Uchaguzi 2020 Membe, ACT Wazalendo kukata pumzi na unafiki wa Zitto

Sep 8, 2020
67
133
MEMBE, ACT WAZALENDO KUKATA PUMZI KAMPENI NA UNAFIKI WA ZITTO

Na Mwamba wa Kaskazini

Jana au juzi nimesoma andiko la vijana wa ACT wakiuliza swali muhimu sana ambalo naona limeibua mambo ndani ya Chama hicho kuhusu yu wapi mgombea wao wa Urais Benard Membe?

Mwanadiplomasia anayeelezwa kuwa si tu mbobezi na aliyepokewa kwa mbwembwe zote ACT, bali mwanamikakati mwandamizi ambaye sasa amejikuta hana ushawishi wala uwezo wa kufanya kampeni hata anazidiwa na Mzee wetu wa ubwabwa, Hashim Rungwe Sipunda

Nini kimetokea? Vijana wa ACT jana wanetupa hinti kidogo kuelewa hali ya mambo; ni ajabu kuona Zitto Kabwe anayejiita Kiongozi wa Chama akiendesha kampeni za kidikteta za "one-man-show" yaani akijiidhinishia mamilioni ya Chama aonekane yeye kuliko mgombea Urais bwana Membe.

Maana wakati mgombea Urais Membe amekwama hana fedha na amesema hadharani pale Airport, inaonekana Zitto amemtumia Membe kupata hela na kuzitumbua akipita nchi nzima huku akielekeza zaidi kampeni zake kwa wadada ambao ACT imewaingiza kwa wingi na ambao siri yao tutaijadili hapa kesho Jumatano jioni maana kuna jambo kubwa litatokea siku hiyo mchana kuhusu pembetatu hii ya uharamu na uharamia ndani ya ACT.

Zitto amedhihirisha umangimeza wa ndani ya ACT na udikteta uliokithiri unaoashiria 'very poor governance' ndani ya ACT. Hili la kwanza.

La pili mtu mmoja amepata kunihadithia maisha ya Zitto Kabwe kwa kumweleza kuwa si tu ni kiongozi mnafiki bali ni salesman. Mtanisaidia Kiswahili chake.

Na hapa unaiona hiyo. Ameanza kutaka kumuuza Mzee Membe rejareja kwa Chadema. Bila shaka katika mpango huo Zitto atapiga dili Yaani yeye na Maalim Seif wanamtaja na kumfagilia Lissu zaidi ya mgombea wao Membe!

Maskini Membe, yuko kwenye mtanziko mkubwa alipo sasa; ameingia chama kilichokuwa na mbwembwe kwenye twitter na kujikuta mtaani kumbe hakipo na wala hakiwezi kuwepo!!!

Sasa anajikuta anaelekea kuuzwa eti ajitoe amuunge mkono Lissu; maskini yani ni hadithi ya kusikitisha ya kutoka Waziri mbobezi, mwanadiplomasia nguli hadi kuongozwa na Lissu, mtu ambaye hata ukuu wa Idara ya sheria pale ndani ya Chadema aliutumia kidikteta kwa kiwango cha kubinya demokrasia na kusababisha akina Zitto kufukuzwa ndani ya Chama hicho walipotoa maoni ya kukosoa Chama na mwenendo wa kiKIAKIA wa Mwenyekiti wao Freeman Mbowe.

Namshauri Membe, akatae ujinga huu, akatae unafiki huu wa kuahidiwa sapoti na Zitto kuwa wangekuwa na kampeni ya kijanja hadi hali sasa kubadilika Zitto kujisainisha hela yeye peke yake na sasa anataka kumuuza mbobezi Membe kwa wahuni wa Chadema.

Nashauri tena, kwa unafiki huu na udikteta anaofanyiwa ndani ya ACT, ni kheri Mzee wetu mbobezi akahuisha kale kaleseni kake kauwindaji, akarejea Londo kwenda kuwinda, akipumzika kusubiri round nyingine ya kikao cha Bodi, aende zake Dubai. Ni ushauri tu.

Niite Mwamba (sema mara tatu) wa Kaskazini
 
Membe anajua fika kuwa Nyota yake katika uchaguzi huu imefifia sana sana Nyota inayowaka ni ya Tundu Lissu
 
Membe anajua fika kuwa Nyota yake katika uchaguzi huu imefifia sana sana Nyota inayowaka ni ya Tundu Lissu
Membe kachezewa faulu kubwa kwenye pesa zake zote wamempora na rafiki zake na baadhi ya ndugu zake wamefungiwa A/c zao
 
MEMBE, ACT WAZALENDO KUKATA PUMZI KAMPENI NA UNAFIKI WA ZITTO

Na Mwamba wa Kaskazini

Jana au juzi nimesoma andiko la vijana wa ACT wakiuliza swali muhimu sana ambalo naona limeibua mambo ndani ya Chama hicho kuhusu yu wapi mgombea wao wa Urais Benard Membe?

Mwanadiplomasia anayeelezwa kuwa si tu mbobezi na aliyepokewa kwa mbwembwe zote ACT, bali mwanamikakati mwandamizi ambaye sasa amejikuta hana ushawishi wala uwezo wa kufanya kampeni hata anazidiwa na Mzee wetu wa ubwabwa, Hashim Rungwe Sipunda

Nini kimetokea? Vijana wa ACT jana wanetupa hinti kidogo kuelewa hali ya mambo; ni ajabu kuona Zitto Kabwe anayejiita Kiongozi wa Chama akiendesha kampeni za kidikteta za "one-man-show" yaani akijiidhinishia mamilioni ya Chama aonekane yeye kuliko mgombea Urais bwana Membe.

Maana wakati mgombea Urais Membe amekwama hana fedha na amesema hadharani pale Airport, inaonekana Zitto amemtumia Membe kupata hela na kuzitumbua akipita nchi nzima huku akielekeza zaidi kampeni zake kwa wadada ambao ACT imewaingiza kwa wingi na ambao siri yao tutaijadili hapa kesho Jumatano jioni maana kuna jambo kubwa litatokea siku hiyo mchana kuhusu pembetatu hii ya uharamu na uharamia ndani ya ACT.

Zitto amedhihirisha umangimeza wa ndani ya ACT na udikteta uliokithiri unaoashiria 'very poor governance' ndani ya ACT. Hili la kwanza.

La pili mtu mmoja amepata kunihadithia maisha ya Zitto Kabwe kwa kumweleza kuwa si tu ni kiongozi mnafiki bali ni salesman. Mtanisaidia Kiswahili chake.

Na hapa unaiona hiyo. Ameanza kutaka kumuuza Mzee Membe rejareja kwa Chadema. Bila shaka katika mpango huo Zitto atapiga dili Yaani yeye na Maalim Seif wanamtaja na kumfagilia Lissu zaidi ya mgombea wao Membe!

Maskini Membe, yuko kwenye mtanziko mkubwa alipo sasa; ameingia chama kilichokuwa na mbwembwe kwenye twitter na kujikuta mtaani kumbe hakipo na wala hakiwezi kuwepo!!!

Sasa anajikuta anaelekea kuuzwa eti ajitoe amuunge mkono Lissu; maskini yani ni hadithi ya kusikitisha ya kutoka Waziri mbobezi, mwanadiplomasia nguli hadi kuongozwa na Lissu, mtu ambaye hata ukuu wa Idara ya sheria pale ndani ya Chadema aliutumia kidikteta kwa kiwango cha kubinya demokrasia na kusababisha akina Zitto kufukuzwa ndani ya Chama hicho walipotoa maoni ya kukosoa Chama na mwenendo wa kiKIAKIA wa Mwenyekiti wao Freeman Mbowe.

Namshauri Membe, akatae ujinga huu, akatae unafiki huu wa kuahidiwa sapoti na Zitto kuwa wangekuwa na kampeni ya kijanja hadi hali sasa kubadilika Zitto kujisainisha hela yeye peke yake na sasa anataka kumuuza mbobezi Membe kwa wahuni wa Chadema.

Nashauri tena, kwa unafiki huu na udikteta anaofanyiwa ndani ya ACT, ni kheri Mzee wetu mbobezi akahuisha kale kaleseni kake kauwindaji, akarejea Londo kwenda kuwinda, akipumzika kusubiri round nyingine ya kikao cha Bodi, aende zake Dubai. Ni ushauri tu.

Niite Mwamba (sema mara tatu) wa Kaskazini
Membe sasa hana pesa, pesa yake yote imepigwa pini kokote ilipo isimfikie yupo hoi hana kitu yupo anashinda akinung’unika mda wote.
 
Ukimpelekea hata buku membe anakushukuru sana kwani hana pesa kabsa wamemkombea kila kitu kabakia mtupu akinung’unika tu
 
CCM hamuwezi play fair?
Hizi dirty tactics za nini?
Chadema na hivyo vyama vingine hawafanyi dirty tricks? Fair play if is done on your side but what about others? Which country plays fair election? Hapa kazi tu!

 
1602184089315.png
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom