Medical council of Tanganyika(MCT), acheni kuonea vijana wa wanaomaliza udaktari

Bhahebhu

Member
Dec 3, 2021
33
33
Kwanza nikiwa kama mzazi niwape pole sana mamia kwa maelfu wa vijana wanaomaliza udaktari katika vyuo mbalimbali hapa nchini,kwa sababu ni wahanga wakubwa wa hii kitu inaitwa MCT.

Mchakato wa kumpata daktari unajulikana na ni mgumu sana kwani mtu kufikia kumaliza miaka mitano ya udaktari wa binadamu anakuwa amepitia mitihani mingi ya theory na practical.

Sasa hawa MCT wamekuja na kitu kinaitwa pre internship na post internship, kichekesho zaidi ni hiyo pre internship, ndugu zangu duniani kote na hata hapa Tanzania kwenye baadhi ya mabaraza kama famasia, maabara, na wauguzi, hamna kitu kinaitwa pre internship exam, unampima nini kijana ambae anatarajia kufanya mafunzo ya internship mwaka mmoja??? Lengo lenu katika hili ni nini?, Ina maana nchi hii madaktari wametosha kiasi hicho mnaamua kuzima ndoto za vijana??.

Maombi yangu kwa hawa wakubwa;
Waziri wa afya na naibu wake,
Na kwa unyenyekevu Mh. Rais wetu Mama Samia, naomba kuagizwa kufutwa mara moja kwa hiki kitu kinachoitwa pre internship na pia kukiangazia kwa jicho la tatu post internship kama inafaa kuendelea kuwepo kwenye kada hii ya udaktari.
 
Sio upigaji wa hela Mana unasoma ili uwe mtumwa wa fikra uwe unaongozwa na kanuni na watu kila mahali.
Mana hata huko shuleni ulikuwa unaongozwa na kanuni za hesabu kisayansi. So already conditioned long time.
Unahudumiwa kila since shuleni,chuoni bumu ni mfano wa salary wanakuzoesha.
Mpaka wanakutunzia ili ukizeeka uwe unapewa kidogokidogo mpaka unakufa Mana huwezi kuishika like 300M mkononi Mara moja utawewuka
 
Safi sana. Tena mpigwe pepa la nguvu.

Huko vyuoni hamsomi kazi yenu kubwa ni kuingiza chupa sehemu za siri tu.
Acha utaahira huo, una-generalise mambo sana, hizi kozi za miaka mitano we zisikie tu, na si udaktari pekee, kuna nyingine. Ungejua figisu wanazopitia watu hadi kupata hizo degree ungekaa kimya tu. Hiyo pre nini sijui ni kihumzi tu kingine, kutesa watoto wa watu bure tu
 
Sio upigaji wa hela Mana unasoma ili uwe mtumwa wa fikra uwe unaongozwa na kanuni na watu kila mahali.
Mana hata huko shuleni ulikuwa unaongozwa na kanuni za hesabu kisayansi. So already conditioned long time.
Unahudumiwa kila since shuleni,chuoni bumu ni mfano wa salary wanakuzoesha.
Mpaka wanakutunzia ili ukizeeka uwe unapewa kidogokidogo mpaka unakufa Mana huwezi kuishika like 300M mkononi Mara moja utawewuka
MCT kwa sasa imeingia KIRUSI, imeingiwa na MATAPELI, Imeingiwa na WANASIASA,hawa kina Elisha Osati huyu ambaye alikua Rais wa MAT eti naye ni Staff member wa MCT, siasa tupu kuumiza Vijana wa watu.

Haiwezekani kijana huyu aliyekaa chuo miaka 5 au 7 kwa wale wa nje, anataka kuanza mafunzo unampa mtihani, anamaliza unampa mtihani tena, kuna kozi gani ina Pre and Post internership? UTAPELI mtupu kubana pesa za umma. Ngojeni CORONA itawanyoosha na hivi madaktari watakua wachache.
 
MCT kwa sasa ni wanasiasa wote. Tena wanaenda kuivuruga taaluma ya udaktari vibaya mno. Unawapima madaktari waliokokaa chuo miaka 5 shule si uende TCU ukawaulize waliwafaulishaje? Kwani vyuoni wanasomea ubmdaktari Mbwa kiasi kwamba hawataweza kutibu binadamu?

#NONSENSE
 
You have a point!
Sio upigaji wa hela Mana unasoma ili uwe mtumwa wa fikra uwe unaongozwa na kanuni na watu kila mahali.
Mana hata huko shuleni ulikuwa unaongozwa na kanuni za hesabu kisayansi. So already conditioned long time.
Unahudumiwa kila since shuleni,chuoni bumu ni mfano wa salary wanakuzoesha.
Mpaka wanakutunzia ili ukizeeka uwe unapewa kidogokidogo mpaka unakufa Mana huwezi kuishika like 300M mkononi Mara moja utawewuka
 
Woga wa nini kuhusu kufanya mtihani ikiwa mhusika alikaa vizuri darasani na kufaulu? Mimi ninaamini madaktari ni watu wanaojiamini na kuenjoy kufanya mitihani sana, sasa mitihani miwili tu (Pre and post internship), tena mitihani muhimu kwa professional yake iweje Daktari alalamike?
Katika hili nitawatetea MCT kwa 100%.
Kwa mfano:

1. Katika mazingira ya sasa ambao vijana wamesoma katika vyuo vingi tofauti na katika nchi tofauti tofauti sana, kigezo cha kuwapima kuwa wamefuzu kabla ya kuanza internship ni kuweka mtihani tu ili kuwa na standard zinazokubalika.

2. Katika mazingira ambayo vyuo vingi vimekuwa vikichakachua ufaulu, ni kwanini MCT isiweke mtihani ili kujiridhisha kama mhusika anafuzu kutibu watanzania?
 
MCT kwa sasa imeingia KIRUSI, imeingiwa na MATAPELI, Imeingiwa na WANASIASA,hawa kina Elisha Osati huyu ambaye alikua Rais wa MAT eti naye ni Staff member wa MCT, siasa tupu kuumiza Vijana wa watu.

Haiwezekani kijana huyu aliyekaa chuo miaka 5 au 7 kwa wale wa nje, anataka kuanza mafunzo unampa mtihani, anamaliza unampa mtihani tena, kuna kozi gani ina Pre and Post internership? UTAPELI mtupu kubana pesa za umma. Ngojeni CORONA itawanyoosha na hivi madaktari watakua wachache.
Binafsi sijawahi kusikia au kuona Daktari halisi akiogopa au kulalamika kufanyishwa mtihani unaolenga kupima ufahamu wake wa kuweza kutibu wagonjwa.

Woga wa nini ndugu kama ulifuzu vyema udaktari wako?
 
Kwanza nikiwa kama mzazi niwape pole sana mamia kwa maelfu wa vijana wanaomaliza udaktari katika vyuo mbalimbali hapa nchini,kwa sababu ni wahanga wakubwa wa hii kitu inaitwa MCT.

Mchakato wa kumpata daktari unajulikana na ni mgumu sana kwani mtu kufikia kumaliza miaka mitano ya udaktari wa binadamu anakuwa amepitia mitihani mingi ya theory na practical.

Sasa hawa MCT wamekuja na kitu kinaitwa pre internship na post internship, kichekesho zaidi ni hiyo pre internship, ndugu zangu duniani kote na hata hapa Tanzania kwenye baadhi ya mabaraza kama famasia, maabara, na wauguzi, hamna kitu kinaitwa pre internship exam, unampima nini kijana ambae anatarajia kufanya mafunzo ya internship mwaka mmoja??? Lengo lenu katika hili ni nini?, Ina maana nchi hii madaktari wametosha kiasi hicho mnaamua kuzima ndoto za vijana??.

Maombi yangu kwa hawa wakubwa;
Waziri wa afya na naibu wake,
Na kwa unyenyekevu Mh. Rais wetu Mama Samia, naomba kuagizwa kufutwa mara moja kwa hiki kitu kinachoitwa pre internship na pia kukiangazia kwa jicho la tatu post internship kama inafaa kuendelea kuwepo kwenye kada hii ya udaktari.
Hao waliianzisha huo utaratibu enzi zao wakati wanaenda internship hakukuwa na kitu hicho na ilikuwa ukimaliza tu, ripoti ya daktari bingwa aliyekusimamia inatosha unasajiliwa , lakini hao hao ndio wanawawekea vikwazo watoto wa wenzio.

Hixi bodi za kitaaluma zinatska wawe wachache ili kuindoa ushindani wa ajira.
 
Back
Top Bottom