Meli iliyobeba magari 4,041 yatia nanga Dar es Salaam, magari 1105 yanabaki Tanzania

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,458
1.jpg
Bandari ya Dar es Salaam imeendeleaza rekodi ya kupokea meli kubwa, safari hii ikipokea yenye urefu wa mita 189.45 ikitokea nchini Japan, ikiwa na shehena ya magari 4,041 huku magari 1105 yakibaki Tanzania.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa ameziagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kuanza kutumia Bandari za nchi kavu zinazokidhi vigezo ili kupunguza msongamano wa magari bandarini.

Meli hiyo ‘Frontier Ace’ iliwasili jana Ijumaa Aprili 8, 2022 ikielezwa kuwa imewasili ikitokea Singapore kama kituo chake cha mwisho kabla ya kuwasili Dar baada ya safari ya siku 10.

Meli hiyo ilitengenezwa mwaka 2000 inatembea ikiwa na bendera ya Panama ina upana wa mita 33.2.

Baada ya kushusha mzigo Tanzania, inaelezwa kuwa magari 2,936 ni kwa ajili ya Nchi za DRC, Uganda, Zambia, Zimbabwe, Malawi na Afrika Kusini

Agosti 2021, bandari hiyo iliweka historia ya kupokea meli ya Tranquil Ace yenye urefu wa mita 199.95 na upana wa mita 32.2, ikiwa imebeba magari 3,743, ambapo asilimia 65 ya magari hayo ambayo ni 2,945 yalikuwa yakisafirishwa kwenye mataifa mengine wakati ni 798 yaliyobaki Tanzania.
Frontier Ace.jpg

Source: The Citizen
 
Nafikiri hii inaweza kua niche yetu kukusanya pesa kupitia uugazaji wa magari katika bandari yetu. Tuongeze ufanisi katika kuhakikisha magari yanatoka kwa muda nafuu. Kuwe na kodi na ushuru mwingine himilivu na unaofahamika.

Kazi ya transit itakua nzuri. Gari zote 2000 vijana wanasafirisha
 
Magari, adhabu mnaletewa tu

Mitozo ya parking, tochi &fine za traffic etc

Ova
 
Kama bandari ikisimamiwa vizuri si inaweza kuleta mapato ya kutosha tu na serikali ikapunguza mzigo kwenye mambo mengine kweli?

Hawafikirii hata kufanya subsidies kwenye mambo ya msingi kama mafuta ya kula, mafuta ya magari ili kumpunguzia mwananchi ugumu wa maisha?
 
Back
Top Bottom