Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Huyu waziri ambaye inasemekana ni ndugu wa mbali wa mkuu wa kaya ni magumashi kabisa, kama alivyo huyo jamaa yake. Wote wawili ni mafundi wakubwa wa kupasia mipira, hawataki kukaa nayo.
Mpira wa sakata la meli kisha upasia kwa UN na EU. Kuina mengine bado anatafuta namna ya kupasi kama vile lile la hela za Libya.
Lakini kuna hili la vigogowaliowekewa mabilioni katika mabenki ya Uswisi ambayo mamlaka za nchi hiyo ya Ulaya inayo majina ya vigoigo sita wa hapa TZ. Kwa kuwa yeye ni waziri wa nje tunaomba alichangamkie hili, kama vile alivyolichangamkia la hela za rada -- si katika kutaka hela zirejeshwe hapa -- kwani hizo hela si mali ya wananchi wa TZ, ni mali ya makampuni ya nje waliowawekea vigogo wetu.
Kitu tunachotaka kutoka kwa Membe ni kupata hayo majina ya vigogo na kuyatangaza hadharani. Bila shaka hayo majina yameshakabidhiwa serikali ya TZ kwani itakuwa haina mantiki kwa mamlaka za benki za Uswisi kutangaza kuwepo kwa majina ya wala rushwa hao halafu iyakalie majina isiyakabidhi kwa nchi husika. haitaingia akilini hii!
Jee, Membe anaweza kuonyesha 'umahiri' wake na ubavu kwa kuitisha waandishi wa habari na kuyatangaza majina hayo? Sana sana atafanya danadana tu kwamba bado majina hayajapatikana.
Hawezi kabisa!!! na hapo ndiyo umagumashi wake utadhihirika.
Mpira wa sakata la meli kisha upasia kwa UN na EU. Kuina mengine bado anatafuta namna ya kupasi kama vile lile la hela za Libya.
Lakini kuna hili la vigogowaliowekewa mabilioni katika mabenki ya Uswisi ambayo mamlaka za nchi hiyo ya Ulaya inayo majina ya vigoigo sita wa hapa TZ. Kwa kuwa yeye ni waziri wa nje tunaomba alichangamkie hili, kama vile alivyolichangamkia la hela za rada -- si katika kutaka hela zirejeshwe hapa -- kwani hizo hela si mali ya wananchi wa TZ, ni mali ya makampuni ya nje waliowawekea vigogo wetu.
Kitu tunachotaka kutoka kwa Membe ni kupata hayo majina ya vigogo na kuyatangaza hadharani. Bila shaka hayo majina yameshakabidhiwa serikali ya TZ kwani itakuwa haina mantiki kwa mamlaka za benki za Uswisi kutangaza kuwepo kwa majina ya wala rushwa hao halafu iyakalie majina isiyakabidhi kwa nchi husika. haitaingia akilini hii!
Jee, Membe anaweza kuonyesha 'umahiri' wake na ubavu kwa kuitisha waandishi wa habari na kuyatangaza majina hayo? Sana sana atafanya danadana tu kwamba bado majina hayajapatikana.
Hawezi kabisa!!! na hapo ndiyo umagumashi wake utadhihirika.