Melchizedek na utata unaomzunguka

Mkuu hata sisi binadamu tunamuita Mungu ni Baba na Yesu ni kaka yetu ila Je hatuna baba wa kimwili??

Yohana 1:12
12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Wakolosai 1:15
15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

Anaitwa mwanaye sababu ana Roho wa Mungu ndani yake na sisi pia tunaitwa watoto wa Mungu sababu tuna Roho wake ndani yetu lakini sio Baba kimwili.

So Still Yesu hana Baba wala Mama coz alikuwepo kabla hata ya uumbaji ila huyo Maria alitumika kma njia ya kumleta duniani ila sio kwamba ndio alimzaa Yesu tokea dunia haijaumbwa.

So bado Yesu hana Baba wala Mama na anathibitisha hapa

Mathayo 12
46 Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye.
47 Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.
48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani?
49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!
50 Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu.

Bwana Zitto Junior hebu fafanua hili la Yesu kuitwa Mzaliwa wa kwanza wa viumbe wote, hii maana yake ni nini?
(Wakolosai 1:15 )

Pili unasema Yesu ana roho wa Mungu ndani yake na unasema pia na sisi pia tuna roho wa Mungu ndani yetu, Je utofauti wa Roho wa Mungu aliyemo ndani ya Yesu na yule aliyemo ndani yetu ni nini?
 
Bwana Zitto Junior hebu fafanua hili la Yesu kuitwa Mzaliwa wa kwanza wa viumbe wote, hii maana yake ni nini?
(Wakolosai 1:15 )

Pili unasema Yesu ana roho wa Mungu ndani yake na unasema pia na sisi pia tuna roho wa Mungu ndani yetu, Je utofauti wa Roho wa Mungu aliyemo ndani ya Yesu na yule aliyemo ndani yetu ni nini?
Mkuu kabla hatujatanua mada elewa hivi.
1. Yesu anaitwa mwana wa Mungu sio sababu alizaliwa kutoka viunoni kwa mtu bali sababu ana ROHO wa Mungu ndani yake same as sisi wanadamu tukiwa na ROHO wa Mungu basi tunaitwa wana wa Mungu Johana 1:12, 1 Petro 1:23.

2. Kwa muktadha huu inaua hoja huko juu kwamba ''Yesu ana Baba kama Sisi wanadamu ila melchizedek hana Baba''.

3.Hapa tuelewane kwanza then ndio tuje why Yesu anaitwa first born

4.Kiufupi tu Yesu ndio Kivuli/copy/Kioo cha Mungu hapa duniani kupitia hilo fungu so licha ya kwamba wote tutakuwa wana wa Mungu tukimpokea ila Yesu (Ambaye alishuka duniani kama mwanadamu) anakuwa Top ya wote maana ndio kuhani wetu kutupatanisha na Mungu. Hyo ndio distinguishing factor ila kama angekuwa tu Nabii kama Nabii mwingine basi angekuwa mwana wa Mungu tu ila sio FIRST BORN..... Hii ni kwa muktadha wa hilo fungu.

5. All in all inaonyesha superiority yake dhidi ya wote waliowahi kuishi duniani
 
Mkuu kabla hatujatanua mada elewa hivi.
1. Yesu anaitwa mwana wa Mungu sio sababu alizaliwa kutoka viunoni kwa mtu bali sababu ana ROHO wa Mungu ndani yake same as sisi wanadamu tukiwa na ROHO wa Mungu basi tunaitwa wana wa Mungu Johana 1:12, 1 Petro 1:23.

2. Kwa muktadha huu inaua hoja huko juu kwamba ''Yesu ana Baba kama Sisi wanadamu ila melchizedek hana Baba''.

3.Hapa tuelewane kwanza then ndio tuje why Yesu anaitwa first born

4.Kiufupi tu Yesu ndio Kivuli/copy/Kioo cha Mungu hapa duniani kupitia hilo fungu so licha ya kwamba wote tutakuwa wana wa Mungu tukimpokea ila Yesu (Ambaye alishuka duniani kama mwanadamu) anakuwa Top ya wote maana ndio kuhani wetu kutupatanisha na Mungu. Hyo ndio distinguishing factor ila kama angekuwa tu Nabii kama Nabii mwingine basi angekuwa mwana wa Mungu tu ila sio FIRST BORN..... Hii ni kwa muktadha wa hilo fungu.

5. All in all inaonyesha superiority yake dhidi ya wote waliowahi kuishi duniani

Sasa kama hoja ya uwana wa Mungu wa Yesu unatokana na roho aliye ndani yake kwa nini sasa aitwe GOD'S ONLY BEGOTTEN SON? (John 3:16 )

Nadhani neno Begotten unaelewa maana yake nini kwenye english:(Maana yake KUMZAA)

Kwa mfano hapa tunaelezwa geneology mbali mbali kwenye biblia ya Kiingereza (Mathew 1: 6-9)kwa kutumia neno begot

David the king begot Solomon by her [a]who had been the wife of Uriah. 7 Solomon begot Rehoboam, Rehoboam begot Abijah, and Abijah begot [b]Asa. 8 Asa begot Jehoshaphat, Jehoshaphat begot Joram, and Joram begot Uzziah. 9 Uzziah begot Jotham, Jotham begot Ahaz, and Ahaz begot Hezekiah.

Sasa kama Yesu ni THE ONLY BEGOTTEN SON wewe iweje utafsiri kuwa hiyo ina maanisha kuwa ni SON SIMPLY TU KWA SABABU ANA ROHO WA MUNGU NDANI?

Hoja yako ingekuwa na nguvu kama na Sisi tungekuwa BEGOTTEN SONS WA MUNGU, hiyo tungesema kuwa uSON unaozungumziwa hapa ni huo wa Kuwa na Roho ya Mungu ndani mwetu lakini iweje YESU sasa isemwe ni THE ONLY BEGOTTEN SON?, huO uONLY huohuo maana yake nini?
 
Baba mbinguni na mama duniani,,,huyo baba wa mbinguni Alikuwa anakuja duniani kulala na huyo mama wa duniani??????

Kwa kiasi nakuonyesha ukuhani wa Yesu anza na Wakolosai 1:19~22

Zingatia maneno haya
#kufanya amani kwa damu ya msalaba

#kupatanisha
Yesu Maelezo yake yana jitosheleza sio kuhàni mkuu yesu ni mwana maana yake ana baba mbinguni pia ana mama duniani ndio maana yesu ana sema tutaketi pamoja kwa baba yangu
 
Haruni kama kuhani Mkuu wa kwanza ila aliekuwa kwenye ukuhani wa kuashiria/wa ishara alikuwa akifanya mambo ambayo hayana utofauti na yale yalio kwenye uhalisia na ndio Maana Unaweza pata picha ya Melkizedech na role yake kwenye ukuhani

Hesabu 18:8~32
 
Sasa huyo Melkizedeki ni tofauti na Yesu maana maandiko yanasema kuwa pamoja na huyo Melkizedeki kuwa hapa duniani, hata hapahapa duniani kwenyewe hakuwa na mama, wakati kwa upande wa Yesu ni tofauti yeye alipokuwa hapa duniani, alikuwa na mama!

Halafu si maandiko yanasema Yesu ni mwana wa Mungu?, sasa vipi mnasema hana baba?

Melkizekedi yeye si mwana wa Yeyote maana maandiko yanasema hana baba wala mama
Wewe ndio umenyoosha maelezo mkuu. Wengine wanazunguka.
 
Melkizedeki sio jina rasmi la mtu, bali ni jina la sifa aliyokuwa nayo huyo mtu. Alikuwepo kuhani aliyetajwa kwa hilo jina katika kitabu cha mwanzo, aliitwa hivyo ikimaanisha kuhani mkuu, kuhani mwaminifu, na ndio maana kwenye kitabu cha Ebrews Yesu anatajwa kuwa kuhani mkuu mfano wa Melkizedeki, utofauti ni kwamba Yesu anatajwa ka sifa za kiungu za kutokuwa na baba wala mama nk, ila bado anaitwa Melkizedeki yaani kuhani mkuu.
 
Habari za masiku wanajukwaa wote, leo ningependa tujadili watu mysterious kwenye vitabu vyetu vya dini kama ilivyo kawaida yetu. Hivyo twendeni pamoja ili tusolve mystery hii, kubwa ya yote tuongeze tu maarifa na kujibu maswali ambayo yameonekana magumu kwenye vitabu hivi.

Niweke rai mapema pamoja na kwamba inaongelea mtu wa kwenye imani zetu ila mada hii isijengwe kidini yaani kukashifiana bali ijikite kwenye mrengo wa kuelemishana. Karibuni

UTANGULIZI
Melchizidek anaongelewa kwa mara ya kwanza ndani ya Biblia kwenye kitabu cha mwanzo 14:18 ambapo baada ya Abraham kutokea vitani alikutana na Mfalme wa eneo la Salem (Jerusalem ya leo) ambapo alimbariki na Adam alimpa kikumi cha kila alichokuwa nacho wakati huo.

Kwahiyo kitabu cha mwanzo kinamueleza kama MFALME WA SALEM na kuhani wa Mungu YAHWEH

View attachment 1176929
AGANO JIPYA
Upande wa agano Jipya Melchizedek anaelezwa kuwa ana uhusiano ma Yesu.

Waebrania 5
6 kama asemavyo mahali pengine,Ndiwe kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki

Zaburi 110:4, Waebrania 5:10,6:20 zote zinaeleza kuwa Yesu ni kuhani kwa mfuatano na huyu melchizedek. Ikumbukwe Makuhani wengi wamepita hapo kati na Yesu ametokea kwenye uzao wa Abraham sasa iweje afananishwe na melchizedek na sio kuhani yeyote yule??

Je huyu melchizedek ni nani hasa?

UTATA ZAIDI
Utata zaidi unaibuka pale ambapo muandishi wa kitabu cha waebrania (ambaye mpaka leo hafahamiki ni nani) anaandika haya
Waebrania 7
3 hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.

Tunaambiwa huyu ''Jembe'' hakuwa na baba wala mama na anaishi milele hata sasa???

Ukisoma sura yote inamsifia mtu huyu wa ajabu (mysterious) na kusema licha ya ukuu wa Abraham kama Baba wa wayahudi ila haoni ndani kwa huyu Melchizedek!!

Book of Enoch
Muandishi wa kitabu hiki anajaribu kutupa mwanga kidogo kuhusu utata huu. Ukisoma Enoch 2 sura ya 71 inaeleza kuwa Kuhani Nir (Kaka yake Nuhu) alikuwa na mke ambaye hakulala naye toka alipoteuliwa na Mungu kuwa kuhani. Siku moja anagundua mke wake ana mimba, hivyo ukazuka ugomvi mkubwa mwishowe yule mama akapata presha akaanguka akafa, sasa cha ajabu walipotaka kuizika maiti haraka haraka ''kuua soo'' Wakashangaa mtoto ametoka tayari!!!. Yaani maiti imezaa!!!
Hivyo ikawa concluded kuwa kazaliwa bila baba wala mama.

Ikumbukwe alizaliwa kabla ya gharika, hivyo ili unabii utimie kuwa atakuwa kuhani wa makuhani wote ikabidi Malaika Gabriel amchukue na kumficha bustani ya Eden hivyo akapona gharika na akarudishwa baada ya gharika kupita.

HITIMISHO
Katika pekua pekua zangu sijakutana kabisa na maandiko yeyote kwenye biblia na pseudepigrapha (vilivyoachwa) ambacho kinagusia mwisho wake zaidi vyote vinasema anaishi milele ingawa havisemi wapi ama lini aliacha kuwa mfalme wa Salem.

Sasa wajuvi wa Historia na Dini mtusaidie je mtu huyu alikua nani hasa??

Pia kma alikuwa mkuu kuliko Abraham na amefananishwa na Yesu kwanini hajaongelewa sana kwenye Bible??

Je historia yake ni ipi??

Je mwisho wake ni upi hapa duniani? Au bado anaishi na sisi kwa sura tofauti?

Karibuni....
Siku ukielewa kuwa Agano la kale ni kivuli cha Agano jipya utafunguka ufahamu. Hata hivyo nakushangaa wewe kwa sababu Melkizedeki kaandikwa wazi kwenye Biblia. Unakwama wapi?
 
Melkizedeki sio jina rasmi la mtu, bali ni jina la sifa aliyokuwa nayo huyo mtu. Alikuwepo kuhani aliyetajwa kwa hilo jina katika kitabu cha mwanzo, aliitwa hivyo ikimaanisha kuhani mkuu, kuhani mwaminifu, na ndio maana kwenye kitabu cha Ebrews Yesu anatajwa kuwa kuhani mkuu mfano wa Melkizedeki, utofauti ni kwamba Yesu anatajwa ka sifa za kiungu za kutokuwa na baba wala mama nk, ila bado anaitwa Melkizedeki yaani kuhani mkuu.

Hakuna mahali kwenye bible Yesu anatambulishwa kwa sifa ya uungu, hii ni theolojia ya kuunga unga tu kama hii ya kujaribu kumfananisha Yesu na Melkizedeki, lakini theolojia hiyo imebase kwenye logical inferences tu badala ya maandiko!, yaani imebase kwenye watu kuconnect dots badala ya kauli thabiti ya Yesu mwenyewe

Mathayo 24:36 Yesu mwenyewe kwa kauli yake anasema anasema, "hakuna ajuaye saa wala muda wa siku ile SI MALAIKA WALA MWANA AJUAYE ILA BABA PEKE YAKE (3“But concerning that day and hour no one knows, not even the angels of heaven, nor the Son,[a] but the Father only. ")
hili andiko peke yake linakuonyesha kuwa Yesu yuko limited in knowledge, hajui mambo yote na siri zote za ulimwengu huu, na hiyo peke yake ni ushahidi kuwa siyo Mungu
 
HITIMISHO
Katika pekua pekua zangu sijakutana kabisa na maandiko yeyote kwenye biblia na pseudepigrapha (vilivyoachwa) ambacho kinagusia mwisho wake zaidi vyote vinasema anaishi milele ingawa havisemi wapi ama lini aliacha kuwa mfalme wa Salem.

Sasa wajuvi wa Historia na Dini mtusaidie je mtu huyu alikua nani hasa??

Pia kma alikuwa mkuu kuliko Abraham na amefananishwa na Yesu kwanini hajaongelewa sana kwenye Bible??

Je historia yake ni ipi??

Je mwisho wake ni upi hapa duniani? Au bado anaishi na sisi kwa sura tofauti?

Karibuni....

Hii ni mojawapo ya masomo ambayo nimeyapitia kwa undani kidogo. Sijui kama kuna nafasi ya kutosha. Lakini kwa ufupi niseme tu Mwandishi wa Waebrania, wa Zaburi na yule wa Mwanzo wote wanamzungumzia mtu yule yule; Yesu Kristu. Kumbuka Waebrania ina mstari mmoja muhimu sana Waeb. 13.8 ambayo inasema "Yesu Kristu ni yule yule, Jana, na leo, na hata milele". Na kama unakumbuka katika unabii wa Isaya kuhusu kuzaliwa kwa Yesu tunaambiwa kati ya majina yake mengi mojawapo ataitwa "Mfalme wa Amani"... Mfalme wa Amani ni Mfalme wa Salemu (Salemu ni "amani").

Hii ndio sababu Ibrahim alipokutana na Melkizedek alimpa fungu la kumi (kumbuka hii ilikuwa kabla ya zaka kuingizwa katika sheria za wayahudi). Ukitaka kuelewa hili rejea maneno ya Yesu ambayo anawaambia Wayahudi kuwa "Ibrahim baba yenu aliitamani kuiona siku yangu, aliiona na akafurahi (Yoh 8:56). Na utaona kuwa Yesu hamuiti Ibrahimu "baba yetu" bali "baba yenu"... Lakini pia alitoa dai moja sehemu nyingine (mistari miwili tu chini) ambalo nusura wayahudi wampige. Alisema katika mstari mwingine maarufu "Kweli kweli nawaambia" Yesu akasema, "kabla Ibrahim hajazaliwa mimi Niko" (Yoh 8:58).

Basi hapo kwa ufupi tu; ni sehemu ya tafiti yangu moja ndefu sana; labda siku moja ikimpendeza Mungu nitawashirikisha.
 
Hii ni mojawapo ya masomo ambayo nimeyapitia kwa undani kidogo. Sijui kama kuna nafasi ya kutosha. Lakini kwa ufupi niseme tu Mwandishi wa Waebrania, wa Zaburi na yule wa Mwanzo wote wanamzungumzia mtu yule yule; Yesu Kristu. Kumbuka Waebrania ina mstari mmoja muhimu sana Waeb. 13.8 ambayo inasema "Yesu Kristu ni yule yule, Jana, na leo, na hata milele". Na kama unakumbuka katika unabii wa Isaya kuhusu kuzaliwa kwa Yesu tunaambiwa kati ya majina yake mengi mojawapo ataitwa "Mfalme wa Amani"... Mfalme wa Amani ni Mfalme wa Salemu (Salemu ni "amani").

Hii ndio sababu Ibrahim alipokutana na Melkizedek alimpa fungu la kumi (kumbuka hii ilikuwa kabla ya zaka kuingizwa katika sheria za wayahudi). Ukitaka kuelewa hili rejea maneno ya Yesu ambayo anawaambia Wayahudi kuwa "Ibrahim baba yenu aliitamani kuiona siku yangu, aliiona na akafurahi (Yoh 8:56). Na utaona kuwa Yesu hamuiti Ibrahimu "baba yetu" bali "baba yenu"... Lakini pia alitoa dai moja sehemu nyingine (mistari miwili tu chini) ambalo nusura wayahudi wampige. Alisema katika mstari mwingine maarufu "Kweli kweli nawaambia" Yesu akasema, "kabla Ibrahim hajazaliwa mimi Niko" (Yoh 8:58).

Basi hapo kwa ufupi tu; ni sehemu ya tafiti yangu moja ndefu sana; labda siku moja ikimpendeza Mungu nitawashirikisha.
Ahsante Sana umeleza vizuri mno
 
Hii ni mojawapo ya masomo ambayo nimeyapitia kwa undani kidogo. Sijui kama kuna nafasi ya kutosha. Lakini kwa ufupi niseme tu Mwandishi wa Waebrania, wa Zaburi na yule wa Mwanzo wote wanamzungumzia mtu yule yule; Yesu Kristu. Kumbuka Waebrania ina mstari mmoja muhimu sana Waeb. 13.8 ambayo inasema "Yesu Kristu ni yule yule, Jana, na leo, na hata milele". Na kama unakumbuka katika unabii wa Isaya kuhusu kuzaliwa kwa Yesu tunaambiwa kati ya majina yake mengi mojawapo ataitwa "Mfalme wa Amani"... Mfalme wa Amani ni Mfalme wa Salemu (Salemu ni "amani").

Hii ndio sababu Ibrahim alipokutana na Melkizedek alimpa fungu la kumi (kumbuka hii ilikuwa kabla ya zaka kuingizwa katika sheria za wayahudi). Ukitaka kuelewa hili rejea maneno ya Yesu ambayo anawaambia Wayahudi kuwa "Ibrahim baba yenu aliitamani kuiona siku yangu, aliiona na akafurahi (Yoh 8:56). Na utaona kuwa Yesu hamuiti Ibrahimu "baba yetu" bali "baba yenu"... Lakini pia alitoa dai moja sehemu nyingine (mistari miwili tu chini) ambalo nusura wayahudi wampige. Alisema katika mstari mwingine maarufu "Kweli kweli nawaambia" Yesu akasema, "kabla Ibrahim hajazaliwa mimi Niko" (Yoh 8:58).

Basi hapo kwa ufupi tu; ni sehemu ya tafiti yangu moja ndefu sana; labda siku moja ikimpendeza Mungu nitawashirikisha.
Natamani ungeendelea tupate uelewa zaidi,maelezo mazuri
 
Kumbe kabla ya Bikira Maria yupo mwanamke mwingine aliyewahi kumleta Yesu duniani!

Maana Melkizedeki hakuibuka from nowhere lazima kwa maisha ya hapa duniani alizaliwa, hakudondoka from the sky!

Na ukuhani zama zake ulikuwa ni kwa koo, hii inamaanisha watu waliokuwepo enzi za Melkizedeki walikuwa wanaujua ukoo wake vizuri tu!

Guys let me tell you one thing:
Tatizo lilikuwepo hapa ni baadhi ya Wakiristo kuhijack mafundisho ya Kiyahudi na kujaribu kuyaposses na kuyaangalia katika miwani ya theolojia ya Ukiristo. Hata kwa yale maandiko yasiyomhusu Yesu, wanasema yanamhusu Yesu

Ni kweli kwenye Agano la kale kuna utabiri juu ya Yesu, lakini baadhi ya zile prophecy watu wanazozitumia kumhusisha Yesu wala hazimhusu Yesu kabisa

Ni watu wanajaribu kutumia akili zao tu, kutumia logic zao tu kuungaunga vitu ambavyo wala havihusiani

Ishu ya Melkizedeki na sifa alizopewa ni figurative zaidi lakini watu wanachukulia kuwa ndivyo ilivyo literary

Kwa mfano kwa nini udhani Melkizedeki ni YESU lakini siyo FATHER?
 

Similar Discussions

35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom