BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Membe: CCM inajimaliza
> Uchaguzi UVCCM Dar vituko
na Mwandishi Wetu | Tanzania Daima~Sauti ya Watu
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinajimaliza chenyewe kutokana na kuendekeza makundi ndani yake.
Alisema uzoefu alionao, unaonyesha kuwa vyama tawala haviondolewi madarakani na vyama vya upinzani, bali hujiondoa vyenyewe kwa kutokuwa makini na kuendekeza makundi, chuki, fitina, majungu na migogoro isiyo na tija.
Alisema kwa sasa CCM inatafunwa na makundi na kusababisha mgawanyiko miongoni mwa wanachama, jambo ambalo likiachwa liendelee, linaweza kukimaliza chama hicho tawala.
Membe alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Dar es Salaam, uliofanyika jana katika Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam.
Katika uchaguzi huo uliotawaliwa na vituko vya kila aina, mtoto wa Mbunge wa Viti Maalumu, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi, aliibuka mshindi na kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, hivyo kupata nafasi ya kuingia katika Baraza Kuu la UVCCM.
Alisema ndani ya CCM kuna makundi yanayokua kila kukicha, hususan ndani ya jumuiya za chama na kushusha heshima ya chama hicho.
Mbali ya UVCCM, jumuiya nyingine za CCM ni Umoja wa Wanawake (UWT) na Jumuiya ya Wazazi, ambazo mwaka huu, zinafanya uchaguzi wa viongozi wao.
Membe ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mkutano huo, uliofanyika kwa ajili ya kuwachagua viongozi wa UVCCM, Mkoa wa Dar es Salaam, alionyesha kutokufurahishwa na makundi ndani ya chama hicho, ambayo alisisitiza yamesababisha baadhi ya watu kutokukubaliana na matokeo ya uchaguzi ndani ya chama hicho na kuleta mgawanyiko.
Aliwataka wana CCM kutambua kuwa maadui wa CCM wamo ndani ya chama na si nje ya chama hicho, kinachoongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.
Vyama tawala haviwezi kuondolewa madarakani au kuuawa na vyama vya upinzani ila vinajiua vyenyewe, angalia Kenya, KANU ilijimaliza yenyewe na hata CCM tukiendekeza makundi, tutajimaliza wenyewe, alisema Waziri Membe.
Historia inaonyesha kuwa jumuiya za chama ndizo zina nguvu, lakini kama jumuiya hizo zinaanza kukitafuna chama kwa kukipinga au wanachama kutafunana wenyewe kwa wenyewe ni dhahiri kuwa chama hakiwezi kupambana na wapinzani, alisema Membe.
Alisema CCM ina changamoto kubwa mbele yake, ikiwa ni pamoja na wanachama kutokukubaliana na baadhi ya mambo ndani ya chama, ikiwemo majungu, chuki, kugeukana na makundi ambayo yanashusha heshima ya chama.
Wapinzani si maadui, maadui wamo ndani ya chama, ugomvi, chuki, majungu, kutukanana, kudhalilishana na kutokukubali kushindwa katika uchaguzi, hao ndio maadui wakubwa wa chama, alisema Waziri Membe.
Baada ya ufunguzi huo, uchaguzi huo ulifanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi na maofisa usalama.
Katika uchaguzi huo, wajumbe walipiga kura kumchagua Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa, Makamu wake pamoja na wajumbe watano wa Mkutano Mkuu wa Taifa.
Wagombea katika nafasi ya Mwenyekiti alikuwa Glorius Luoga, Hamisi Kifimbo na Said Ntimizi.
Kabla ya kutangazwa kwa matokeo kamili, Ntimizi ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Tatu Ntimizi, alikuwa na kila dalili za ushindi kutokana na kuungwa mkono na wajumbe wengi ambao hawakuweza kuficha hisia zao tangu mwanzo.
Katika kuthibitisha hilo, baadhi ya wafuasi wake walianza kunywa bia nje ya Ukumbi wa Karimjee, kwa madai kuwa walikuwa wakishangilia ushindi wa Ntimizi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam.
Moja ya vituko vilivyoonekana katika uchaguzi huo ni kurudiwa kwa kazi ya upigaji kura kwa nafasi ya mwenyekiti bila sababu za msingi kutolewa.
Hali hiyo iliwafanya wafuasi wa Ntimizi na Luoga waliokuwa wakichuana vikali, kurushiana maneno makali na lugha chafu ndani ya ukumbi huo kiasi cha polisi kuingilia kati.
Baadhi ya wajumbe waliiambia Tanzania Daima kuwa kura hizo zimelazimika kurudiwa baada ya kura za awali za Ntimizi na Luoga kugongana.
Baada ya kumaliza kupiga kura za nafasi ya mwenyekiti kwa mara ya pili, wajumbe hao waliendelea kuwachagua wajumbe wa uwakilishi wa jumuiya mbalimbali.
Hata hivyo, wakati wajumbe ndani ya ukumbi wakiendelea kupiga kura za wajumbe wawakilishi, nje ya ukumbi wajumbe wengine walikuwa wameanza kupiga kelele za kushangilia na kunywa bia, wakicheza kwa furaha kuwa wamemaliza kazi waliyokuja kuifanya ya kumtangaza Ntimizi kuwa mwenyekiti.
Mwenyekiti tunaye siku nyingi, tumekuja kumbatiza tu aitwe mwenyekiti, ameshashinda hata kabla kura hazijahesabiwatumefanya kweli walisikika baadhi ya wajumbe hao huku wakipongezana kwa kunywa bia.
Hali iliendelea kuwa ya kushangilia nje ya ukumbi, makelele, na wengine wakitukana kuwa Luoga amewaletea polisi kuwasimamia kwenye uchaguzi wakati wao hawana vurugu.
Wakati wajumbe wa mkutano huo wakipiga kura, Nape Nnauye aliyevuliwa uanachama wa UVCCM, hivyo kukosa sifa ya kugombea na kupiga kura, alisema hatua yake ya kusema ukweli kuhusu mradi wa jengo la UVCCM, ndiyo iliyomgharimu.
Alisema kutokana na uamuzi huo na kuchelewa kutolewa uamuzi wa rufaa yake, kunamfanya ashindwe kutumia haki yake ya kupiga na kupigiwa kura katika uchaguzi huo.
Nape alienguliwa na Baraza Kuu la UVCCM kwa madai kuwa alisema uongo kuhusu mradi wa jengo la makao makuu ya umoja huo, kwamba uligubikwa na harufu ya rushwa na kumtaka Mwenyekiti anayemaliza muda wake, Dk. Emmanuel Nchimbi, Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamani la UVCCM, Edward Lowassa na Kaimu Katibu Mkuu wa umoja huo, Francis Isaac, kuwajibika.
> Uchaguzi UVCCM Dar vituko
na Mwandishi Wetu | Tanzania Daima~Sauti ya Watu
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinajimaliza chenyewe kutokana na kuendekeza makundi ndani yake.
Alisema uzoefu alionao, unaonyesha kuwa vyama tawala haviondolewi madarakani na vyama vya upinzani, bali hujiondoa vyenyewe kwa kutokuwa makini na kuendekeza makundi, chuki, fitina, majungu na migogoro isiyo na tija.
Alisema kwa sasa CCM inatafunwa na makundi na kusababisha mgawanyiko miongoni mwa wanachama, jambo ambalo likiachwa liendelee, linaweza kukimaliza chama hicho tawala.
Membe alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Dar es Salaam, uliofanyika jana katika Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam.
Katika uchaguzi huo uliotawaliwa na vituko vya kila aina, mtoto wa Mbunge wa Viti Maalumu, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi, aliibuka mshindi na kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, hivyo kupata nafasi ya kuingia katika Baraza Kuu la UVCCM.
Alisema ndani ya CCM kuna makundi yanayokua kila kukicha, hususan ndani ya jumuiya za chama na kushusha heshima ya chama hicho.
Mbali ya UVCCM, jumuiya nyingine za CCM ni Umoja wa Wanawake (UWT) na Jumuiya ya Wazazi, ambazo mwaka huu, zinafanya uchaguzi wa viongozi wao.
Membe ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mkutano huo, uliofanyika kwa ajili ya kuwachagua viongozi wa UVCCM, Mkoa wa Dar es Salaam, alionyesha kutokufurahishwa na makundi ndani ya chama hicho, ambayo alisisitiza yamesababisha baadhi ya watu kutokukubaliana na matokeo ya uchaguzi ndani ya chama hicho na kuleta mgawanyiko.
Aliwataka wana CCM kutambua kuwa maadui wa CCM wamo ndani ya chama na si nje ya chama hicho, kinachoongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.
Vyama tawala haviwezi kuondolewa madarakani au kuuawa na vyama vya upinzani ila vinajiua vyenyewe, angalia Kenya, KANU ilijimaliza yenyewe na hata CCM tukiendekeza makundi, tutajimaliza wenyewe, alisema Waziri Membe.
Historia inaonyesha kuwa jumuiya za chama ndizo zina nguvu, lakini kama jumuiya hizo zinaanza kukitafuna chama kwa kukipinga au wanachama kutafunana wenyewe kwa wenyewe ni dhahiri kuwa chama hakiwezi kupambana na wapinzani, alisema Membe.
Alisema CCM ina changamoto kubwa mbele yake, ikiwa ni pamoja na wanachama kutokukubaliana na baadhi ya mambo ndani ya chama, ikiwemo majungu, chuki, kugeukana na makundi ambayo yanashusha heshima ya chama.
Wapinzani si maadui, maadui wamo ndani ya chama, ugomvi, chuki, majungu, kutukanana, kudhalilishana na kutokukubali kushindwa katika uchaguzi, hao ndio maadui wakubwa wa chama, alisema Waziri Membe.
Baada ya ufunguzi huo, uchaguzi huo ulifanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi na maofisa usalama.
Katika uchaguzi huo, wajumbe walipiga kura kumchagua Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa, Makamu wake pamoja na wajumbe watano wa Mkutano Mkuu wa Taifa.
Wagombea katika nafasi ya Mwenyekiti alikuwa Glorius Luoga, Hamisi Kifimbo na Said Ntimizi.
Kabla ya kutangazwa kwa matokeo kamili, Ntimizi ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Tatu Ntimizi, alikuwa na kila dalili za ushindi kutokana na kuungwa mkono na wajumbe wengi ambao hawakuweza kuficha hisia zao tangu mwanzo.
Katika kuthibitisha hilo, baadhi ya wafuasi wake walianza kunywa bia nje ya Ukumbi wa Karimjee, kwa madai kuwa walikuwa wakishangilia ushindi wa Ntimizi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam.
Moja ya vituko vilivyoonekana katika uchaguzi huo ni kurudiwa kwa kazi ya upigaji kura kwa nafasi ya mwenyekiti bila sababu za msingi kutolewa.
Hali hiyo iliwafanya wafuasi wa Ntimizi na Luoga waliokuwa wakichuana vikali, kurushiana maneno makali na lugha chafu ndani ya ukumbi huo kiasi cha polisi kuingilia kati.
Baadhi ya wajumbe waliiambia Tanzania Daima kuwa kura hizo zimelazimika kurudiwa baada ya kura za awali za Ntimizi na Luoga kugongana.
Baada ya kumaliza kupiga kura za nafasi ya mwenyekiti kwa mara ya pili, wajumbe hao waliendelea kuwachagua wajumbe wa uwakilishi wa jumuiya mbalimbali.
Hata hivyo, wakati wajumbe ndani ya ukumbi wakiendelea kupiga kura za wajumbe wawakilishi, nje ya ukumbi wajumbe wengine walikuwa wameanza kupiga kelele za kushangilia na kunywa bia, wakicheza kwa furaha kuwa wamemaliza kazi waliyokuja kuifanya ya kumtangaza Ntimizi kuwa mwenyekiti.
Mwenyekiti tunaye siku nyingi, tumekuja kumbatiza tu aitwe mwenyekiti, ameshashinda hata kabla kura hazijahesabiwatumefanya kweli walisikika baadhi ya wajumbe hao huku wakipongezana kwa kunywa bia.
Hali iliendelea kuwa ya kushangilia nje ya ukumbi, makelele, na wengine wakitukana kuwa Luoga amewaletea polisi kuwasimamia kwenye uchaguzi wakati wao hawana vurugu.
Wakati wajumbe wa mkutano huo wakipiga kura, Nape Nnauye aliyevuliwa uanachama wa UVCCM, hivyo kukosa sifa ya kugombea na kupiga kura, alisema hatua yake ya kusema ukweli kuhusu mradi wa jengo la UVCCM, ndiyo iliyomgharimu.
Alisema kutokana na uamuzi huo na kuchelewa kutolewa uamuzi wa rufaa yake, kunamfanya ashindwe kutumia haki yake ya kupiga na kupigiwa kura katika uchaguzi huo.
Nape alienguliwa na Baraza Kuu la UVCCM kwa madai kuwa alisema uongo kuhusu mradi wa jengo la makao makuu ya umoja huo, kwamba uligubikwa na harufu ya rushwa na kumtaka Mwenyekiti anayemaliza muda wake, Dk. Emmanuel Nchimbi, Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamani la UVCCM, Edward Lowassa na Kaimu Katibu Mkuu wa umoja huo, Francis Isaac, kuwajibika.