Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
NA; BAHATI K MWAMBA
-----1------
Kikao cha watu watatu kiliendelea na kila Mjumbe, tayari alishatoa wazo lake aliloona ni sahihi kwa wakati huo. Makubaliano ya hapa na pale yalifikiwa, lakini ukaibuka utata kwenye hitaji lao la mwisho, na lilowafanya wakutane siku hiyo.
Maongezi yao yalihama kuwa ya kibiashara, yakaelekea kuwa ya kibabe na kila mmoja akitaka hoja yake ipite bila kupingwa.
Wazee hawa wenye umri sawa, walivimbiana huku kila mmoja akijinasibu kwa sifa zake, achilia mbali uwezo wa fedha na, mali walizomiliki ambapo; Mali zote hazikupatikana kwa njia halali na hilo ndilo, lilifanya uibuke mzozo, kwa kuwa kila mmoja alikuwa na aina ya watu ambao, aliwatumia ili kutimiza ujazo wa mifuko yake.
Ukiachilia mbali wazee hawa kuibuka kuwa wenye ukwasi wa kutisha, pia walikuwa ni wasitaafu wa jeshi, wakiwa na vyeo vya chini kabisa.
Kila aliyewafahamu, alijiuliza ukwasi huo waliupata vipi ikiwa, mafao yao yalikuwa hayawezi kuwafikisha kwenye kilele cha ubilionea. Wengine walidhani watakuwa walienda kuroga ili wasife masikini, huku wengine wakidhani walikopa bank ili waziishi ndoto zao.
Mengi yalisemwa, lakini ni wao waliofahamu ukwasi huo waliupata vipi.
Wakati watu wakishangaa utajiri huo wa baada ya kustaafu, lakini wao walianza kuuishi miaka mingi hata wingali kazini. Waliufanya kuwa siri, huku wakiendelea kufanya unyama wa hapa na pale, ili kutunisha hazina zao.
Lakini waliendelea kujivika mwamvuli wa kazi, huku kazi zao zikifanywa na watu maalumu wa kukodi. Watu hawa maalumu ndiyo waliozua zogo kwenye kikao chao hicho, kila mmoja aliamini mtu wake ni sahihi kuifanya kazi waliokusudia kuifanya.
Si kwamba watu hao wa kununua hawakuwafahamu kwa ujumla wao; la hasha, waliwafahamu vema lakini, kila mmoja alimwamini yule alieyefanya nae kazi kwa muda mrefu na kwa uaminifu mkubwa.
“Jamani eeh, hebu tusigombane. Sisi sote ni BoysAmongMen, ni lazima tukubaliane kwa sauti moja bila kukwazana” Alizungumza Mzee mmoja ambae hupenda kujiita Rich'one.
Ukapita ukimya mfupi huku kila mmoja akijaribu kushusha morali yake.
“Mimi bado naona hii kazi tumpe Kiuno cha nyoka, huyu bwana anaijua kazi yake vilivyo na mazingira yoyote anaweza kufanya kazi yake.” Alizungumza mzee mwingine, ambae alipenda kujiita Omega'one.
“Lakini nabaki na msimamo wangu, Kiuono cha nyoka hawezi kuifanya kazi hii. Kwanza anatamaa sana, pia ni mtu asie na msimamo kabisa. Akipata dili lenye pesa kubwa, ni rahisi kuitosa kazi yetu.” Alizungumza Rich'one huku akiwatizama wenzake kwa umakini, kuona kama hoja yake inawaingia.
“Tukisema kila mmoja ampambe mtu wake, hakuna mbabe kati yao, maana, kila mmoja atakuwa na sifa sawa na zile za mwenzake kwa kuwa, sifa zote zitakuwa ni za weledi wa kufanya kazi kwa usahihi” Omega aliongea huku akiwatizama wenzake kwa utulivu mkubwa na kufanya umakini, uongezeke miongoni mwao.
Alipohakikisha wenzake wametulia na wanamsikiliza, aliendelea.
“Sifa zote tumezisikia na sasa ni wakati wa kuweka majina yote mezani, kisha tuchambue sifa zao zote kwa umakini na, tutoke na jina moja lenye nguvu.”
Mzee aliyependa kujiita Omega'one alikaa vema kwenye kiti, huku akisubiri wenzake watekeleze wazo lake.
“Mm-mh-mh-...” Mzee mwingine ambae alikuwa kimya kwa muda mrefu, alirekebisha koo na kujiweka vema ili aongee jambo lake.
Wenzake walikaa kimya na kumsikiliza.
“Mawazo yenu yako sawa kabisa. Boys among men, daima huwa hatogombani kirejareja namna hii, bali huwa tunaamua wazo moja lenye tija.” Alinyamaza kidogo na kuwatazama wenzake, kisha alipoona wanamsikiliza, aliendelea..
“Mmewataja watu wenu na sifa zao; mmemtaja Kiuno cha nyoka na
Tembe za chai, kama ni watu makini na hatari kwenye kufanikisha matukio makubwa na yenye kuogofya.” Alinyamaza na kuwatizama tena wenzake, ambao walikuwa wamekaa kimya wakimsikiliza.
Aliendelea..
“Lakini pengine hamjapima uzito wa Nazi hii tunayowapa. Kazi hii inaugumu kwa kiasi kikubwa na inahitaji mtu makini sana na mwenye kutumia akili, kuliko nguvu na uchawi. Mtu huyu pia awe ni mwenye ujuzi wa mapigano na mwenye kujua kuitumia vema silaha yoyote, awe ni mwenye kuendesha chombo chochote cha moto, awe ni mtu ambae amefunga mkataba na kifo, wakati wowote kikimuita yuko tayari kukipokea. Mtu huyu awe zaidi ya komando wa jeshi la uzunguni.” Mzee yule alimaliza kuongea na kuegemea mwenye kiti alichokalia, huku macho yake yakihama; kutoka kushoto kwenda kulia na kulia kwenda kushoto. Aliwatizama wenzake ambao walikuwa kimya wakitafakari uzito wa hoja ya Alfa'one, ambae mara nyingi walimheshimu kwa busara zake miongoni mwao.
“Kwa hiyo unashauri tuachane na hawa jamaa?” Rich'one alimuuliza.
“Hapana! Hawa hawa wanatosha, lakini tuchague mmoja ambae anaweza kupiga vita peke yake kwenye nchi ngeni” Alijibu.
“Unahisi ni yupi anaefaa kuibeba kazi hii?” Omega'one aliuliza.
“Wote wanafaa kuibeba kazi hii, lakini nampendekeza zaidi huyu jamaa anaeitwa Miguu ya Kuku.”
Ukapita ukimya mfupi kila mmoja akitafakari la kwake kisha, ukimya ule ukavunjwa kabla ya dakika haijaisha.
“Unahisi huyu jamaa anasifa gani kubwa, kuliko wenzake tuliowataja?” Rich'one aliuliza.
“Huyu jamaa anapiga kila aina ya mapigo unayoyajua, anapiga hadi suplex lakini kubwa zaidi, huyu jamaa ni mdunguaji aliyekamilika”
Wenzake walitumbua macho kwa kutomuelewa, nae akaamua kuwaelewesha.
“Hii ni kazi ya nje ya nchi na hatuwezi jua ataenda kukabiliana na magumu gani huko aendako na atatumia mbinu gani, kuhakikisha kila kitu kinaenda vile ilivyopangwa. Ni vema kumpeleka mtu ambae anajua kila aina ya mapambano ili lengo letu litimie” Alinyamaza tena na kuwatizama wenzake, kisha akaendelea kumpamba Miguu ya Kuku.
“Huyu jamaa angelikuwa mwanajeshi basi, angelikuwa anashikilia rekodi ya mdunguaji bora duniani. Anaweza kudungua kitu chenye unene wa kidole, akiwa umbali wa mita mia tano. Pia anaweza kubapata shabaha yake ndani ya sekunde mbili tu, baada ya kufyatua risasi ya kwanza. Anakimbia mita mia moja kwa sekunde nane tu, pia aliitwa Miguu ya Kuku kwa sababu hatoi kishindo na mguu wake mmoja una vidole vinne tu. Sasa kwa sifa hizo kuna mdunguaji gani hapa duniani anaweza kumfikia? Nani anaweza kupambana nae ikiwa anapiga kila aina ya mipigo pia, anatumia akili nyingi kupata windo lake kuliko nguvu.” Alfa’one akatua maelezo yake.
“Duh, huyu kweli kiboko!” Omega’one akaongea kwa mshangao huku akijiweka sawa kwenye kiti.
“Hata mimi ameanza kuniingia hivi” Rich’one nae akaunga hoja.
“Lakini nisingependa nichukue mawazo yenu, nataka tujiridhishe na uwezo wa watu hawa wote, kabla hatujatuma mtu huko Goma.” Alfa'one aliwambia wenzake.
“Unataka kusema nini tena?” Omega’one aliuliza.
“Nataka tuwachambue kwanza” Alijibiwa.
“Uchambuzi tena wa nini ikiwa sifa zote umempa? Haina haja bwana, kuendelea kumjadili ni kupoteza rasilimali muda.”
“Hapana Boy. Lengo langu nataka tupate mtu miongoni mwa watu. Mtu wa kazi, mtu anaweza kuwakalisha watu wengine wenye sifa kama zake”
“Eleza lengo lako, pengine tunaweza kuelewana.”
“Namaanisha hawa watu wote watatu tuwapambanishe hapa mjini, kisha mshindi apewe kazi ya kwenda huko Goma”
“Lakini unajua hawa watu huwa hawatoi jasho bila kulipwa?”
“Hilo nalijua, lakini tusiogope garama kama tunahitaji kupata mali zetu zenye ukwasi wa kutosha. Wapewe kazi ya kutafutana wao kwa wao, kisha mbabe anapewa tenda”
“Lakini unajua hawa mamluki mara nyingi huwa hayapendi kushindwa, inaweza kutoke mmoja akashindwa lakini akaenda kuanzisha vita itakayochafua mji wote wa Dar es laam”
“Hapa sheria itakayotumika si kumuacha aliyeshindwa akiwa hai. Hapa inabidi ipigwe DOA mzee.”
“DOA! Unamaana gani?”
“Namaanisha Dead or Alive”
“Hii ni hatari sasa na wakigundua tunawachezeshea kamari na wakatugeuka itakuwaje?”
“Usisahau wewe ni mstaafu ambae umepigana vita ndani ya Katanga, Kivu yote ukiwa chini ya amri ya walinda amani na, kumbuka; once a soldier always remain a soldier na, mwenye akili ndiye mshindi”
Ukapita ukimya kila mmoja akiwaza lake.
“Alfa yupo sahihi, lazima tuchuje pumba na mchele ili tusije kimbilia tui, tukidhani ni maziwa.” Rich’one alikubaliana na hoja.
“Tuko pamoja Boys” Omega’one alikubaliana na wenzake, kisha akauliza.
“Hatua gani zinafuata?”
“Kila mtu ampe taarifa mtu wake, kisha wote wakutane jengo la mauzo, gorofa namba tano kwenye duka la simu na wachukue mkoba mweusi watakoukuta humo” Alfa alitoa mkakati wake.
“Sasa itakuwaje mmoja akiwahi kuuchukua mkoba na kuufikisha sehemu husika kabla ya wenzake?” Rich’one alitoa wasiwasi wake.
“Mamluki hawako hivyo, huwa hawana haraka ya kioga hivyo na kazi yoyote mezani kwao, huwa ni kiashiria cha hatari hata kama kapewa kazi ya kumchamba mtoto, ni lazima atie wasiwasi” Alfa alifafanua.
“Basi waingie mzigoni kesho”
“Yeah, Kesho mji utachafuka si kitoto”
“Hahaa! Sisi ndo wazee vijana, Boys among men…” Alfa alicheka kifedhuli huku akiichukua simu yake ya garama kubwa na kulitafuta jina la Miguu ya Kuku.
Wakati yeye akiwasiliana na Miguu ya Kuku, Omega yeye alikuwa anawasiliana na Kiuno cha nyoka na Rich’one aliwasiliana na Tembe za chai.
Walikuwa wanatengeneza bomu la kulipua nyoyo za wakazi wa jiji la Dar es laamu na viunga vyake.
Lakini kitu ambacho hawakujua ni kuwa, chatu hafugwi ndani ya nyumba, kwa kuwa ipo siku atakugeuka.
Dar ikawa ya moto.
*****
Endelea kuwa nami hadi mwisho wa kazi hii
-----1------
Kikao cha watu watatu kiliendelea na kila Mjumbe, tayari alishatoa wazo lake aliloona ni sahihi kwa wakati huo. Makubaliano ya hapa na pale yalifikiwa, lakini ukaibuka utata kwenye hitaji lao la mwisho, na lilowafanya wakutane siku hiyo.
Maongezi yao yalihama kuwa ya kibiashara, yakaelekea kuwa ya kibabe na kila mmoja akitaka hoja yake ipite bila kupingwa.
Wazee hawa wenye umri sawa, walivimbiana huku kila mmoja akijinasibu kwa sifa zake, achilia mbali uwezo wa fedha na, mali walizomiliki ambapo; Mali zote hazikupatikana kwa njia halali na hilo ndilo, lilifanya uibuke mzozo, kwa kuwa kila mmoja alikuwa na aina ya watu ambao, aliwatumia ili kutimiza ujazo wa mifuko yake.
Ukiachilia mbali wazee hawa kuibuka kuwa wenye ukwasi wa kutisha, pia walikuwa ni wasitaafu wa jeshi, wakiwa na vyeo vya chini kabisa.
Kila aliyewafahamu, alijiuliza ukwasi huo waliupata vipi ikiwa, mafao yao yalikuwa hayawezi kuwafikisha kwenye kilele cha ubilionea. Wengine walidhani watakuwa walienda kuroga ili wasife masikini, huku wengine wakidhani walikopa bank ili waziishi ndoto zao.
Mengi yalisemwa, lakini ni wao waliofahamu ukwasi huo waliupata vipi.
Wakati watu wakishangaa utajiri huo wa baada ya kustaafu, lakini wao walianza kuuishi miaka mingi hata wingali kazini. Waliufanya kuwa siri, huku wakiendelea kufanya unyama wa hapa na pale, ili kutunisha hazina zao.
Lakini waliendelea kujivika mwamvuli wa kazi, huku kazi zao zikifanywa na watu maalumu wa kukodi. Watu hawa maalumu ndiyo waliozua zogo kwenye kikao chao hicho, kila mmoja aliamini mtu wake ni sahihi kuifanya kazi waliokusudia kuifanya.
Si kwamba watu hao wa kununua hawakuwafahamu kwa ujumla wao; la hasha, waliwafahamu vema lakini, kila mmoja alimwamini yule alieyefanya nae kazi kwa muda mrefu na kwa uaminifu mkubwa.
“Jamani eeh, hebu tusigombane. Sisi sote ni BoysAmongMen, ni lazima tukubaliane kwa sauti moja bila kukwazana” Alizungumza Mzee mmoja ambae hupenda kujiita Rich'one.
Ukapita ukimya mfupi huku kila mmoja akijaribu kushusha morali yake.
“Mimi bado naona hii kazi tumpe Kiuno cha nyoka, huyu bwana anaijua kazi yake vilivyo na mazingira yoyote anaweza kufanya kazi yake.” Alizungumza mzee mwingine, ambae alipenda kujiita Omega'one.
“Lakini nabaki na msimamo wangu, Kiuono cha nyoka hawezi kuifanya kazi hii. Kwanza anatamaa sana, pia ni mtu asie na msimamo kabisa. Akipata dili lenye pesa kubwa, ni rahisi kuitosa kazi yetu.” Alizungumza Rich'one huku akiwatizama wenzake kwa umakini, kuona kama hoja yake inawaingia.
“Tukisema kila mmoja ampambe mtu wake, hakuna mbabe kati yao, maana, kila mmoja atakuwa na sifa sawa na zile za mwenzake kwa kuwa, sifa zote zitakuwa ni za weledi wa kufanya kazi kwa usahihi” Omega aliongea huku akiwatizama wenzake kwa utulivu mkubwa na kufanya umakini, uongezeke miongoni mwao.
Alipohakikisha wenzake wametulia na wanamsikiliza, aliendelea.
“Sifa zote tumezisikia na sasa ni wakati wa kuweka majina yote mezani, kisha tuchambue sifa zao zote kwa umakini na, tutoke na jina moja lenye nguvu.”
Mzee aliyependa kujiita Omega'one alikaa vema kwenye kiti, huku akisubiri wenzake watekeleze wazo lake.
“Mm-mh-mh-...” Mzee mwingine ambae alikuwa kimya kwa muda mrefu, alirekebisha koo na kujiweka vema ili aongee jambo lake.
Wenzake walikaa kimya na kumsikiliza.
“Mawazo yenu yako sawa kabisa. Boys among men, daima huwa hatogombani kirejareja namna hii, bali huwa tunaamua wazo moja lenye tija.” Alinyamaza kidogo na kuwatazama wenzake, kisha alipoona wanamsikiliza, aliendelea..
“Mmewataja watu wenu na sifa zao; mmemtaja Kiuno cha nyoka na
Tembe za chai, kama ni watu makini na hatari kwenye kufanikisha matukio makubwa na yenye kuogofya.” Alinyamaza na kuwatizama tena wenzake, ambao walikuwa wamekaa kimya wakimsikiliza.
Aliendelea..
“Lakini pengine hamjapima uzito wa Nazi hii tunayowapa. Kazi hii inaugumu kwa kiasi kikubwa na inahitaji mtu makini sana na mwenye kutumia akili, kuliko nguvu na uchawi. Mtu huyu pia awe ni mwenye ujuzi wa mapigano na mwenye kujua kuitumia vema silaha yoyote, awe ni mwenye kuendesha chombo chochote cha moto, awe ni mtu ambae amefunga mkataba na kifo, wakati wowote kikimuita yuko tayari kukipokea. Mtu huyu awe zaidi ya komando wa jeshi la uzunguni.” Mzee yule alimaliza kuongea na kuegemea mwenye kiti alichokalia, huku macho yake yakihama; kutoka kushoto kwenda kulia na kulia kwenda kushoto. Aliwatizama wenzake ambao walikuwa kimya wakitafakari uzito wa hoja ya Alfa'one, ambae mara nyingi walimheshimu kwa busara zake miongoni mwao.
“Kwa hiyo unashauri tuachane na hawa jamaa?” Rich'one alimuuliza.
“Hapana! Hawa hawa wanatosha, lakini tuchague mmoja ambae anaweza kupiga vita peke yake kwenye nchi ngeni” Alijibu.
“Unahisi ni yupi anaefaa kuibeba kazi hii?” Omega'one aliuliza.
“Wote wanafaa kuibeba kazi hii, lakini nampendekeza zaidi huyu jamaa anaeitwa Miguu ya Kuku.”
Ukapita ukimya mfupi kila mmoja akitafakari la kwake kisha, ukimya ule ukavunjwa kabla ya dakika haijaisha.
“Unahisi huyu jamaa anasifa gani kubwa, kuliko wenzake tuliowataja?” Rich'one aliuliza.
“Huyu jamaa anapiga kila aina ya mapigo unayoyajua, anapiga hadi suplex lakini kubwa zaidi, huyu jamaa ni mdunguaji aliyekamilika”
Wenzake walitumbua macho kwa kutomuelewa, nae akaamua kuwaelewesha.
“Hii ni kazi ya nje ya nchi na hatuwezi jua ataenda kukabiliana na magumu gani huko aendako na atatumia mbinu gani, kuhakikisha kila kitu kinaenda vile ilivyopangwa. Ni vema kumpeleka mtu ambae anajua kila aina ya mapambano ili lengo letu litimie” Alinyamaza tena na kuwatizama wenzake, kisha akaendelea kumpamba Miguu ya Kuku.
“Huyu jamaa angelikuwa mwanajeshi basi, angelikuwa anashikilia rekodi ya mdunguaji bora duniani. Anaweza kudungua kitu chenye unene wa kidole, akiwa umbali wa mita mia tano. Pia anaweza kubapata shabaha yake ndani ya sekunde mbili tu, baada ya kufyatua risasi ya kwanza. Anakimbia mita mia moja kwa sekunde nane tu, pia aliitwa Miguu ya Kuku kwa sababu hatoi kishindo na mguu wake mmoja una vidole vinne tu. Sasa kwa sifa hizo kuna mdunguaji gani hapa duniani anaweza kumfikia? Nani anaweza kupambana nae ikiwa anapiga kila aina ya mipigo pia, anatumia akili nyingi kupata windo lake kuliko nguvu.” Alfa’one akatua maelezo yake.
“Duh, huyu kweli kiboko!” Omega’one akaongea kwa mshangao huku akijiweka sawa kwenye kiti.
“Hata mimi ameanza kuniingia hivi” Rich’one nae akaunga hoja.
“Lakini nisingependa nichukue mawazo yenu, nataka tujiridhishe na uwezo wa watu hawa wote, kabla hatujatuma mtu huko Goma.” Alfa'one aliwambia wenzake.
“Unataka kusema nini tena?” Omega’one aliuliza.
“Nataka tuwachambue kwanza” Alijibiwa.
“Uchambuzi tena wa nini ikiwa sifa zote umempa? Haina haja bwana, kuendelea kumjadili ni kupoteza rasilimali muda.”
“Hapana Boy. Lengo langu nataka tupate mtu miongoni mwa watu. Mtu wa kazi, mtu anaweza kuwakalisha watu wengine wenye sifa kama zake”
“Eleza lengo lako, pengine tunaweza kuelewana.”
“Namaanisha hawa watu wote watatu tuwapambanishe hapa mjini, kisha mshindi apewe kazi ya kwenda huko Goma”
“Lakini unajua hawa watu huwa hawatoi jasho bila kulipwa?”
“Hilo nalijua, lakini tusiogope garama kama tunahitaji kupata mali zetu zenye ukwasi wa kutosha. Wapewe kazi ya kutafutana wao kwa wao, kisha mbabe anapewa tenda”
“Lakini unajua hawa mamluki mara nyingi huwa hayapendi kushindwa, inaweza kutoke mmoja akashindwa lakini akaenda kuanzisha vita itakayochafua mji wote wa Dar es laam”
“Hapa sheria itakayotumika si kumuacha aliyeshindwa akiwa hai. Hapa inabidi ipigwe DOA mzee.”
“DOA! Unamaana gani?”
“Namaanisha Dead or Alive”
“Hii ni hatari sasa na wakigundua tunawachezeshea kamari na wakatugeuka itakuwaje?”
“Usisahau wewe ni mstaafu ambae umepigana vita ndani ya Katanga, Kivu yote ukiwa chini ya amri ya walinda amani na, kumbuka; once a soldier always remain a soldier na, mwenye akili ndiye mshindi”
Ukapita ukimya kila mmoja akiwaza lake.
“Alfa yupo sahihi, lazima tuchuje pumba na mchele ili tusije kimbilia tui, tukidhani ni maziwa.” Rich’one alikubaliana na hoja.
“Tuko pamoja Boys” Omega’one alikubaliana na wenzake, kisha akauliza.
“Hatua gani zinafuata?”
“Kila mtu ampe taarifa mtu wake, kisha wote wakutane jengo la mauzo, gorofa namba tano kwenye duka la simu na wachukue mkoba mweusi watakoukuta humo” Alfa alitoa mkakati wake.
“Sasa itakuwaje mmoja akiwahi kuuchukua mkoba na kuufikisha sehemu husika kabla ya wenzake?” Rich’one alitoa wasiwasi wake.
“Mamluki hawako hivyo, huwa hawana haraka ya kioga hivyo na kazi yoyote mezani kwao, huwa ni kiashiria cha hatari hata kama kapewa kazi ya kumchamba mtoto, ni lazima atie wasiwasi” Alfa alifafanua.
“Basi waingie mzigoni kesho”
“Yeah, Kesho mji utachafuka si kitoto”
“Hahaa! Sisi ndo wazee vijana, Boys among men…” Alfa alicheka kifedhuli huku akiichukua simu yake ya garama kubwa na kulitafuta jina la Miguu ya Kuku.
Wakati yeye akiwasiliana na Miguu ya Kuku, Omega yeye alikuwa anawasiliana na Kiuno cha nyoka na Rich’one aliwasiliana na Tembe za chai.
Walikuwa wanatengeneza bomu la kulipua nyoyo za wakazi wa jiji la Dar es laamu na viunga vyake.
Lakini kitu ambacho hawakujua ni kuwa, chatu hafugwi ndani ya nyumba, kwa kuwa ipo siku atakugeuka.
Dar ikawa ya moto.
*****
Endelea kuwa nami hadi mwisho wa kazi hii