Kwanza poleni lakini ninawasiwasi kuwa mnanunua mechi hata hiyo kamati ya ligi kuna namna haiwezekani refa afungiwe halafu nyie mpewe ushindi.....sheria za fifa timu ina takiwa ipumzike kuanzia siku mbili kwa hiyo inarudiwa ili azam fc ichoke halafu kagera ikiifunga yanga inarudi juu what a trick lakini tutashinda na nafasi ya pili ni yetu..
hala azam fc
Ni watendaji naweza kusema baada ya yule katibu mkuu kuondoka ndiyo madudu yameongezeka amalize muda wake aondoke....Tenga ni mtu ambaye tulimwamini sana kuliendeleza soka letu lakini imekua kinyume! Yaani uongozi wake naona ndo umepoteza muelekeo wa soka kabisa na hata rank yetu inazidi kushuka.
mpambano uliomalizika dakika tano kabla ya dk 90 kumalizika umeamliwa kurudiwa. mamuzi hayo yamefikiwa na kamati ya usuruhishi inayoongozwa na Alfred Tibaigana..
Kwanza poleni lakini ninawasiwasi kuwa mnanunua mechi hata hiyo kamati ya ligi kuna namna haiwezekani refa afungiwe halafu nyie mpewe ushindi.....
Mkuu acha woga, pamoja na kunyang'anywa pointi tatu za mezani bado hata mkipoteza mechi zote mbili tayari mna pointi 53 ambazo hata kama Yanga watufunge sisi magoli mengi kiasi gani wataishia kuwa na pointi 52 tu, kwa hiyo hizo nafasi mbili za juu zimejaa kilichobaki ni nani awe wa kwanza na nani awe wa pili, Yanga waondoe kabisa kushika nafasi ya pili, wao kama wana nia ya kushiriki ya kimataifa wamwombea tu mnyama aungurume hadi hatua ya makundi tayari tutakuwa tushawakatia tiketi ya kushiriki mashindano ya shirikisho.sheria za fifa timu ina takiwa ipumzike kuanzia siku mbili kwa hiyo inarudiwa ili azam fc ichoke halafu kagera ikiifunga yanga inarudi juu what a trick lakini tutashinda na nafasi ya pili ni yetu..
hala azam fc
Una udhibitisho upi kuwa Azam wananunua mechi au ukisikia tu udaku tu basi unathibitisha?Tatizo soka la bongo maneno ni mengi sana,mechi zikiwa live watu kimya wakijua kwamba hatukuona mechi live utasikia habari kama hizi-za kuonewa,kubebwa,magoli ya offside...Yes wafungwe mechi zote mbili si kwasababu nawachukia AZAM lakini hii tabia waliyoanzisha ya kununua mechi ndio inakela haiwezekani kila mechi watu wanalaumu tu.