Mdude Nyangali arejesha fomu ya kuomba Uenyekiti wa Taifa BAVICHA

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
116,495
215,349
Rasmi leo nimerudisha fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti baraza la vijana chad ( 800 X 640 ).jpg

Unaambiwa siasa za awamu hii ni zile siasa ngumu kabisa , ni siasa za vitendo zaidi badala ya maneno , ni siasa za jasho na damu .

Wanatakiwa Vijana shupavu wasioogopa kuuawa .
 
Kila la kheri kwake ila tumeona wengi sana waliobadilika baada tu ya kuonja joto yao wasiojulikana. Huyu naye asije badilika. Tz hajawahi kutokea mbabe wa siasa ka Mtikila RIP. Lakini baada ya kupitia mikononi mwao, mbona tulidhani katokea photo copy???
Be ware CDM na waliokwisha onja utamu wa wasiojulikana
 
Siku ambayo mdude anakuwa mwenyekiti chadema wenye akili wote wanajiondoa au kuhama chama.muwe serious na chama nyie CDM hivi mnadhani every tom,dick and harry anaweza kuwa mwenyekiti wa chama ?kama ni kikundi cha wana harakati sawa.mdude huyu ambaye anakosa hata busara ya kujua aandike nini kuwasilisha mawazo mazuri leo mnataka awe mwenyekiti?kuweni serious kidogo.

Wapiga kura wataamua
 
Siku ambayo mdude anakuwa mwenyekiti chadema wenye akili wote wanajiondoa au kuhama chama.muwe serious na chama nyie CDM hivi mnadhani every tom,dick and harry anaweza kuwa mwenyekiti wa chama ?kama ni kikundi cha wana harakati sawa.mdude huyu ambaye anakosa hata busara ya kujua aandike nini kuwasilisha mawazo mazuri leo mnataka awe mwenyekiti?kuweni serious kidogo.
Huyu unayemtukana hapa ni ofisa wa chama kanda ya Nyasa , kama mlitaka siasa za kistaarabu kwanini Heri James hamumuonyi , Bashiru uchafu anaouropoka kule Zanzibar ndio ustaarabu ule ?
 
Sijui kama watakuelewa.maana wanaanza kuwa kama mazezeta.ni aibu mdude kuwa mwenyekiti wa chadema.aibu kubwa sana.hakupaswa hata kufikiriwa. Ingawa ni haki yake kikatiba
Kwani yukoje mkuu..!? Au anatakiwa mwenyekiti dingi? Mi naona sio mbaya vijana kama yeye kutjitokeza na angalau anaweka historia na anajiongezea CV pia!
 
Mimi binafsi nampenda sana Mdude Nyangali kwa uthubutu wake na kutokuwa muoga. Lakini kupewa udereva wa BAVICHA TAIFA hapana. Hicho cheo inataka watu kama alivyokuwa Heche. Mtu makini lakini sio mwoga, mwenye kuchuja maneno ayasemayo.
Kuongoza chama sio kila wakati ni vita tuu Bali kuna wakati wa kuwa soft kidogo na kujadiliana.
Mdude nafasi kuu ya maamuzi bado hajaweza kuruhusiwa kuipewa, labda zingine kama makamu, katibu wa uenezi nk nk ambazo anaweza kudhibitiwa.
Sina namna ya kuwasiliana naye ningeweza kumshauri vinginevyo. Maana watu aina ya Mdude naye akikosa nafasi hiyo anaweza tena kujikuta kageuka sumu kwa chama chake.
Mdude kama utasoma ujumbe huu ACHANA NA UENYEKITI utumikie chama kwa njia zingine.
 
33 Reactions
Reply
Back
Top Bottom