Medard Kalemani alikuwa Mkurugenzi wa sheria Wizara ya Madini, Mikataba ilipita kwake, anaponaje?

Prof alitumwa kwenda migodi awamu gani?? Mbona vyeo vyake ilikuw kabla awamu hii????.....au ndio amemsafisha kufukia makaburi yaliyopita?? Chongo kuwa kengeza kwa aliependa??? Sawa tutasikia mengi....nimeagiza bullet proof....na sina nkojo.....!!!!
 
Mbona ripoti imeanisha kabisa wao ndio waliomshauri waziri asisaini lakini waziri akasaini,sasa kosa lake lipo wapi kutoa ushauri wa kutokusaini kwa kuwa kampuni haijulikani ama vipi?
 
Wakuu,
Niliwahi kujiuliza maswali mengi kuhusu Medard Kalemani-Mbunge wa jimbo la Chato na Naibu, Waziri nishati na Madini. Dr. Medard Kalemani kabla ya nafasi aliyonayo hivi sasa, alikuwa mwanasheria mkuu katika hiyo hiyo ya Nishati na Madini. Hii ina maana kwamba wakati wizara hiyo ikiongozwa na mawaziri kadhaa waliopita ( William Njeleja, Sospeter Muhongo) na ambao wametajwa kwenye ripoti mbili za makinikia pamoja na ripoti za Almasi na ile ya Tanzanite, huyu bwana alikuwa mshauri mkuu wa wizara katika masuala ya sheria. Kwa mantiki hiyo ameshiriki na kushauri mikataba yote ya madini ambayo imegundulika kuwa mibovu na haina maslahi ya taifa.

Sasa kinachoshangaza ni huyu baba kujifanya watu wanaomfahamu hawajui aliyoyafanya wakati akiwa mtumishi wa umma. Busara ndogo tu ingemshauri ajiuzulu kabla mambo hayajamfikia. Nadhani anafikiria Mkulu atamteua au kumpandisha cheo kuwa waziri kamili. Jambo analosahau ni kwamba mkulu anaona huyu baba atakuwa chanzo cha kusakamwa na balaa kila siku.

Kujiondoa serikalini kutamuongezea heshima zaidi kuliko kusubiri mpaka mambo yamfikie. Ajipime na aangalie kama bado anastahili kuwa kiongozi ndani ya serikali ya Magufuli.

Leo tumeona mpaka raisi anwaambia wakae kando watu waliotajwa kwenye ripoti ya almasi na Tanzanite.

Hivi hawa mawaziri hawajioni wenyewe kuwa wamepoteza sifa zo uongozi?

Watanzania tujifunze ustaarabu wa kujipima wenyewe.
Game over
 
Mbona ripoti imeanisha kabisa wao ndio waliomshauri waziri asisaini lakini waziri akasaini,sasa kosa lake lipo wapi kutoa ushauri wa kutokusaini kwa kuwa kampuni haijulikani ama vipi?
Kwanini hakujizulu,hawa ni watu hatari sana,ndumila kuwili.
 
Mbona ripoti imeanisha kabisa wao ndio waliomshauri waziri asisaini lakini waziri akasaini,sasa kosa lake lipo wapi kutoa ushauri wa kutokusaini kwa kuwa kampuni haijulikani ama vipi?

Kalemani alihudumu wizara ya Nishati na madini kwa miaka 20,kuna Waziri aliyekaa kwa kipindi hata cha miaka 5??

Na baada ya kutoka hapo akaajiriwa na waliopewa madini yetu??Bado tumuite msafi??Duh
 
Najiuliza hili swali...

Huyu mtu ni kama "anarukwarukwa" katika tuhuma hizi za Wizara ya nishati na Madini

Mkurugenzi wa sheria ndiye "mpishi wa mikataba na mshauri mkuu wa waziri na katibu mkuu" katika masuala ya sheria

Akichemka Waziri au Katibu mkuu katika masuala ya sheria, maana yake mkurugenzi wa sheria wa wizara haponi na moja kwa moja anaonyesha hafai kwa kuwa anawapotosha wakuu wake

Namshauri Kalemani ajiondoe mwenyewe katika nafasi yake, mambo yanayosumbua taifa (mikataba ya Madini) ilipita na kuandikwa mezani kwake!

Kubaki kwake Wizarani kwa hali yoyote anaweza kuingilia uchunguzi ili ajilinde, kumbuka huyu ni NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI
Hivi mnajua kazi ya kitengo kweli ninyi,mengine mwachieni Rais,he is in control.Mnataka mkaange mpaka pilipili hoho,nyanya na vitunguu?
 
Back
Top Bottom