Media TZ zapigwa stop ku publicise CHADEMA!

Mpeni sifa Yesu

JF-Expert Member
May 23, 2010
646
129
Jamani, hivi nikisema kuwa media za tz zimepigwa stop kuwaonyeshaonyesha sana wana chadema nitakuwa nimekosea? kama sijakosea naombeni wahusika watoe maelezo ya kutosha hapa. Kwasababu inavyoonekana hali halisi ni kama media zetu zimenunuliwa na selikali kabisa, selikali ndiyo inayowaambia nini cha kuongea na nini si cha kuongea...pamoja na kwamba zingine ni private owned.

Nikianzia mtu mmoja aliongea jana kuwa, wakati dr.slaa ametangaza kuwa hatamtambua rais baada tu ya uchaguzi, hakuna chombo chochote kiliamka kwenda kwa slaa kumwuliza kuwa matokeo yameshatangazwa wewe unasemaje, unachukua msimamo gani etc, kwasababu waliogopa kuwa kile atakachoongea slaa baada ya matokeo kitaleta fujo, so wakawapiga stop.

pili, wanachadema walipotoka nje ya bunge, ni mbunge gani alihojiwa siku ile, hasa kiongozi wa upinzani na dr.slaa ambaye ni katibu wa chama ili kutoa msimamo wa chadema...kwasababu wengi kusema ukweli tulikuwa tunahitaji kusikia toka wa wabunge wetu nini wamefanya kwa kutoka nje ya bunge na nini kinaendelea na kwanini? lakini media zime mute zote hawataki kuwaonyesha....

Kuna mambo mengi sana, si cha star tv, itv, tbc, channel ten wala nini, zoote zimebaki kimyaaa, kitu ambacho kinaonyesha kama zimepigwa stop na selikali. kwanini media zetu hazina uhuru? au haziko impartial? tunaelekea wapi?

kwa namna hii, utakuwa mambo yote tunayoletea kwenye luninga yanakuwa ya kutu brainwash tu, propaganda za kutupiga upofu wa akili tusione mabaya ya selikali, tusikosoe selikali etc. UKITAKA KUAMIN HILI, ANGALIA TV ZA NJE AFU LINGANISHA NA ZA KWETU. utakuta za kwetu zinaboa kwasababu mtu mmoja anakua anapandikia chochote anachokitaka au kukiamini kwa interest zake binafsi kwa wananchi na si hali halisi...tutafika wapi hivi jamani,

ndo maana waandishi wa habari wa kenya walikuja vyema sana kipindi kile wakawa wanakubalika sana, na selikali ikawatimua kwasababu walikuwa wanaendesha mambo kiprofessional kuliko hawa waandishi wetu wa habari waliohitimu certificate pale BUGURUNI.
 
fuatilia mjomba yaelekea uko nyuma saaana... CHADEMA wameshine magazeti yooote leo.. Na usipoandika neno CHADEMA hakuna ataenunua gazeti lako
 
achana na magazeti, wangapi tz wanasoma magazeti? watz wengi wanasikiliza na kuangalia tv na radio. hivyo ndivyo vyombo vyenya nguvu zaidi kuliko magazeti ambayo hadi uyasome unatakiwa kutoa pesa si chini ya mia tano, ambayo watz wengi hawana....kwanini tv na radio zimewanyamazia sana? hata kama wameongea, hawajaongea kwa kiwango kilichokuwa kinatakiwa kwao kaama ma professonal.
 
waandishi wengi wa nchi maskini kwa mfano nchi za afrika, kwa sababu ya umaskini wao , hawako huru kuandika kile wanachokitaka bali mabwana zao wanachotaka. kifupi waandishi wa habari tanzania wengi walikimbia umande kwa mf. marina hassan hata kazi aliipata kibahati bahati tu. so hana la kufanya zaidi ya kuandika habari zile tu zilizo njema machoni pa mumewe.
 
duh, great thought! wana mapinduzi hawatuwezi,kama chama chao kimeshindwa kufanya mabadiliko, basi waiache CHADEMA wafanye. Haf nowadays, simu ni cheap sana; ppl speak,educate one another;one step at a time tutafika hata wafanyeje!. Hio inajulikana wamenunua radio,tv zote kwani hizo leseni wanazizibiti wao. Eeh MUNGU ISAIDIE TANZANIA
 
achana na magazeti, wangapi tz wanasoma magazeti? watz wengi wanasikiliza na kuangalia tv na radio. hivyo ndivyo vyombo vyenya nguvu zaidi kuliko magazeti ambayo hadi uyasome unatakiwa kutoa pesa si chini ya mia tano, ambayo watz wengi hawana....kwanini tv na radio zimewanyamazia sana? hata kama wameongea, hawajaongea kwa kiwango kilichokuwa kinatakiwa kwao kaama ma professonal.
una jina zuri lakini muongo
 
najua ni shida hizo za waandishi wetu wa habari na vyombo vyenyee...hakuna kingine..njaa na ugonjwa wa fikra potofu!!!
 
Hivi habari leo ni Gazeti la CCM au ni Gazeti la Serikali, sijawahi kuona siku hata moja likiandika positive news kuhusu Oposition parties....!
 
Its true. Kituo pekee kilichoripoti siku ile ni Idhaa ya kiswahili ya BBC kwenye dira ya dunia.
 
Jamani, hivi nikisema kuwa media za tz zimepigwa stop kuwaonyeshaonyesha sana wana chadema nitakuwa nimekosea? kama sijakosea naombeni wahusika watoe maelezo ya kutosha hapa. Kwasababu inavyoonekana hali halisi ni kama media zetu zimenunuliwa na selikali kabisa, selikali ndiyo inayowaambia nini cha kuongea na nini si cha kuongea...pamoja na kwamba zingine ni private owned.

Nikianzia mtu mmoja aliongea jana kuwa, wakati dr.slaa ametangaza kuwa hatamtambua rais baada tu ya uchaguzi, hakuna chombo chochote kiliamka kwenda kwa slaa kumwuliza kuwa matokeo yameshatangazwa wewe unasemaje, unachukua msimamo gani etc, kwasababu waliogopa kuwa kile atakachoongea slaa baada ya matokeo kitaleta fujo, so wakawapiga stop.

pili, wanachadema walipotoka nje ya bunge, ni mbunge gani alihojiwa siku ile, hasa kiongozi wa upinzani na dr.slaa ambaye ni katibu wa chama ili kutoa msimamo wa chadema...kwasababu wengi kusema ukweli tulikuwa tunahitaji kusikia toka wa wabunge wetu nini wamefanya kwa kutoka nje ya bunge na nini kinaendelea na kwanini? lakini media zime mute zote hawataki kuwaonyesha....

Kuna mambo mengi sana, si cha star tv, itv, tbc, channel ten wala nini, zoote zimebaki kimyaaa, kitu ambacho kinaonyesha kama zimepigwa stop na selikali. kwanini media zetu hazina uhuru? au haziko impartial? tunaelekea wapi?

kwa namna hii, utakuwa mambo yote tunayoletea kwenye luninga yanakuwa ya kutu brainwash tu, propaganda za kutupiga upofu wa akili tusione mabaya ya selikali, tusikosoe selikali etc. UKITAKA KUAMIN HILI, ANGALIA TV ZA NJE AFU LINGANISHA NA ZA KWETU. utakuta za kwetu zinaboa kwasababu mtu mmoja anakua anapandikia chochote anachokitaka au kukiamini kwa interest zake binafsi kwa wananchi na si hali halisi...tutafika wapi hivi jamani,

ndo maana waandishi wa habari wa kenya walikuja vyema sana kipindi kile wakawa wanakubalika sana, na selikali ikawatimua kwasababu walikuwa wanaendesha mambo kiprofessional kuliko hawa waandishi wetu wa habari waliohitimu certificate pale BUGURUNI.
Nitajibu ya kwanza kwamba, The citizen waliongea juu ya hio swala tena fasta - Slaa: Why we gave swearing-in ceremony wide berth

alafu jambo ya pili ninakubali na wewe kwamba tv za nje kwa mfano za Kenya wantoaga siri nyingi za serikali bila hofu kwa hio hapo nakubali kabisa. Tena sana.
 
Wakati mwingine hata hawajakatazwa. Ni wao wenyewe tu wanaamua kujipendekeza na kuwalamba miguu watawala...
 
Inawezekana ikawa true coz the day CHADEMA wamefanya walkout nilisubiri kwa hamu newz ya saa mbili.TBC walipretend kama nothin lyk that ever happend or they didnt had the walkout newz instead wakazungumzia tu hotuba ya JK aliyoitoa. Kesho yake ndo wakaja na edited version yao ya kilichotokea ambacho ni mchujo unaowaponda CHADEMA tu kwa hatua yao. Ndo nikajua direct kuwa TBC=CCM
 
una jina zuri lakini muongo
ndugu yangu, wewe fikiria tu, siku ile tulisubiri sana kusikia toka kwa Dr.slaa akijibu ni kwanini wametoka nje ya bunge, ITV, Star TV, channel ten, TBC etc, hakuna aliyekwenda kumhoji ili tujue upande mwingine wa shilingi. that means walitaka tuujue tu upande wao kina ccm wanavyotaka ieleweke.

Pili, Dr.slaa alisema hamtambui kikwete, lakini baada ya deadline kupita, hakuna chombo chochote kilichoenda kumhoji ili kusikia anachukua hatua gani. this is too dangerous kwasababu inaweka madukuduku mioyoni mwa watu...

kama wengi walivyosema, wengi tulisubiri sana kusikia kwenye taarifa za habari, lakini tukaona hakuna kitu. ajabu kweli. ndo tunasema kuwa hapa ni wazi wamepigwa stop, ccm ndo inaamua nini mtangaze, nini msitangaze. ninachoongelea hapa ni television, sio magazeti, magazeti usiongelee kabisa kwasababu sio kitu direct na pia yanahitaji mtu anunue kwa pesa, watz wengi wanaona bora watumie 500 kwa mlo kuliko kununua karatasi...

tutafika wapi kama vyombo vyetu haviko huru kiasi hiki? karibuni magazeti na television za kenya, tunawakaribisha kwa hamu. hapa ndio napata jibu kwanini wale waandishi wa kikenya walifukuzwa mara moja kipindi kile hapa tz.....kwasababu walikuwa wanafuata professio yao.
 
jamani tuwe wakweli, ili uandikwe na kuonyeshwa kweny runinga ni lazima utengeneze habari. Kutokea bunge la kuapisha wabunge, kuunda kambi ya upinzani, kumsusia rais hotuba hadi mhe zitto alipotoa kauli zake chadema imekuwa hi habari kuu katika vyombo vyote hivyo.

kama tunataka chadema iandikwe na kuonyeshwa zaidi ni lazima tutengeneze habari kama vile tufanya makongamano, maandamano ya amani ya kujadili na kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi n.k


tukiendelea na utaratibu huu wa kumsubiri dr slaa aanzishe kila kitu, ndio tutaishia kulalamika kuwa waandishi wamenunuliwa kumbe tunashindwa kutengeneza habari.

Mfano halisi pale takukuru ilipomsafisha chenge na ubalozi wa uingereza kutoa kauli tofauti, kama tunataka kuandikwa na chadema kubaki juu ilitakiwa wenye uchungu na nchi hii tuandamane kushinikiza dr hosea ajiuzulu. Hapo lazima magazeti, tv na redio zote zingeitangaza chadema kwa muda mrefu sana. Hivi familia ya lowasaa inachunguzwa tngefanya maandamano mengine ya amani kushinikiza vyombo vya uchunguzi kutoa taarifa hizo tutaandikwa mpaka tuchoke.


ni lazima tukubali ukweli kwamba baada ya uchguzi kupita dr slaa ni raia wa kawaida kama mimi na wewe tu, wakati vyomboi vya habari vinatafuta habari mpya zinazouzika. Hivyo tuachane na uvivu wa kufikiri na kukosa ubunifu wa kuiweka chadema juu. Tuchukue hatua tutengeneze habari.
 
Udikiteta, njaa za baadhi ya waandishi, kujipendekeza na kukwepa kodi baadhi ya wamiliki ndio sababu uhuru wa hao wandishi unapotea ni hatari kwa taifa, lakini msijali wanamapinduzi tunayo magazeti ya mapinduzi raia mwema na mwanahalisi hawa ni makamanda wa vita wamejotoa mhanga kulitetea taifa hili na watu wake tunataka mjasilia mali mmoja aanzishe tv manake tv zote zilizopo ni wachakachuaji wa habari na wanajipendekeza saana kwa kusahau ethics zao. Hawajua kuwa media ni muhimili unaojitegemea wenyewe na unaweza kufanya lolote likatokea, poor tanzania media poor country
 
Back
Top Bottom