Media kuikosoa Serikali: Je, Tanzania tuna Strong Media au Strong Journalists wenye Uwezo huo?

Most media ambazo ziliikosoa serikali either zilifungiwa, kutishiwa au kuundiwa kesi
Mkuu Luse, not necessarily, japo ukosoaji unahitaji kufanywa na manguli wenye weledi wa hali ya juu mfano Ukisema Tumpinge Magufuli ni Dikiteta kwa sababu tuu amezuia mikutano ya kisiasa, utaitwa mchochezi. Lakini ukisema kuwa Magufuli ni Dikiteta, ukaonyesha vifungu vya katiba vilivyotoa haki ya kukutana, ukaonyesha jinsi Magufuli alivyovunja Katiba, ukaonyesha mipaka ya mamlaka ya rais kuwa hana mamlaka ya kwenye kinyume cha katiba, kisha ukauliza alipopiga marufuku mikutano ya siasa alitumia mamlaka gani na kumalizia kuelekeza hatua za kumchukulia rais pale anapovunja katiba, amini usiamini Magufuli angeifuta kauli yake na media ingekuwa very safe, ndio maana sisi wengine tulisupport UKUTA but conditionally.
Kufuatia Umuhimu wa Maandamano ya UKUTA ... - JamiiForums
Paskali
 
Mkuu Mkaruka TBC ni public media not government media ndio maana ina bodi yake independently hivyo inaweza kuikosoa serikali kama ilivyo BBC.

Sijazungumzia neutrality, nimesema public media inatanguliza mbele maslahi ya umma, kazi ya serikali ni kuutumikia umma, hivyo serikali ikikosea TBC ilipaswa kuwa na uwezo wa kuikosoa.
Paskali

Unachokizungumza kuhusu TBC ni mambo ambayo tungetarajia iyatende kwa umma, lakini imegeuka ni chombo cha chama fulani na serekali na sio umma. Waandishi wa habari nao ugumu wa maisha umewageuza mateka wa tumbo.
 
tulikuwa tunakutegemea wewe ila na wewe ukamezwa maana ulivyokuwa unamtetea bashite utadhani ulikuwa nae uko koromije.......................

inshort ni hakuna ata mmoja wote njaa na uwoga vimewajaa
 
Nashukuru sana kwa kunipa heshima ya kunijibu. Kwanza nashukuru umetupa track yako ya u media, ambayo imenisaidia ku confirm kuwa ni kweli wewe si muandishi wa habari. Kuwa host wa kipindi kinacholeta magwiji sio kuwa muandishi wa habari. Ni sawasawa na kumuita Zembwela Muandishi wa habari, kama tulivyomuuliza makonda, tuletee track yako ya uandishi wa habari, investigative na public interest, Maxence hajawahi kujiita muandishi wa habari, pamoja na kuwa na kuwa na uwezo mkubwa sana wa kuwakutanisha watu kuzungumzia habari. Zile habari sio zake, ni sawa na wewe, kiti moto hakikuwa investigative work yako, wale madiwani wa ccm wanaotoka kibaha na wazalendo wengine walikua wanatulietea scops tu, sio wewe. Pili nashukuru pia kuwa miaka yako 27 ya kukaa studio, not even press room, haitoshi kukuita muandishi wa habari. Ni sawa na kutuambia kuwa kwa kuwa unakaa karibu na mahakama basi wewe ni mwanasheria. Ndio maana karani wa mahakama aliyekaa mahakamani miaka 30 haitwi mwanasheria. Swala la Makonda haliweze kuwa your piece of literature, ni swala linalohusu integrity ya Taifa la Tanzania na kitu kinachoitwa Good Governance, sio mambo ya opinion zako, ulitakiwa ujue hata hilo kabla hujaingiza ujikombi wako, kwenye mambo serious. Once again, usipende kujikwaza sana na kujifanya mjuaji, neno linasema, ajikwezaye atashushwa, kwanini kama huna point lazima tu uongee, jitambue kuwa wewe sio opinion leader kwenye sekta ya media, kwanza sidhani hata kama unazo qualification zaidi tu ya ujanja ujana fulani, kama we bingwa weka vyeti vyako hapa tuone kama walau diploma ya uandishi, sana sana pengine una certificate ya Royal bahati kama una ya TSJ. (over) nakusubiri!

Ha ha ha
 
Wanabodi,

Declaration of Interest: Mwanzisha Mada ni Mwandishi wa Habari Mstaafu ambaye amehudumu kwenye tasnia hii kwa miaka 27, hivi sasa ni mstaafu akiendelea kuhudumu kama Mwandishi/Mtangazaji was Kujitemea kupitia kampuni ya PPR.

Serikali zote duniani huendeshwa na mihimili 3 ambayo ni rasmi, Serikali, Bunge na Mahakama, ila kuna mihimili wa nne ambao ni mihimili usio rasmi, huu ni mhimili wa Media, The Fourth Protocol.

Waziri wa Habari Mhe. Nape Mnauye ametoa ruhusa kwa media kuikosoa Serikali. Ili hili liweze kufanyika kwa manufaa na kuleta tija, lazima kwanza tuwe na Independent Stong Media na tuwe na waandishi mahiri ambao ni ma Iconic figures akiandika "This is wrong", Serikali itasikiliza.

Swali ni jee Tanzania tunazo hizo strong media?, jee tunao hao strong journalists wenye uwezo wa kuikosoa Serikali na Serikali ikawasikiliza? .

Kama tunazo ni zipi? . Kama hatuna kwa nini hatuna strong media?. Na jee hao waandishi strong journalists tunao?, ni kina nani wakiandika au wakisema Serikali itasikia, itabadilika?.

Mifano ya Strong Media.
US wana strong media. Wana vyama viwili vikuu vya siasa The Democrats na The Republican. Wana magazeti makuu mawili, The New York Times na The Washington Post. Pia wana TV mbili kubwa CBS na ABC.

UK pia wana Strong Media. Wana vyama vikuu viwili vya siasa, Labour na Conservative. Wana gazeti moja kuu, The Daily Telegraph. Wana radio moja kuu na TV moja kuu, BBC.

Sisi na huu utitiri wa vyama, utitiri wa magazeti, utitiri wa TV stations na utitiri wa magazeti, jee tuna any strong media ndani ya utitiri huu?.

Paskali
Unlee otherwise tundu lisu atakuwa anawasumbua mahakamani kila siku
 
Wanabodi,

Declaration of Interest: Mwanzisha Mada ni Mwandishi wa Habari Mstaafu ambaye amehudumu kwenye tasnia hii kwa miaka 27, hivi sasa ni mstaafu akiendelea kuhudumu kama Mwandishi/Mtangazaji was Kujitemea kupitia kampuni ya PPR.

Serikali zote duniani huendeshwa na mihimili 3 ambayo ni rasmi, Serikali, Bunge na Mahakama, ila kuna mihimili wa nne ambao ni mihimili usio rasmi, huu ni mhimili wa Media, The Fourth Protocol.

Waziri wa Habari Mhe. Nape Mnauye ametoa ruhusa kwa media kuikosoa Serikali. Ili hili liweze kufanyika kwa manufaa na kuleta tija, lazima kwanza tuwe na Independent Stong Media na tuwe na waandishi mahiri ambao ni ma Iconic figures akiandika "This is wrong", Serikali itasikiliza.

Swali ni jee Tanzania tunazo hizo strong media?, jee tunao hao strong journalists wenye uwezo wa kuikosoa Serikali na Serikali ikawasikiliza? .

Kama tunazo ni zipi? . Kama hatuna kwa nini hatuna strong media?. Na jee hao waandishi strong journalists tunao?, ni kina nani wakiandika au wakisema Serikali itasikia, itabadilika?.

Mifano ya Strong Media.
US wana strong media. Wana vyama viwili vikuu vya siasa The Democrats na The Republican. Wana magazeti makuu mawili, The New York Times na The Washington Post. Pia wana TV mbili kubwa CBS na ABC.

UK pia wana Strong Media. Wana vyama vikuu viwili vya siasa, Labour na Conservative. Wana gazeti moja kuu, The Daily Telegraph. Wana radio moja kuu na TV moja kuu, BBC.

Sisi na huu utitiri wa vyama, utitiri wa magazeti, utitiri wa TV stations na utitiri wa magazeti, jee tuna any strong media ndani ya utitiri huu?.

Paskali
Ukitaka strong media tumchukue /lisu/lema/zito/lijualikali/halima mdee/ tuwapeleka journalism institute ndipo tathnia ya habari itabadilika
 
Unachokizungumza kuhusu TBC ni mambo ambayo tungetarajia iyatende kwa umma, lakini imegeuka ni chombo cha chama fulani na serekali na sio umma. Waandishi wa habari nao ugumu wa maisha umewageuza mateka wa tumbo.
TBC inapoitete serikari na chama kilichopo madarakani si ndiyo hivyo kuwatetea wananchi? Serikali ni nini? wapo kwa ajili gani? so kama TBC haiweza kusimamia misingi ya upinzani kwa kuwa upinzani unaipinga serikali na serikali inafanya kazi ya kuwatumikia wananchi... iacheni TBC ifanye kazi yake ya kuelimisha umma.
Umesema sahihi sana.Naomba nichangie kwenye ili la utitiri wa vyombo vya habari.

Ingawa uwepo wa vyombo vingi vya habari unatoa fursa za ajira kwa wananchi wenzetu.Lakini ni wakati wa kuangalia sheria ya uanzishwaji wa vyombo hivi.Sasa hivi imekua kama "fasheni" kila mkoa kuwa na either kituo cha radio/tv. Lakini hazina impact yoyote katika kukuza maendeleo/maadili na uchumi wa sehemu husika!!

Hii inatoka either na ubora na umahiri wa wanahabari hawa.
 
stong=strong
nirudi kwenye mada mimi nadhani hizo media zipo hao watu wapo tatizo moja tuu linakuja jee hao watu wapo tayari kujitenga na tumbo???wapo tayari kusimama upande wetu na sio upande wao kwa maslahi mapana ya nchi yetu??nikitendo cha kujitathmini na kuamua uelekeo wa kufuata....
Mkuu Tony Antony, kwanza asante kukubali kuwa hizo strong media zipo na hao strong brave journalists pia wapo tatizo ni tumbo. Unaweza kunifafanulia unamanisha nini? .
Paskali
 
Naunga mkono hoja ila hizo serikali za kidomokrsia zina udikiteta wake. Kitu ambacho ni kweli kuhusu serikali zote za kidikiteta zina kiuka haki za binaadamu na ku suppress the media, hakuna freedom of expression. Tanzania bado hatujafika huko na hata Zimbabwe sio udikiteta bali ni African Democracy. Kama hoja ni ile ya Mugabe kung'ang'ania madaraka, tumependekeza Magufuli apewe muda zaidi
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?
Paskali

Hamna tofauti ya haki ya binadamu inayotegemea na rangi ya ngozi!

Aidha nchi ina demokrasia au haina!

There is no such thing as "African" and "non-African" democratic system.

Basic Human Rights is a UNIVERSAL right, as declared by the United Nations.

Get your facts straight, please.
 
Mkuu Nimeguswa sana bandiko lako hili, this is very inspirational words. Mwanzo nilipanga to work out of media 2015 baada ya uchaguzi ikatokea mayai yangu yote nikayaweka kwenye kukapu kimoja, hivyo yakapasuka yote! .

Sasa nitawalk out 2020, hivyo in between najiandaa kuondoka kwa kuacha kitu. Kuna wakati nilijaribu kupitia JF, lakini nilipigwa sana madongo nika abandon.

Vipindi Maalum vya JF kwenye TV: Naomba Maoni Yako!

Kwa sasa nazifanyia kazi some of these 10 TV Programs ideas kabla sijaagana rasmi na media.

rams.
3.1 Prog. 1-KWA MASLAHI YA TAIFA- TV Political Hard Talk Show- 30min
3.2 Prog. 2-SIRI YA MAFANIKIO – Profile Program-30 min
3.3 Prog. 3- TANZANIA NA MAENDELEO- Descriptive Program 30 min
3.4 Prog. 4- KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA- Feature Program
3.5 Prog. 5- KIPINDI MAALUM- Documentary in any specific Topic-30 min
3.6 Prog. 6- PPR NEWS EXTRA- 5 Minutes News extra "Habari Zaidi ya Habari na PPR.
3.7 Prog.7- IJUE KATIBA, SHERIA NA HAKI ZAKO-30 Minutes kuhusu Katiba, sheria na haki.
3.8 Prog.8- ITS ALL ABOUT POWERS THAT MATTERS -30 Minutes TV Program about power be it Supernatural, Devine, Psychic, Meditation,Mind Over Matter etc.
3.9 Prog. 9- TULIPOTOKA, TULIPO NA TUNAPOKWENDWA -30 Minutes Program about Trends za issues za Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii.
3.10 Prog.10- HIFADHI YA JAMII NI HAKI YAKO- 30 Minutes Program kuhusu hifadhi ya Jamii ni haki kwa wote sio privilege to some or favors.

Paskali

Pascal Mayalla Shukrani sana nimesoma uzi ulioambatanisha kwa umakini sana. Kukwambia kiukweli nimehamasika na mtazamo na maono yako. Ila kuna kitu nigusie na kukufungua macho kupitia michango ya wanabodi kweye uzi ule.

Kaka yangu Paskali unachoona wewe sicho ninachoona mimi au kuna nichoona mimi na nitamani niwe wewe. Kutafuta muongozo kwenye mijadala hususani humu niwe muwazi ni kupoteza muda kwa sababu hatuko sawa.

Wakati Nokia imetawala soko la dunia Steve Jobs aliwaambia watu wake wa karibu kuwa "nakwenda kutengeneza simu so sexy kiasi watu watalamba buttons zake" na akapingwa lakini hakukata tamaa akaendelea na leo Apple Phone iko wapi???

Ukitaka kufanya mambo makubwa dont ask "the average" watakukatisha tamaa, wewe ndiye mwenye maono hivyo usiulize ushauri wa mtu wanonaje maono yako ila uliza utafikaje kule unakoona?

Usisubiri 2020 anza sasa, kwanini nasema hivyo sababu ulishawahi kuamka asubuhi ukasema sitatoa gari yangu mpaka taa zote ziwe za kijani barabarani?

Utasema resources zinakukwamisha ila unashindwa kutambua kuwa wewe ni resourceful tayari na kama hujui kuna watu wanatamani wawe wewe. Kuna watu wako tayari kufanya kazi na wewe na unataka muongozo nitakushika mkono kaka na utashangaa watavyokugombania.

Kama utaanzisha hicho kipindi kwa maslahi ya taifa utatoboa sababu ni kipindi endelevu ila hivyo tisa vingine vina time limit na hicho cha siri ya mafanikio watanzania wengi kitafanana na kipindi kama Mkasi na Vingine.

Start simple but aim Big Brother utatoboa, mfano Sporah Show started from a back room show to main stream media. Tafuta vitabu na naweza kusema be like Jeremy Pax wa tanzania in your own way unaweza Paskali. Miaka ya nyuma M.M. Mwanakijiji alikuwa na podcast zake sijui ziliishia wapi lakini kama angepata mwongozo angekuwa mbali sana.

Stop procrastinating do it now Paskali, this is your time, its a very exiting time kwa Tanzania ya leo Paskali.

N.B: Nimeandika kwa haraka sababu napeleka familia sehemu ila nitarudi hapa
 
Hii nchi ambayo Polisi wanamuua mwandishi wa Habari kwa kumpiga Bomu hadharani, Vipi mwandishi akikamatwa kwa uficho jiulize atafanywa nini?
Mkuu Bujibuji kiukweli hili tukio la kifo cha Daudi Mwangosi kiliniumiza sana hadi niliamua kuachana kabisa na hii fani ya uandishi ila kitu kikishakuwa kwenye damu kukiacha ni vigumu sana.
IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality!. Utampeleka JK The Hague-Part II!
Ni kufuatia matukio kama haya, ndio kumepelekea sheria mpya kulazimisha media kuwawekea bima ya maisha waandishi wake. Haya ni baadhi ya mambo mazuri ya sheria mpya ya Habari.

Paskali
 
Kama Strong media zenyewe ni Clouds Fm ndio iikosoe serikali basi tumeumia
Mkuu Kitumbotala, moja ya sifa kubwa ya strong media, ni zile media zinazojiendesha kwa funds kutoka vyanzo vingine ambazo hazitegemei matangazo. Clouds media sio tuu inategemea matangazo bali inajua kuzipanga vizuri na kuzicheza vizuri karata zake na mkono unaokulisha, ila kiukweli Clouds TV inafanya kazi nzuri zaidi ya ukosoaji kuliko TV nyingine yoyote kupitia kipindi chake cha 360 degrees

Kama Magufuli Anaangalia Clouds TV na Kuipongeza, Kunatuma Ujumbe Gani kwa TV yake ya TBC?!.

Zitto Zuberi Kabwe Ni Mchochezi, Akamatwe, Ashitakiwe Kwa Uchochezi, Adai Rais Magufuli ni...

Pascal
 
Makala zangu kuhusu wivu wenu dhidi ya mafanikio ya Makonda ni baadhi tuu ya my pieces of literature, kama huna uwezo wa kusoma "in between the lines, you just have completely missed the point.

Pole.

Paskali

Ni Wivu gani huo juu ya alichonacho Makonda unaouzungumzia? Huyo disgraced RC Makonda ana kitu gani wanachokosa wengine hadi watu wamwonee wivu unaoupigia jaramba?
Yaani hapo ndipo unapojiingiza katika kundi la brown envelope journalists aka wachumia tumbo.
Jaribu kutafari maneno 3 katika fani ya uandishi
1. Integrity
2. Credibility
3. Objectivity

Ukiyazingatia hayo matatu yakuongoze utafanikiwa katika fani yako
Obrigado!
 
Waandishi wengi ni njaa kali na elimu za kuunga unga.
Mkuu Prishaz, japo kuna kaukweli katika hili, ila pia kuna waandishi wa aina 3.
1. Waandishi walioingia kwenye uandishi baada ya kufeli masomo, sifa za kuingia uandishi hata DIV IV ya points 31. Hivyo wameingia ili kujiokoa tuu. Hawa elimu zao ni za kuunga unga.

2. Waandishi wenye vipaji ambao wana vipaji hata kama amepata division 0 anakuwa mwandishi. Hawa elimu zao ni za kuunga unga ila wanategemea vipaji vyao.

3. Waandishi ambao wako vizuri academically wamefanya vizuri darasani na wameingia uandishi by choice for the love of it. Hawa hawana elimu ya kuungaunga.

Hivyo sio waandishi wote ni vilaza na elimu ya kuungaunga. Kuna waandishi vichwa wa ukweli.

Paskali
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom