Membe: Gaddafi amefikia mwisho lakini hatuwatambui waasi!

I personally heard the talks between our Minister (Membe) and the BBC this morning. He really showed the kind of diplomatic leaders we are currently having; very bad.

Nilijiuliza, hivi huyo Balozi wa Libya anapaswa kutii mamlaka ya nani? (Balozi) Anajua fika bosi wake wa zamani (Gaddafi) hayuko tena madarakani na order imetolewa na watawala wapya (waasi), japo hawajaapishwa, juu ya mambo mbalimbali yahusuyo taifa lao ikiwamo kwa balozi za nje kupeperusha bendera mpya; hivi ni mpumbavu gani angekuwa na ujasiri wa kukataa agizo kama hilo? Nani asiyependa maisha yake, potelea mbali kazi?

Kitendo alichofanya Membe ni kibaya mno kiasi kwamba kinahatarisha hata usalama wa raia wa Tanzania na waafrika wengine waishio Libya kwa sasa. Kuna taarifa kwamba waasi wanawalenga waafrika weusi kwa madai kwamba wanmuunga mkono adui wao Gadafi kama ilivyopostiwa hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/167969-libya-rebels-now-target-%91blacks%92.html

Hivi waasi wakisikia statement ya Membe unategemea watawafnyia nini watanzania wenzetu waishio huko? Busara zaidi zitumike kwenye suala hili badala ya kujuana na ubabe wa kijinga.

Waasi wenyewe wamechemsha kwa kufanya mambo shaghalabaghala.

Balozi wa nchi anapotambuliwa na nchi nyingine hupeleka credentials zake Ikulu, huyu balozi wa sasa wa Libya alipeleka credentials za Gaddafi Ikulu, hao waasi hawajaleta balozi wao na credentials zao, kwanza hawana hata serikali.

The Libyan situation exposes a lot of hypocrisy.Mijitu imefanya kazi na serikali ya Gaddafi miaka yote, imeua naye, leo imeona Gaddafi anapigwa, imemgeuka. Hawa ma rebel wana risk kupigwa dafrao style ya Shibuda CHADEMA. Kwa nini wasiunde serikali kwanza, kuondoa mabalozi wa Gaddafi, na kuchagua mabalozi wao wapya?

Hawa mabalozi wa Gaddafi wanaojifanya kuuona mwanga dakika ya mwisho wakiwa wanavujisha habari muhimu za kidiplomasia kwa Gaddafi hawa waasi watafanyaje? Hapa naona inexperience tu.
 
Nafikiri aliyoyasema Membe si msimamo wa watanzania bali ni msimamo wake yeye na kundi lake linalomwonea huruma Gadafi kwa sababu wanazozijua wenyewe
 
Maskini Tanzania, yaani sisi leo tunafuata? Hawa wangekuwa wakati wa harakati za ukombozi PLO, POLISARIO, ANC, FRELIMO n.k wasingepata nafasi Tanzania. je wanaitambua serikali ya Misri au ya Tunisia? Na hiki kipimo cha "Kuapishwa kwanza" kimeanza lini. Si waseme tu kuwa urafiki ulikuwa na Gaddafi lakini siyo wananchi wa Libya? Hii ni aibu kwa Tanzania.

Kwa heshima ya kipekee Mzee Mwanakijiji,

Ninadhani unaijua vema siasa/diplomasia za mataifa ya ulimwengu zikiwemo hizo za Libya. Nina amini kwa weledi wako uliotukuka katika nyanja hizi unakijua vizuri sana chanzo haswa cha mgogoro Walibya. Iweje leo uutamkie ulimwengu kuwa, kwa msimamo iliotoa Tanzania wa kutowatambua "wahuni wa Bengharz" ingawa kwa sababu zisizo na hoja nzito sana ila zenye ujumbe uliofichika, kuwa Tanzania ilikuwa rafiki wa Gaddaf wala si Walibya. Libya ni ya sehemu ya Afrika na kama kweli ulikuwa unaitakia mema Afrika huwezi kushangilia machafuko yaliyotokea katika nchi za kaskazini mwa afrika, vivyo hivyo huwezi kusema Tanzania imetia aibu kwa msimamo wake juu ya Libya. Mbali na mapungufu yake kwa kiasi Serikali imeonyesha kukerwa na mwenendo wa mambo huko Libya na inajari Umoja, Amani, Maendeleo ya msingi kwa bara la Afrika na waafrika kwa ujumla. Kama unafikiria uhuru wa Afrika huwezi kufikiria kuwatambua "wahuni wa Bengarz" wakisaidiwa na 'nAtO' kwa kuazimia kuanza kujiibia wenyewe rasilimali zao ambazo zingewasaidia kuimarisha uchumi wa nchi yao. Sijawahi kuhoji mada zako, kwani huwa unaandika mambo yanayoelekeza kujikwamua kwa kila hali kwa kila rika, lakini hii imenishtua kidogo Mzee Mwanakijiji, kwani napata shida kuelewa msimamo wako juu ya mstakabali wa maendeleo ya Afrika iliyo huru. Nina imani utakuwa na nafasi ya kulitolea ufafanuzi jambo hili.

Ninajitambulisha kama Mwafrika wa Tanzania.
 
huyo balozi wa Libya anatetea masalhi yake. nakumbuka alishiriki maandamno kuunga mkono utawala wa Gadaffi mwanzoni kabisa wakati mgogoro ndio unaanza. maandamano yaliishia viwanja vya Biafra, Kinondoni, Dsm. sasa kaona jamaa kan'goka ndio anajifanya anawaunga mkono. ni unafiki mkubwa!
 
Nchi zilizoitambua NTC tunazijua,mbona makarai,wangefanya nini zaidi.Wamefanya what is expected of them na mambwana zao.Kwa mtu mwenye akili timamu, kuitambua NTC ni kitendo cha kisaliti kwa wananchi wa dunia wanaopata mateso ya kutisha kwa ajili ya mikakati ya New World Order.No doubt Tanzania will follow suit,haya maneno ya Membe yanadhihirisha hilo.
Membe amesema Tanzania inajua kwamba hatima ya Kanali Muammar Gaddafi kuongoza Libya imekwishafikia, lakini haiwezi kuwatambua waasi wakati bado hawajaunda serikali. “Serikali ni pamoja na kuwa na viongozi walioapishwa, tutawatambua kama watakuwa na mihimili mitatu ya serikali, bunge na mahakama,” alisema Membe.

Hadi sasa nchi za Afrika ziizoitambua serikali ya waasi wa Libya ni pamoja na Kenya, Botswana, Ethiopia, Djibut, Rwanda na Tunisia. Nyingine ni Senegal, Gabon, Gambia, Bokina Faso, Benin na Nigeria. Zingine ni Morocco, Chad, Ivory Coast, na Ghana.

Source: Mwananchi
 
On the outset, let me state that I am against tyrants and for democracy, and I am glad to see Gaddafi go.

Membe kapatia kwamba Gaddafi amefikia mwisho wa kamba.

Membe kapatia kwamba serikali ya Tanzania haitakiwi kuwatambua "waasi".

Membe kakosea kwa kutupa sababu mbuzi za kuapishwa. On a broader scale, anaweza kutafsiriwa kumaanisha kwamba hawezi kuitambua serikali ambayo haipo, in which case, he is right.

Kusema kwamba huwezi kuitambua entity ambayo haijaapishwa kama serikali kuwa ni serikali rasmi ni sawa, kusema kwamba huwezi kuitambua entity ambayo haijaapishwa kama serikali rasmi, kama serikali rasmi, si sawa. Biafra notwithstanding. Nyerere could have erred, or bended governmental procedure to make a moral point. Our Foreign Policy - if it exist at all, Game Theory would disagree that it does- is not written in stone.

Kwamba Gaddafi kafikia mwisho wa kamba, kila mtu - ukiondoa the usual < 5% die hard supporters, anaelewa. Hilo mjadala wake si mkubwa.

Serikali ya Tanzania ikiwatambua waasi, iwatambue waasi gani? Kwanza waasi wenyewe ni kina nani? Siasa yao ya nje ni ipi? As far as I can see on TV naona machizi wanapiga risasi hewani tu. Wana msimamo gani kuhusu interests za Tanzania? Na kwa nini tuwatambue kabla hata hatujajua wanasimamia wapi? Waacheni waunde serikali, tujue watawapa haki wa Berber au wataendelea kuwakandamiza kama alivyowakandamiza Gaddafi, kama watajipendekeza kwetu kama alivyofanya Gaddafi siku za mwisho au watatudiss.

Hivi tunatambua dynamics zenye upana zaidi ya "tyrant Gaddafi versus the Libyan people" ziinazo play hapa?

Hivi tunatambua Tripoli vs. Bengahazi drama iliyopo hapa? Tunatambua Royalists vs. Gaddafi? Tunatambua kwa nini waasi wanatumia bendera ya King Idris if they are really for democracy?

Like I said on the outset, Gaddafi is a terrible tyrant. That does not give the rebels a free pass.

The west has it's own agenda to see Gaddafi go and the rebels in power, that is why they are quick to recognise the rebels and paint them with the oversimplified brush of "freedom fighters" as disgraced as they are (lying about capturing Gaddafi sons, wanton waste of ammunition ,killing et).

While I don't exactly buy into the "Gaddafi is an African hero, and the rebels are Al-Qaeda and agents of western imperialism" per se ( what a contradiction) I also don't buy into the notion that the rebels are freedom fighters on a par with the then ANC and deserve a free pass and unmitigated recognition.

If making a public position was not required, we could have done better with a wait and see approach, not disclosing anything publicly.

As Dr. Kisinger had it, being noncommitatnt has a lot to do with successful diplomacy.
It makes sense,i aggree with this analysis.
 
huyo balozi wa Libya anatetea masalhi yake. nakumbuka alishiriki maandamno kuunga mkono utawala wa Gadaffi mwanzoni kabisa wakati mgogoro ndio unaanza. maandamano yaliishia viwanja vya Biafra, Kinondoni, Dsm. sasa kaona jamaa kan'goka ndio anajifanya anawaunga mkono. ni unafiki mkubwa!
<br />
<br />

ni mtumishi wa serikali, lazima atetee yeyote inayoingia madarakani.
 
Kwa heshima ya kipekee Mzee Mwanakijiji,

Ninadhani unaijua vema siasa/diplomasia za mataifa ya ulimwengu zikiwemo hizo za Libya. Nina amini kwa weledi wako uliotukuka katika nyanja hizi unakijua vizuri sana chanzo haswa cha mgogoro Walibya. Iweje leo uutamkie ulimwengu kuwa, kwa msimamo iliotoa Tanzania wa kutowatambua "wahuni wa Bengharz" ingawa kwa sababu zisizo na hoja nzito sana ila zenye ujumbe uliofichika, kuwa Tanzania ilikuwa rafiki wa Gaddaf wala si Walibya. Libya ni ya sehemu ya Afrika na kama kweli ulikuwa unaitakia mema Afrika huwezi kushangilia machafuko yaliyotokea katika nchi za kaskazini mwa afrika, vivyo hivyo huwezi kusema Tanzania imetia aibu kwa msimamo wake juu ya Libya. Mbali na mapungufu yake kwa kiasi Serikali imeonyesha kukerwa na mwenendo wa mambo huko Libya na inajari Umoja, Amani, Maendeleo ya msingi kwa bara la Afrika na waafrika kwa ujumla. Kama unafikiria uhuru wa Afrika huwezi kufikiria kuwatambua "wahuni wa Bengarz" wakisaidiwa na 'nAtO' kwa kuazimia kuanza kujiibia wenyewe rasilimali zao ambazo zingewasaidia kuimarisha uchumi wa nchi yao. Sijawahi kuhoji mada zako, kwani huwa unaandika mambo yanayoelekeza kujikwamua kwa kila hali kwa kila rika, lakini hii imenishtua kidogo Mzee Mwanakijiji, kwani napata shida kuelewa msimamo wako juu ya mstakabali wa maendeleo ya Afrika iliyo huru. Nina imani utakuwa na nafasi ya kulitolea ufafanuzi jambo hili.

Ninajitambulisha kama Mwafrika wa Tanzania.

Naomba nichangie; Inawezekana kweli serikali yetu, kama ambavyo wote tungependa iwe, inajali Umoja, Amani, na Maendeleo. Lakini nchi yoyote hata kama ingekuwa na amani au maendeleo makubwa kiasi gani bila watawala kuruhusu "UHURU WA FIKRA" kwa wananchi wao ni kazi bure. Na uhuru huu, au demokrasia ya kweli, ndicho Gadafi alishindwa/alikataa kuwapa watu wake.

UHURU bila FIKRA HURU ni kazi bure; ni udikteta. Kwa nini sehemu kubwa ya wananchi wa Libya wameungana na waasi na NATO (japo NATO pengine ina agenda zake nyingine) against Gaddafi anayeaminika kuwapatia wananchi wake ASALI na MAZIWA? Jibu lake ni neno moja tu - DEMOKRASIA.
 
Wakuu zangu Membe yuko sawa kabisa. hatuwezi kuitambua serikali ya Wanamapinduzi ambao hawana UONGOZI.. Hadi pale watakapo unda uongozi wao ndipo tunaweza kusema tunawatambua chama so and so kikiongozwa na fulani.. Hata wakati wa Biafra, South Afrika, Zimbabwe, Msumbiji kote tulivitambua vyama fulani chini ya uongozi fulani kabla kabisa ya vyama hivyo kupata uhuru, na ndivyo tuliwapa support toka mwanzo wa harakati zao hadi wanapata Uhuru lakini huko Libya picha haijakaa vizuri kabisa.. Hakuna chama wala hakuna makubaliano baina ya hao Wanamapinduzi ktk uongozi wa Mapinduzi haya na nawahakikishia kwamba mchezo bado mbichi kabisa!...

Tufanye subira kwani case ya Libya sio sawa kabisa na case ya South Sudan na tufahamu kwamba waliotangulia kuwatambua hawa jamaa wana interest zao tayari na walizipigania kama Nyerere alivyowaunga mkono wanamapinduzi wengine..
 
Ccm wasiwasi unawasumbuwa, na ndicho kinachowafanya washindwe mambo ya siasa za nje, hiyo sio sababu walio wengi wameshasema
awaridhiki na utawala wa kimabavu aliokuwa akiufanya Ghaddafi kwa muda wa miaka arobaini na mbili aliyokuwa madarakani kutawala nchi yeye pamoja na watoto wake na kuelekea kulithishana utawala. Matumizi mabaya ya fedha, mauaji yasiyokuwa na kikomo na ukandamizi wa demokrasia
Akumbuke wakati anampindua mfalme wa Libya mwaka 1969 kwa ahadi ya kuleta mazuri kwa Walibya lakini aligeuka na kuwa yeye mfalme zaidi
ya wafalme wote duniani, hapo ccm fadhila ndio inawasumbuwa na madeni na uwekezaji wa kiufisadi aliowekeza nchini. ccm wapo katika kusikilia
wakisikia ameuwawa au kukamatwa ndio maamuzi yao yatatoka,
 
Ziara ya mwisho ya kiwewe na mende kule Libya , Gaddafi aliwalipia gharama zote za safari yao , hicho ndio kigugumizi ya mende kuacha kuongea ukweli sasa wanatafuta pa kutokea kuonesha kuwa wapo pamoja nae , Daaaaaaa aibu ni bora wangekaa kimya tu kama museven !
 
Membe yuko sawa kabisa. Utawatambuaje waasi. Mi ningeona vema watanzania tuache woga kwani hatuwezi ishi bila misaada ya western. isitoshe wakileta lonolongo tunakatisha dili ya Ur... na madini. Hatuwezi kukubali udhalimu waziwazi kwa ajili ya njaa za siku moja. Kama NATO wana huruma waende somalia, palestina, kongo na syria na siku zile Rwanda. Mapinduzi yanaonekana hayakuwa na Timing sawasawa ingawa it was time for change. Wale waliporwa ufalme wanautaka wala si demokrasia na NATO hailindi walibya bali yalinda makampuni yake libya. Unless mzee aliomba wakae mezani muda mrefu sana.
 
Ccm wasiwasi unawasumbuwa, na ndicho kinachowafanya washindwe mambo ya siasa za nje, hiyo sio sababu walio wengi wameshasema
awaridhiki na utawala wa kimabavu aliokuwa akiufanya Ghaddafi kwa arobaini na mbili aliyokuwa madarakani kutawala nchi yeye pamoja na
watoto wake na kuelekea kulithishana utawala katika muda wa miaka arobaini na mbili aliyokuwa madarakani. matumizi mabaya ya fedha
na mauaji yasiyokuwa na kikomo na uikandamizi wa Demokrasia. Pili fadhila zinawasumbua ccm pamoja na madeni na uwekezaji wa kiufisadi
aliowekeza nchini, ccm wako katika kusikilizia wakisikia kakamatwa au kauliwa mtasikia kauli ya serikali.

If any political party in Tanzania will take advantage on situation in Libya by interpolating with our own situation, they will be short sighted. We are looking for a political party which knows western politics and how to side with there ideology.
 
Hili jamani wana-JF mnategemea kweli serikali yetu iwe na strong decision juu ya Libya wakata imeshindwa kufanya strong decision katika matatizo yetu madogo madogo ya humu ndani?

Membe pamoja na kuwa waziri wa mambo ya nje bado amekuwa mtu hasije juwa siasa ya kimataifa inafanywa vipi! wamebaki kushangaa na kulala. Kama kweli serikali yetu ilikuwa na maamuzi yoyote ya kumuunga mkono Qadhaffi walipaswa kuyafanya mapema na kuweka msimamo wao wazi mbele ya Jumuiya ya kimaifa kwa sababu imara ambazo zinaeleweka.

Angalia wakati wanasuasua kutoa msimamo wao juu Qadhaffi US tayari walimbia wakanunu Dowans, watu wetu wa security wamelala wanakoroma na mpaka leo hwaoni wala hawajui madhara ya kampuni ya US kuinunua Dowans! Haya tusubiri mwisho wa siku tutaona matunda ya hiyo kampuni ya US kununua Dowans kama Qadhaffi alivyoona matunda ya kushika urafiki na UK baada ya kulipua ndege ya US.
 
Fikra mgando. Maamuzi ya kutotambua waasi yasingeweza kuchukuliwa kabla ya utawala wa Gaddafi kuanguka na hili limetokea siku chache tu zilizopita. Pili, uamuazi huu umezingatia pia kikao cha baraza la usalama la AU ambalo Tanzania nayo ilishiriki. Tatu, suala la waasi kuamua kubadilisha alama za nchi yao bila kufuata utaratibu na kama Vienna Convention inavyosema nalo si la kuliangalia kwa jicho jepesi. Hivi kuna ayaejua ni nani anaongoza Libya sasa hivi? Utatambuaje kikundi cha waasi ambao bado hawajashika hatamu za utawala zaidi tu ya kuteka miji na majengo?
Unataka kutuambia kwa Tanzania kufuata taratibu za Vienna convention ina akili sana kuliko nchi nyingi duniani zilizowatambua waasi, mtakaa hivyo hivyo na umasikini wakati wenzenu wakichangamkia opportunities kwa haraka kadri zinavyopatikana.
 
Does it really matter if the Tanzanian leadership support the NTC or not?
Muda wa kumuokoa rafiki yao ulikuwepo and they did nothing. Wananchi wa Benghazi wamepiga kelele kuomba msaada hawa wakubwa wakasema 'we are lying low'. Chicken!
 
Does it really matter if the Tanzanian leadership support the NTC or not?
Muda wa kumuokoa rafiki yao ulikuwepo and they did nothing. Wananchi wa Benghazi wamepiga kelele kuomba msaada hawa wakubwa wakasema 'we are lying low'. Chicken!
Duh mkuu wangu ama kweli nyani haoni kundule.. yaani matatizo tulokuwa nayo sisi unaanza kuizungumzia serikali hali sisi wenyewe ni sawa na Bangazi lakini tumeshindwa kuona makalio yetu, isipokuwa kutafuta mchawi.. Hii tabia itakwisha lini jamani...? Why blame the Government mnayoidharau, ambayo wengi wenu mnataka iondoke madarakani lakini kinachofanyika ni maneno matupu!
 
Back
Top Bottom