Meli ya Iran yachanganyikiwa na kufyatulia nyingine makombora na kuua wanajeshi 19 wa Iran

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,517
47,756
Japo Waajemi wenyewe wanasema ilikua ajali kazini.

One Iranian warship accidentally struck another with a missile during an exercise, killing 19 sailors and wounding 15 others, Iran's navy said on Monday.

The incident took place during training in the Gulf of Oman, a sensitive waterway that connects to the Strait of Hormuz through which about a fifth of the world's oil passes. Iran regularly conducts exercises in the area.

=======

The incident took place during training in the Gulf of Oman, a sensitive waterway that connects to the Strait of Hormuz through which about a fifth of the world's oil passes. Iran regularly conducts exercises in the area.

According to the Qatar-based Al Jazeera network, an Iranian destroyer accidentally fired a C-802 Noor missile at a sister warship during military exercises.

"The incident took place in the perimeter of Iran's southern Bandar-e Jask port on the Gulf of Oman during Iranian Navy drills on Sunday afternoon, in which 19 sailors were killed and 15 others were injured," state TV said, quoting the navy.

The Konarak, a Hendijan-class support ship, which was taking part in the exercise, was too close to a target during an exercise on Sunday when the incident happened, the reports said. The vessel had been putting targets out for other ships to target.

The friendly fire incident happened near the port of Jask, some 1,270 kilometers (790 miles) southeast of Tehran, in the Gulf of Oman, state TV said.

A local hospital admitted 12 sailors and treated another three with slight wounds, the state-run IRNA news agency reported.

Iranian media said the Konarak had been overhauled in 2018 and was able to launch sea and anti-ship missiles. The Dutch-made, 47-meter (155-foot) vessel was in service since 1988 and had a capacity of 40 tons. It usually carries a crew of 20 sailors.

Iranian media rarely report on mishaps during its exercises, signaling the severity of the incident. This incident also comes amid months of heightened tensions between Iran and the US since President Donald Trump unilaterally withdrew from Tehran's nuclear deal with world powers in 2018 and imposed crushing sanctions on the country.


=====

Wanamaji 19 wameuawa na wengine 15 wakajeruhiwa katika tukio la ajali lililohusisha meli za kijeshi za Iran katika Ghuba ya Oman, jeshi la Iran limesema.

Vyombo vya habari vya Iran vimesema kwamba meli hiyo kwa jina Konarak ilishambuliwa na kombora jipya lililokuwa likijaribiwa na meli ya kijeshi ya Frigate Jamaran wakati wa zoezi la kijeshi siku ya Jumapili.

The Konarak ilishambuliwa na kombpora jipya Jumapili mchana wakati wa zoezi la kijeshi katika maji ya Bandar-e Jask kusini mwa pwani kulingana na runinga ya taifa katika tovuti yake.

Wanamaji hao walisema kwamba meli hiyo ilivutwa hadi ufukweni na kwamba uchunguzi umeanza.

Kisa hicho kilitokea karibu na mkondo wa bahari ya hormuz , eneo muhimu la kimkakati ambapo kiwango kikubwa cha mafuta duniani hupitia.

Uchanganuzi wa mwandishi wa BBC Jonathan Marcus

Sio mara ya kwanza kwa jeshi la Iran kufanya makosa hayo.

Mwezi Januari , kitengo cha ulinzi wa angani kilirusha kumbora kutoka ardhini kikilenga kitu kisichojulikana, hatua ilioangusha ndege ya kampuni ya Ukrain na kuwaua wote waliokuwa wakiabiri ndege hiyo.

Makosa hayo yalifanyika wakati wa hali ya wasiwasi huku Iran ikisubiri kombora la kulipiza kisasi kutoka kwa Marekani.

Lakini tukio hilo la siku ya Jumapili lilifanyika katika hali tofauti - wakati wa zoezi la wanamaji - na linaibua maswali mengi kuhusu uongozi na udhibiti na utaalam wa jeshi la wanamaji wa Iran.

Iran inataka kupanua operesheni zake na kuimarisha silaha katika meli zake, Frigate Jamaran ambayo ni miongoni mwa vyombo vilivyoundwa nchini humo ikitarajiwa kuweka rekodi mpya.

Lakini ni jeshi lisililotiliwa maanani . Ni jeshi la wanamaji wa Revolutionary Guard lenye boti zinazopiga doria katika eneo hilo ambalo linahusika mara kwa mara katika kuhangaisha na kuchunguza meli za Marekani na nyenginezo katika Ghuba hilo.

"Siku ya Jumapili jioni...wakati wa zoezi la wanamaji ambalo lilihusisha vyombo kadhaa vya wanamaji katika maji ya Jask and Chabahar , tukio moja lilifanyika likihusisha meli ya Konarak , na kuwaua baadhi ya wanajeshi jasiri wa jeshi hilo, wanamaji hao walisema katika taarifa siku ya Jumatatu.

Taarifa hiyo iliongezea kwamba meli hiyo ya Konarak ilikuwa imepelekwa katika bara moja kwa uchunguzi wa kiufundi, lakini haikutaja tukio la ajali hiyo.

Vyombo vya habari vya Iran awali vilikuwa vimeripoti kwamba meli ya Konarak ilishambuliwa kwa bahati mbaya na kombora moja lililifyatuliwa kutoka katika meli.

Meli hiyo ilishambuliwa baada ya kupita katika eneo ambalo kombora hilo lilikuwa likirushwa baada ya kushindwa kupita mbali, runinga ya serikali ilisema katika tovuti yake.

Chombo cha habari cha Tasnim kilituma ujumbe wa twitter kwa kiingereza kwamba Konarak ilizamishwa katika tukio hilo.

Kiliripoti kwamba meli hiyo iliharibiwa vibaya. Haijulikani kulikuwa na wanamaji wangapi ndani yake wakati huo.

Meli ya kivita ya Konarak ina urefu wa mita 47 na ilitenegenezwa nchini Uholanzi na kununuliwa na Iran kabla ya mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979.

BBC Swahili
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom