Kingsmann
JF-Expert Member
- Oct 4, 2018
- 4,448
- 16,311
Hili pambano wa kuamua ni baba lao TTCL tu. Huyo ndio refa pekee atakayeamua hii mechi kali yenye mitifuano na rafu za hatari.
Ni muda mrefu wateja wa hii mitandao miwili pendwa tumewalalamikia sana kuhusu vifurushi vyao hasa vya internet (data). Ulimwengu wa sasa umebadilika, watu hawatumii maongezi sana kwa mawasiliano bali wanatumia data kwa ajili ya kuwasiliana kwa njia ya social networks. Lakini hii mitandao haikusikiliza kabisa.
Raia tukaona isiwe kesi, tukahamia kwa akina TTCL na Halotel. Kule wanajali wateja wao sana, vifurushi viko affordable na vinaisha kwa uhalali tofauti na hawa Vodacom na Tigo ambao data zinaisha kwa speed ya 8G.
Sasa January mwishoni Tigo wakaboresha vifurushi vyao, wakaanza kutoa dakika za mitandao yote pamoja na kuongeza wingi wa data kwa gharama za chini kidogo. Wengi tuliwakimbilia nikiwemo mimi, niliwahama Voda baada ya miaka kama 10 ya kuwa wateja wao.
Juzi Voda nao wakaja na maboresho ya vifurushi vyao hasa vya data ambapo wakaongeza viwango vya data ambavyo viko juu kuliko vya Tigo kwa gharama ileile. Mfano Tigo kwa mwezi walikuwa wanatoa GB 13 kwa shilingi 20,000/=. Voda wao wakaja na GB 20 kwa kiwango kilekile cha 20,000/=.
Sasa Tigo walipoona wamepigwa chenga ya mwili wakasema isiwe shida, kwani kupiga counter attack shilingi ngapi?. Leo asubuhi wakaamua kuja na mabadiliko mazuri zaidi kwa sisi clients wao. Mfano mwanzo walipoboresha walikuwa wanatoa GB 5 kwa 10,000/= kwa mwezi, sasa wameongeza mpaka GB 10 kwa 10,000/= ileile. Kwa 20,000/= sasa unapata GB 22 badala ya GB 13 za mwanzo.
Hii sasa ni vita rasmi kwani lengo hapa sio kuongeza vifurushi tu bali kuvutia wateja zaidi. Tunaomba huu mpambano uendelee maana inaleta ahueni kwetu sisi watumiaji baada ya kuteseka kwa muda mrefu.
Tunaomba Voda mfanye mabadiliko tena na tena maana hamna mlichokifanya. Vifurushi vya wiki na mwezi vya data mmetoa option moja moja tuu, wakati wenzenu Tigo wana a lot of options. Voda kifurushi chenu cha wiki kinaaanzia na 15,000/= wakati Tigo wanaanzia na 3,000/=. Voda kifirushi chenu cha mwezi kinaanzia na 20,000/= tena ndio hichohicho kimoja tu wakati wenzenu Tigo wanaanzia na 5,000/=. Mpaka hapo mmeshapigwa KO. Hata mimi siwarudii ng'oo.
Mbaya zaidi mlichojichanganya nasikia mumepunguza speed ya internet yenu, 4G yenu imekuwa kama 2G.
PS: Tunasubiri mabadiliko mapya ya TTCL baba lao ili tujue tunabaki na nyie ama tunahamisha makazi Tigo moja kwa moja. Kwa mabadiliko ya Voda na Tigo ni wazi TTCL mmepigwa gap kubwa sana kwenye unafuu wa vifurushi kwa sasa. Tunategemea mje na mabadiliko mara 3 yao. Yani TTCL tunategemea mje na GB 10 kwa shilingi 5,000/= au GB 5 kwa shilingi 2,000/=.
Ni muda mrefu wateja wa hii mitandao miwili pendwa tumewalalamikia sana kuhusu vifurushi vyao hasa vya internet (data). Ulimwengu wa sasa umebadilika, watu hawatumii maongezi sana kwa mawasiliano bali wanatumia data kwa ajili ya kuwasiliana kwa njia ya social networks. Lakini hii mitandao haikusikiliza kabisa.
Raia tukaona isiwe kesi, tukahamia kwa akina TTCL na Halotel. Kule wanajali wateja wao sana, vifurushi viko affordable na vinaisha kwa uhalali tofauti na hawa Vodacom na Tigo ambao data zinaisha kwa speed ya 8G.
Sasa January mwishoni Tigo wakaboresha vifurushi vyao, wakaanza kutoa dakika za mitandao yote pamoja na kuongeza wingi wa data kwa gharama za chini kidogo. Wengi tuliwakimbilia nikiwemo mimi, niliwahama Voda baada ya miaka kama 10 ya kuwa wateja wao.
Juzi Voda nao wakaja na maboresho ya vifurushi vyao hasa vya data ambapo wakaongeza viwango vya data ambavyo viko juu kuliko vya Tigo kwa gharama ileile. Mfano Tigo kwa mwezi walikuwa wanatoa GB 13 kwa shilingi 20,000/=. Voda wao wakaja na GB 20 kwa kiwango kilekile cha 20,000/=.
Sasa Tigo walipoona wamepigwa chenga ya mwili wakasema isiwe shida, kwani kupiga counter attack shilingi ngapi?. Leo asubuhi wakaamua kuja na mabadiliko mazuri zaidi kwa sisi clients wao. Mfano mwanzo walipoboresha walikuwa wanatoa GB 5 kwa 10,000/= kwa mwezi, sasa wameongeza mpaka GB 10 kwa 10,000/= ileile. Kwa 20,000/= sasa unapata GB 22 badala ya GB 13 za mwanzo.
Hii sasa ni vita rasmi kwani lengo hapa sio kuongeza vifurushi tu bali kuvutia wateja zaidi. Tunaomba huu mpambano uendelee maana inaleta ahueni kwetu sisi watumiaji baada ya kuteseka kwa muda mrefu.
Tunaomba Voda mfanye mabadiliko tena na tena maana hamna mlichokifanya. Vifurushi vya wiki na mwezi vya data mmetoa option moja moja tuu, wakati wenzenu Tigo wana a lot of options. Voda kifurushi chenu cha wiki kinaaanzia na 15,000/= wakati Tigo wanaanzia na 3,000/=. Voda kifirushi chenu cha mwezi kinaanzia na 20,000/= tena ndio hichohicho kimoja tu wakati wenzenu Tigo wanaanzia na 5,000/=. Mpaka hapo mmeshapigwa KO. Hata mimi siwarudii ng'oo.
Mbaya zaidi mlichojichanganya nasikia mumepunguza speed ya internet yenu, 4G yenu imekuwa kama 2G.
PS: Tunasubiri mabadiliko mapya ya TTCL baba lao ili tujue tunabaki na nyie ama tunahamisha makazi Tigo moja kwa moja. Kwa mabadiliko ya Voda na Tigo ni wazi TTCL mmepigwa gap kubwa sana kwenye unafuu wa vifurushi kwa sasa. Tunategemea mje na mabadiliko mara 3 yao. Yani TTCL tunategemea mje na GB 10 kwa shilingi 5,000/= au GB 5 kwa shilingi 2,000/=.