Mei Mosi 2023, Sherehe isiyokuwa na matumaini kwa Wafanyakazi

satininus

Senior Member
Feb 11, 2021
135
171
Baada ya kukaa miaka karibia sita bila kuwa ya wafanyakazi wa umma kupewa nyongeza ya mshahara na increments katika awamu ya tano,wafanyakazi walikata tamaa kabisa ya maisha Bora na kujiingiza katika madeni makubwa ambayo yanawatesa hadi sasa.

Kuingia kwa awamu ya sita wafanyakazi walipata matumaini makubwa sana kwa rais ambaye waliamini kuwa atawapa ahueni katika maslahi yao ambayo kimsingi ni haki yao.Mei mosi ya mwaka 2021 wafanyakazi waliahidiwa kumpa muda rais ambaye ndio kwanza alikuwa na miezi miwili tu tangu aingie madarakani, wafanyakazi kwa ujumla wao walimwelewa sana Mama na kumshukuru kwa kuwapa japo kali za matumaini kinyume mtangulizi wake.

Mwaka 2022 ni mwaka ambao wafanyakazi wote wa watanzania walikuwa na matumaini makubwa sana kwa serikali yao na wakaahidiwa ongezeko la mshahara ambalo lingepunguza sana machungu ya maisha. Lakini kilichotokea kila mtu anajua, hivyo mei mosi ya mwaka huu 2023 hakuna mfanyakazi mwenye matumaini yeyote yale na huenda wengi wao hawajui hata mahali itakayofanyika mwaka huu.

Nategemea serikali itafanya juu chini kurudisha matumaini kwa wafanyakazi ili kuongeza utendaji kazi ma ufanisi kazini ili kuleta tija nchini.Kazi iendelee.
 
Meimosi imebaki sherehe ya kulingishiana sare za Tshirts baina ya watumishi wa umma.
 
Matamko ya viongozi wa vyama vya wafanyakazi Afrika Kusini huwa yanawatisha sana watawala. Lkn Tanzania matamko ya viongozi huwa yanaandaliwa na watawala na yamejaa sifa na pongezi kwa watawala.

Mei mosi ya bongo aibu naona mimi
 
Matamko ya viongozi wa vyama vya wafanyakazi Afrika Kusini huwa yanawatisha sana watawala. Lkn Tanzania matamko ya viongozi huwa yanaandaliwa na watawala na yamejaa sifa na pongezi kwa watawala.

Mei mosi ya bongo aibu naona mimi
Ni kweli kabisa maana hata pale wanapotakiwa kudai haki wao wanaomba.Unawezekana wanafanya hivyo ili kukwepa kufuatiliwa na dola kutokana na ukweli kwamba wengi wao wanahusika na wizi na matumizi mabaya ya michango ya wanachama wao.
 
Umeona kuna mtumishi anashobokea hizo sherehe ...
Hovyo ..hovyo
 
Baada ya kukaa miaka karibia sita bila kuwa ya wafanyakazi wa umma kupewa nyongeza ya mshahara na increments katika awamu ya tano,wafanyakazi walikata tamaa kabisa ya maisha Bora na kujiingiza katika madeni makubwa ambayo yanawatesa hadi sasa.Kuingia kwa awamu ya sita wafanyakazi walipata matumaini makubwa sana kwa rais ambaye waliamini kuwa atawapa ahueni katika maslahi yao ambayo kimsingi ni haki yao.Mei mosi ya mwaka 2021 wafanyakazi waliahidiwa kumpa muda rais ambaye ndio kwanza alikuwa na miezi miwili tu tangu aingie madarakani,wafanyakazi kwa ujumla wao walimwelewa sana Mama na kumshukuru kwa kuwapa japo kali za matumaini kinyume mtangulizi wake.Mwaka 2022 ni mwaka ambao wafanyakazi wote wa watanzania walikuwa na matumaini makubwa sana kwa serikali yao na wakaahidiwa ongezeko la mshahara ambalo lingepunguza sana machungu ya maisha. Lakini kilichotokea kila mtu anajua,hivyo mei mosi ya mwaka huu 2023 hakuna mfanyakazi mwenye matumaini yeyote yale na huenda wengi wao hawajui hata mahali itakayofanyika mwaka huu.Nategemea serikali itafanya juu chini kurudisha matumaini kwa wafanyakazi ili kuongeza utendaji kazi ma ufanisi kazini ili kuleta tija nchini.Kazi iendelee.
Tatizo kubwa lipo katika safu za uongozi wa vyama vya wafanyakazi. Vyama hivi ni vinyonge na dhaifu sana mbele ya serikali. Sehemu zingine duniani vyama kama hivi huwa na nguvu kubwa katika kuiwajibisha serikali kulipa mishahara iendanayo na hali halisi ya maisha.

Sehemu nyingine viongozi wa vyama hivi wana nguvu na mtaji mkubwa sana wa kisiasa. Na hata kupitia historia ya uhuru wa nchi yetu inathibitisha nguvu ya vyama hivi na viongozi wao. Vyama hivi vikijipanga vyema huweza kuchochea maandamano ama migomo ili kuhakikisha kilio cha wafanyakazi kinasikilizwa na kufanyiwa kazi.

Lakini hapa Tanzania hakuna kitu kama hicho. Vyama hivi vime "compromise" na serikali, na kujishusha chini. Vimetelekeza jukumu lao la msingi la kupigania haki za msingi za wafanyakazi. Vinaona chochote kile wanachofanyiwa wafanyakazi ni hisani na upendeleo tu wa kipekee kwao.

Viongozi wa vyama hivi hawaguswi na kilio cha wale wanao waongoza. Wanafanya hivyo kwa kuwa hawana mgongano wowote ule wa kimaslahi dhidi ya viongozi wa serikali, kwa kuwa wao ni wamoja, wanaongea lugha moja na pia wanakula meza moja. Kwa hiyo hiki kilio cha siku zote wafanyakazi sio chao.
 
Tatizo kubwa lipo katika safu za uongozi wa vyama vya wafanyakazi. Vyama hivi ni vinyonge na dhaifu sana mbele ya serikali. Sehemu zingine duniani vyama kama hivi huwa na nguvu kubwa katika kuiwajibisha serikali kulipa mishahara iendanayo na hali halisi ya maisha.

Sehemu nyingine viongozi wa vyama hivi wana nguvu na mtaji mkubwa sana wa kisiasa. Na hata kupitia historia ya uhuru wa nchi yetu inathibitisha nguvu ya vyama hivi na viongozi wao. Vyama hivi vikijipanga vyema huweza kuchochea maandamano ama migomo ili kuhakikisha kilio cha wafanyakazi kinasikilizwa na kufanyiwa kazi.

Lakini hapa Tanzania hakuna kitu kama hicho. Vyama hivi vime "compromise" na serikali, na kujishusha chini. Vimetelekeza jukumu lao la msingi la kupigania haki za msingi za wafanyakazi. Vinaona chochote kile wanachofanyiwa wafanyakazi ni hisani na upendeleo tu wa kipekee kwao.

Viongozi wa vyama hivi hawaguswi na kilio cha wale wanao waongoza. Wanafanya hivyo kwa kuwa hawana mgongano wowote ule wa kimaslahi dhidi ya viongozi wa serikali, kwa kuwa wao ni wamoja, wanaongea lugha moja na pia wanakula meza moja. Kwa hiyo hiki kilio cha siku zote wafanyakazi sio chao.
Ni kweli kabisa vyama hivi havina nguvu wala ushawishi wowote ule kwa serikali ni kama wapiga zumari wa hamelini.
 
Binafsi sipendi kabisa kusikia kitu TUCTA!
wezi wa fedha za wafanyakazi bila FAIDA
Amkeni enyi wafanyakazi, mnaibiwa bila sababu!
 
Mei mosi hivi inafanyikia wapi jamani2023 maana junakuwaga na fulsa nyingi sana za biashara
 
Kutegemea ahueni ya maisha kutokana na ujira wa Serikali katika nchi hizi maskini za Ki-Afrika ambako sifa zake kuu za msingi ni ufisadi, matumizi mabaya ya fedha za umma, rushwa, demokrasia ya kudonoa donoa ni kujidanganya tu. Wewe kama unapenda kuajiriwa na hizi Serikali za Africa basi kuwa mpole kuwa upo upande ambao unasogeza maisha kwa kulinda uhai wako usiathiriwe na njaa ya kukosa mlo.

Ndugu zangu, tuwekezeni nguvu kubwa kwenye kujitegemea wenyewe. Kama ni mashamba tulime, kama ni mifugo tufuge. Hata kama sera na mazingira ya kilimo si madhubuti sana kwamba hubadilika kama kinyonga, ila ni bora upate maumivu ukiwa huru kuliko kuwa sehemu ambayo unajipa matumaini hewa. Yaani kabisa watu wanatarajia hizi Serikali za Afrika ziwawezeshe wawe na maisha bora? Ni kujidanganya tu.
 
Ni kweli kabisa vyama hivi havina nguvu wala ushawishi wowote ule kwa serikali ni kama wapiga zumari wa hamelini.
Vitakuwaje na nguvu wakati viongozi wake ni washirika wa state? Jamani hivi mbona tuna macho hatuoni, tuna ubongo hatuwazi?
 
Baada ya kukaa miaka karibia sita bila kuwa ya wafanyakazi wa umma kupewa nyongeza ya mshahara na increments katika awamu ya tano,wafanyakazi walikata tamaa kabisa ya maisha Bora na kujiingiza katika madeni makubwa ambayo yanawatesa hadi sasa.Kuingia kwa awamu ya sita wafanyakazi walipata matumaini makubwa sana kwa rais ambaye waliamini kuwa atawapa ahueni katika maslahi yao ambayo kimsingi ni haki yao.Mei mosi ya mwaka 2021 wafanyakazi waliahidiwa kumpa muda rais ambaye ndio kwanza alikuwa na miezi miwili tu tangu aingie madarakani,wafanyakazi kwa ujumla wao walimwelewa sana Mama na kumshukuru kwa kuwapa japo kali za matumaini kinyume mtangulizi wake.Mwaka 2022 ni mwaka ambao wafanyakazi wote wa watanzania walikuwa na matumaini makubwa sana kwa serikali yao na wakaahidiwa ongezeko la mshahara ambalo lingepunguza sana machungu ya maisha. Lakini kilichotokea kila mtu anajua,hivyo mei mosi ya mwaka huu 2023 hakuna mfanyakazi mwenye matumaini yeyote yale na huenda wengi wao hawajui hata mahali itakayofanyika mwaka huu.Nategemea serikali itafanya juu chini kurudisha matumaini kwa wafanyakazi ili kuongeza utendaji kazi ma ufanisi kazini ili kuleta tija nchini.Kazi iendelee.
serikali za kifisadi hata siku moja huwa hazishughurikii maslahi ya wafanyakazi bali zinajali maslahi ya wanasiasa tu.haingii akilini mbunge baada ya miaka mitano tu anapiga 500m.wafanyakazi waache kuwasaidia wanasiasa kuiba kura wakati wa uchaguzi.wasimamie haki kwa kila mgombea.
 
Serikali ifute chama Cha walimu Tanzania (CWT), Hakina msaada Kwa walimu
Si CWT pekee, vyama vyote vya wafanyakazi bongo havistahili kuwepo hata kwa sekunde. Watu wajitegemee peke yao. Watu walime na kufuga, waache kutegemea eti watapata maisha bora kutokana na mishahara ya kuajiriwa.
 
Siku hizi mei mosi imebaki kama ceremonial day tu hakuna jipya. Mei mosi iliyokuwa worse zaidi ni ile iliyofanyika iringa jpm akiwa mgeni rasmi. Mama akapigilia msumari kwa kutoa ahadi hewa ile ndiyo ilimaliza kabisa matumaini ya wafanyakazi mei mosi
 
Back
Top Bottom