na wa kutosha? Je, na kazi zipo au ndiyo watabebeshwa mikopo ya mamilioni na kazi hamna halafu waambiwe wajiajiri? Kwa maoni yangu nguvu zingeelekezwa kwanza kuboresha shule za msingi na sekondari katika mkoa huo ili wanafunzi wengi wafanye vizuri na hatimaye kupata nafasi katika vyuo vikuu vilivyopo, au si ajabu kutakuwa na University halafu shule za msingi na sekondari mkoani hapo zimeja hohe hahe watupu na wala hazina walimu kabisa.
 
Bubu ataka kusema,

..mawazo yako ni mazuri tu. lazima juhudi zielekezwe ktk kuboresha elimu ya msingi na sekondari.

..utoaji ELIMU ndiyo lengo kuu la kuanzishwa kwa Chuo Kikuu.

..lakini mimi leo hii hata kama wana-Lindi wenyewe hawako tayari kufaidi matunda ya KIELIMU ya chuo kikuu hicho naamini wazo la kuanzishwa kwake ni zuri.

..naomba pia mkiangalie hiki chuo kikuu kama kitega uchumi. kuna miji ambayo imestawi kutokana na "biashara" ya chuo kikuu.

..kuna shughuli nyingi tu za kiuchumi[real estate,hotels,transportation,...] ambazo wana-Lindi watafaidika nazo ikiwa azma ya kuanzisha hicho chuo itafanikiwa.
 
Si haba maana Nyerere aliwaadhibu sana mikoa hiyo ya kusini kama alivyowafanyia watu wa mikoa ya pwani
Kudos Membe hii ni hatua nzuri

Mie kwa Moyo mmoja ninawapongeza Mh. B. Membe na Mh. G. Kabaka kwa wazo hili zuri na la kuendeleza Tanzania yetu.

Ila ndugu yangu GT, uliloliandika sikubaliani nalo; Nivyema ukaangalia historia ya nchi yetu kuanzia Mwarabu, Mreno, Mjerumani na Muingereza hadi Julias unayemshutumu kuwa aliwaadhibu watu wa mikoa ya Pwani.
Hivi na huko Darfur ni Nyerere aliwaadhibu?
 
Membe wazo zuri....

Kuwepo kwa chuo ni Jambo zuri watasoma watu wote...pia wageni kutoka Mikoa na Nchi zingine za jiran watafika..Hii itasababisha mji kukua Haraka!!!...Ila wazee wa Lindi wawe makini na watoto wao wa Kike....maana wanapokuwepo watoto wa chuo....ni kufanya uharibifu tu...!!!
 
Ni kutafuta sifa za Kisiasa bila kuangalia uwezekano wa mafanikio.

Mbona huko huko Lindi wameshindwa kabisa kupta waalimu kwa shule za msingi na sekondari. Siyo zile za kata tu bali hata zile kongwe hazina waalimu.

Ndo hawa tunaodhani wanaweza kuleta maendeleo!
Kama wanasikia, bora waanze na mambo ya msingi ya kusini. Chuo kikuu si tatizo tena TZ, na huyo Membe anatakiwa afahamu hivyo. Si tumesikia serikali ikitangaza idadi ya wanafunzi wanayotakiwa Univ. of Dodoma?

Ni Mbwembwe zisizo manufaa!
 
Suala la kila mkoa kuwa na University yake silishabukii wala siliungi mkono. Kama haja hiyo ipo, basi zingeanza kwa Kanda. Sababu kubwa ni kama ifuatavyo:-
a. Wanafunzi wa kuingia kwenye hizo university wako wapi? Kwa hali ilivyo sasa, mahitaji ya wanafunzi wa sayansi kwenye vyuo vilivyopo bado hayajakidhiwa. Ndio maana SUA wana-admit mpaka watu wenye Subsidiries tu.
b. Wahadhiri waliopo ni hao wa UDSM na SUA. Ndio hao wanaozunguka vyuo vyote vilivyopo. Mfano: ilipoanzishwa Mzumbe Univ. kulikuwa na wahadhiri wangapi wenye PhD? Sembuse hizo za vichochoroni. Hapa panahitajika maandalizi makubwa na kila chuo kinachotaka kufunguliwa kieleze na mipango ya kujiandalia wahadhiri.
c. Kikubwa sasa hivi, baada ya MMEM na MMES, ni uimarishwaji wa elimu ya vidato vya tano na sita. Kuibadili Mkwawa High School kuwa Chuo kikuu ilikuwa ni moja ya makosa makubwa sana. Hiki ndio kilikuwa pool ya undergraduates wa sayansi. je, tulianzisha shule mbadala?

Kielimu, Lindi bado iko nyuma sana. Kuanzisha Chuo kikuu sioni kama itakuwa njia ya kuinua elimu kwa wananchi waliopo Lukuledi, Naipanga, Farm 17 etc.
 
Siku hizi kunazisha "University" ishakuwa fasheni kwa uyoga huu wa vyuo tuahau habari ya viwango...
 
Tatizo letu watanzania hatuna dira kuu inayotouongoza kujua tunataka kwenda wapi ambayo na ilitakiwa kuja baada ya kukaa chini na kujadili matatizo yetu ni yapi na jinsi gani tuyatatuwe. Kwa hiyo kila mtu akilipuka na wazo lake tunaona ni sawa tu ...
 
Mgirima kasema ukweli: Ni lazima kuwa na mipango ya kiukweli.

Shilingi milioni 38 hazitoshi hata kujenga nyumba moja! Sii mtaji wa kuanzishia chuo kikuu. Na muhimu zaidi ni ulimbukeni kupanga kujenga chuo kikuu wakati huna hata sekondari 5 zilizotengamaa!

Hiwezekani kuendeleza nchi na mikoa kuanzia juu kwenda chini. Ukitaka kuleta mapinduzi ya elimu Lindi basi anza na kuimarisha elimu ya sekondari. Kwa sasa, wanaomaliza sekondari Lindi wapeni skolaship kwa kutumia hivyo vimilioni 38 ili wasome vyuo vizuri, wajitayarishe kuwa wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Lindi siku za usoni.

Siku nitatona wazazi kutoka sehemu mbali mbali za Tanzania wanatumia barabara kuu ya Dar hadi Lindi kuwakimbizia watoto wao kwenda kupigania nafasi katika shule nzuri za sekondari za Lindi (kama inavyofanyika kwa Marian College, St. Gorret, etc) basi nitajua kazi inaanza huko Lindi. Linalopangwa sasa ni ulimbukeni (mediocrity) tu.

AMKENI ndugu zangu wa Lindi! Mtalala mpaka lini? Kumekucha?
Mnaweza kuiga mikoa kama Kilimanjaro: haikuinua elimu kwa kukurupukia vyuo vikuu!
 
Hizi University zinachomoka kila kukicha kama uyoga zitakuwa na wahadhiri wenye sifa zinazostahili au ndiyo sifa tu ya kwamba na sisi mkoa wetu una University lakini elimu inayotolewa hapo ni bomu kwa kuwa University haina wahadhiri wenye sifa na wa kutosha? Je, na kazi zipo au ndiyo watabebeshwa mikopo ya mamilioni na kazi hamna halafu waambiwe wajiajiri? Kwa maoni yangu nguvu zingeelekezwa kwanza kuboresha shule za msingi na sekondari katika mkoa huo ili wanafunzi wengi wafanye vizuri na hatimaye kupata nafasi katika vyuo vikuu vilivyopo, au si ajabu kutakuwa na University halafu shule za msingi na sekondari mkoani hapo zimeja hohe hahe watupu na wala hazina walimu kabisa.

Kuanzisha University kwenye mkoa fulani haimaanishi watu wa mkoa husika tu ndo wasome. Pia inaweza kutumika na watu kutoka nje ya mkoa husika ambao watapenda. Watu kutoka nje pia wanaweza kuwa chachu na kuhamasisha watu wa mkoa huo kuchangamkia opportunity hiyo.
 
Kuanzisha University kwenye mkoa fulani haimaanishi watu wa mkoa husika tu ndo wasome. Pia inaweza kutumika na watu kutoka nje ya mkoa husika ambao watapenda. Watu kutoka nje pia wanaweza kuwa chachu na kuhamasisha watu wa mkoa huo kuchangamkia opportunity hiyo.

Vp hii kitu ilifanikishwa tayari? au bado bwana Membe hajaoteshwa ndoto ya kuanza ujenzi wa hii university?
 
Napata shida sana kuona watu wanakuwa na wasiwasi wa kuanzisha vyuo vikuu vya kutosha. Tanzania tumekuwa nyuma sana tukilinganisha na nchi nyingine zilizopata uhuru miaka ya 1960 kwa sababu ya unyuma wa elimu yetu. Maendeleo yeyote yale yanatokea kwenye elimu. Akili za kutukuza uUDSM na uSUA si sahihi hata kidogo za zinadumaza akili. Acha watu wasome. Issue ya ubora wa elimu unaupima kwenye soko la ajira pekee. By the way, kuna graduates wengi tu wa kutoka vyuo tajwa waliomtaani kwa kukosa ajira pengine kwa ajili ya incompetence. Then, how do you measure that? Please stop narrow thinking. Acha vyuo vijengwe vitoe fursa za ajira, elimu na huduma kwa jamii. Peopleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeees...:peace:
 
Hv nyinyi watz mbona akili zenu ndogo sana. Watu wanataka kufanya jambo la maendeleo msaanza kubeza.
Kuna ubaya gani kila mkoa ukawa na chuo kikuu??
Kwani lazima wote tukae dar es salaam??
 
Back
Top Bottom