GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,871
Unakuja Simba SC mdogo wangu hapo utapata Namba ya nani? Kwanini hupendi kusikia Mawazo ya Kaka zako ambao tunakupenda Ibra? Hivi kweli kwa Mfumo wa Kocha Aussems Wewe utapata Namba kweli ndani ya Kikosi cha Simba hii ya sasa Ibra? Ni kwanini Maisha ya hapa Dar es Salaama yanakulevya na yanakuridhisha hivi Mdogo wangu Ibra? Najua kuwa umeshawishiwa na Rafiki zako wakubwa akina Mkude, Ndemla na Tshabalala ila nawe pia ulipaswa ujitathmini Kwanza kabla ya Kuamua ulichoamua Ibra.
Mimi GENTAMYCINE ni Kaka yako, Rafiki yako mzuri tu tena tokea ukiwa Boom FC na wakati ukicheza pia pale Uwanja wa Shule ya Msimbazi achilia mbali Uwanja wa Barafu, ule wa Tanganyika Packers Kawe na hata pale Biafra ukiwa na ' Washikaji ' zako akina Mkude na Sure Boy wa Azam na unajua fika kuwa Mimi ni mwana Simba SC lia lia ila nilikushauri kuwa usije Simba SC na kukupa Sababu zangu nyingi ila kuna Mtu wako wa karibu yupo TRA Makao Makuu ' amenitonya ' kuwa jana ulikuwa na Viongozi wa Simba na huenda ndani ya Saa 48 au 72 kutoka sasa ukasaini rasmi Simba SC.
Nilikushauri vizuri sana Mdogo wangu Ibra kuwa kwa Mafanikio yako makubwa ya Kimpira ni vyema ukaondoka kabisa Tanzania hii ili ' ukatengenezwe ' zaidi na Makocha wakubwa wa Timu zingine na nakumbuka ulipopata ' Offer ' ya TP Mazembe nilifurahi mno na kujua kuwa usingeiacha hiyo bahati na kwa masikitiko makubwa sana nikaja kuambiwa kuwa ' umewachomolea ' kwakuwa tu Simba SC wanakuhitaji na Wewe umekubali kabisa kuingia ' Mtegoni ' na unaelekea Kusaini nao.
Ibra Mdogo wako kutoka Ilala Bungoni najua kuwa umeangalia Pesa na Maisha mazuri ya hapa Jijin Dar es Salaam hasa ukizingatia kuwa unapenda sana Starehe ila ipo Siku utakuja Kunikumbuka Mimi Kaka yako GENTAMYCINE na naamini hata Rafiki yako mkubwa SaluRaka ambaye sasa yupo nchini Ujerumani ( baada ya Kujilipua / Kuchukua Uraia wa huko kama Mkimbizi ) nae akisikia kuwa umekataa kwenda TP Mazembe atakushangaa achilia mbali Kaka yake Hemed wa TRA ambaye ndiyo Mshauri wako Mkuu najua nae pia atakuwa amesikitika mno tu.
Hivi Ibra ungevumilia tu uende zako TP Mazembe ukapikwe na ukatengenezwe hata kwa miaka yako miwili na ukomae vyema unataka kuniambia na Wewe Vilabu vikubwa vya Ulaya visingekuona na Kukusajili? Ibra ni mara ngapi Mwenzako Mbwana Samatta amekuwa akikuambia Wewe na Rafiki yako Mkude kuwa mnachelewa hapa Tanzania na kwamba nyie ni wa Ulaya tu? Hivi hamuoni Mafanikio yake huko KRC Genk?
Najua mida ya baadae tunaweza Kukutana maeneo ya Morocco Hotel katika Duka za Mke wa Mchezaji mwenzako wa Yanga Beki Gadiel Michael ambako huwa unapenda kuwa hapo ukiwa na Wachezaji wenzako bila Kumsahau Beki Mtukutu na Kaka yako Kelvin Yondan ila nimelazimika Kuja na hii ' Kitu ' hapa ili kuwa ' Funzo ' kwa Wachezaji wengine kuwa achaneni na mawazo ' Finyu ' kuwa Maendeleo ya Mchezaji basi ni lazima tu achezee Klabu za Simba na Yanga wakati kumbe ukweli siyo huo.
Nina uhakika kuwa kwa hili Bandiko langu kuna wana Simba SC Wenzangu watanikasirikia kama siyo kuninunia kwakuwa sijapendelea Ibra kuja Simba SC yetu ila ' Kiufundi ' kabisa na ninavyomjua Ibrahim Ajibu alivyo na Kocha wetu wa Simba SC hatoweza kupata Nafasi ya Kudumu Kikosini na atasubiri mno kwa akina Chama, Niyonzima, Muzamiri na hata Ndemla ila kwa Maendeleo yake ya Kimpira angeenda Azam FC angepata Namba tena ya Kudumu ila angeenda huko TP Mazembe au hata Ulaya angefanya vyema zaidi.
Nimefurahi tu Kusikia kwamba Simba SC inamrudisha Beki wetu wa Vijana William Lucien ' Gallas ' ili aje acheze Namba yake ya Kiasili Beki Namba Mbili kwani si uwongo sikufurahishwa na Usajili wa Beki wa ' hovyo hovyo ' ambaye Kiwango chake Kimeshuka kama si Kupotea ghafla Zana Coulibaly na nasikia kuwa anaachwa rasmi ili Nafasi hiyo ya Beki Namba Mbili ibaki tu kwa Nicolas Gyan, William Lucien na Majeruhi Shomary Kapombe.
Mdogo wangu Ibrahim Ajib umeniangusha sana Kaka yako Mimi GENTAMYCINE ila nayaheshimu pia Maamuzi yako.
Nawasilisha.
Mimi GENTAMYCINE ni Kaka yako, Rafiki yako mzuri tu tena tokea ukiwa Boom FC na wakati ukicheza pia pale Uwanja wa Shule ya Msimbazi achilia mbali Uwanja wa Barafu, ule wa Tanganyika Packers Kawe na hata pale Biafra ukiwa na ' Washikaji ' zako akina Mkude na Sure Boy wa Azam na unajua fika kuwa Mimi ni mwana Simba SC lia lia ila nilikushauri kuwa usije Simba SC na kukupa Sababu zangu nyingi ila kuna Mtu wako wa karibu yupo TRA Makao Makuu ' amenitonya ' kuwa jana ulikuwa na Viongozi wa Simba na huenda ndani ya Saa 48 au 72 kutoka sasa ukasaini rasmi Simba SC.
Nilikushauri vizuri sana Mdogo wangu Ibra kuwa kwa Mafanikio yako makubwa ya Kimpira ni vyema ukaondoka kabisa Tanzania hii ili ' ukatengenezwe ' zaidi na Makocha wakubwa wa Timu zingine na nakumbuka ulipopata ' Offer ' ya TP Mazembe nilifurahi mno na kujua kuwa usingeiacha hiyo bahati na kwa masikitiko makubwa sana nikaja kuambiwa kuwa ' umewachomolea ' kwakuwa tu Simba SC wanakuhitaji na Wewe umekubali kabisa kuingia ' Mtegoni ' na unaelekea Kusaini nao.
Ibra Mdogo wako kutoka Ilala Bungoni najua kuwa umeangalia Pesa na Maisha mazuri ya hapa Jijin Dar es Salaam hasa ukizingatia kuwa unapenda sana Starehe ila ipo Siku utakuja Kunikumbuka Mimi Kaka yako GENTAMYCINE na naamini hata Rafiki yako mkubwa SaluRaka ambaye sasa yupo nchini Ujerumani ( baada ya Kujilipua / Kuchukua Uraia wa huko kama Mkimbizi ) nae akisikia kuwa umekataa kwenda TP Mazembe atakushangaa achilia mbali Kaka yake Hemed wa TRA ambaye ndiyo Mshauri wako Mkuu najua nae pia atakuwa amesikitika mno tu.
Hivi Ibra ungevumilia tu uende zako TP Mazembe ukapikwe na ukatengenezwe hata kwa miaka yako miwili na ukomae vyema unataka kuniambia na Wewe Vilabu vikubwa vya Ulaya visingekuona na Kukusajili? Ibra ni mara ngapi Mwenzako Mbwana Samatta amekuwa akikuambia Wewe na Rafiki yako Mkude kuwa mnachelewa hapa Tanzania na kwamba nyie ni wa Ulaya tu? Hivi hamuoni Mafanikio yake huko KRC Genk?
Najua mida ya baadae tunaweza Kukutana maeneo ya Morocco Hotel katika Duka za Mke wa Mchezaji mwenzako wa Yanga Beki Gadiel Michael ambako huwa unapenda kuwa hapo ukiwa na Wachezaji wenzako bila Kumsahau Beki Mtukutu na Kaka yako Kelvin Yondan ila nimelazimika Kuja na hii ' Kitu ' hapa ili kuwa ' Funzo ' kwa Wachezaji wengine kuwa achaneni na mawazo ' Finyu ' kuwa Maendeleo ya Mchezaji basi ni lazima tu achezee Klabu za Simba na Yanga wakati kumbe ukweli siyo huo.
Nina uhakika kuwa kwa hili Bandiko langu kuna wana Simba SC Wenzangu watanikasirikia kama siyo kuninunia kwakuwa sijapendelea Ibra kuja Simba SC yetu ila ' Kiufundi ' kabisa na ninavyomjua Ibrahim Ajibu alivyo na Kocha wetu wa Simba SC hatoweza kupata Nafasi ya Kudumu Kikosini na atasubiri mno kwa akina Chama, Niyonzima, Muzamiri na hata Ndemla ila kwa Maendeleo yake ya Kimpira angeenda Azam FC angepata Namba tena ya Kudumu ila angeenda huko TP Mazembe au hata Ulaya angefanya vyema zaidi.
Nimefurahi tu Kusikia kwamba Simba SC inamrudisha Beki wetu wa Vijana William Lucien ' Gallas ' ili aje acheze Namba yake ya Kiasili Beki Namba Mbili kwani si uwongo sikufurahishwa na Usajili wa Beki wa ' hovyo hovyo ' ambaye Kiwango chake Kimeshuka kama si Kupotea ghafla Zana Coulibaly na nasikia kuwa anaachwa rasmi ili Nafasi hiyo ya Beki Namba Mbili ibaki tu kwa Nicolas Gyan, William Lucien na Majeruhi Shomary Kapombe.
Mdogo wangu Ibrahim Ajib umeniangusha sana Kaka yako Mimi GENTAMYCINE ila nayaheshimu pia Maamuzi yako.
Nawasilisha.