Mdogo wa mke wangu (binti) amenidharau na kunitukana mbele ya mke wangu

Nimekataa

JF-Expert Member
Dec 2, 2018
285
585
Wakuu naomba ushauri.

Mimi ni mkazi wa Morogoro ninaishi kwenye nyumba yangu niliyotafuta pamoja na mke wangu. Baada ya wahitimu kumaliza chuo mwaka huu mke wangu aliniomba mdogo wake aje kuishi nasi pamoja.

Sasa baada ya kipindi kupita mke wangu ameonesha ukaribu sana na mdogo wake ikafika mpaka kumueleza mengi juu ya maisha yetu ndani.

Kisa
Jana nilienda dukan kwetu na mke wangu (duka la vipodozi), lengo kumfuata shemeji na kupiga hesabu na kufunga duka. Dakika chache mke wangu alipokea simu kutoka kwa baba yake mazazi akimuomba aje aishi nyumbani kwangu.

Walikubaliana wao yeye na baba yake mzazi akiwa na mdogo wake na hata akaamua kumtumia nauli bila ya mimi kuhusishwa chochote. Ikumbukwe yote haya yanafanyika dukani tukiwa wote watatu namaanisha mimi, mke wangu na shemeji. Baada ya hili zoezi kuisha ndipo mke wangu ananieleza kuwa "Baba atakuja kesho na nimeshamtumia na nauli"

Mi nikamjibu kwa njia ya ujumbe wa simu, "Unaniambia ama unanipa taarifa?" Baada ya hii kauli alinuna na kukasirika sana na kuamua kuongea Kikurya yeye na mdogo wake (mimi mchaga). Mimi hapo sielewi kitu ila nyuso zao ni kama wamefura kwa hasira.

Dada mtu aliamua kurudi nyumbani kwa pikipiki, mdogo mtu (shemeji) alibaki dukani na kufunga hesabu. Baada ya muda kidogo niliwasha gari na kuelekea nyumbani. Nilipofika nyumbani sasa nikamuuliza mke wangu kwanini umekasirika kwa ujumbe kama ule angali sijaandika tusi?

Ailinijibu we niache kwanza, ushamzika baba yako hivyo huna cha kupoteza. Mimi nikamwambia taswira kama hiyo unanijengea picha mbaya kwa mdogo wako, maana yanayoongeleka ni mengi sana hasa juu ya mimi na wewe.

Maana unayomueleza nduguyo huwaeleza hata watu wa karibu. Dah, baada ya kusema hivyo akampigia simu mdogo wake na kumwambia shemeji yako anasema wewe huwa una muongelea vibaya hapo dukani kwa watu wake wakaribu.

Alifunga duka na akarudi nyumbani spidi ya jeti na kunikuta sebulen nimekaa naperuzi JF. Kwanza alipofika tuu nyumbani aligonga mlango kwa nguvu sana kana kwamba kuna mtu ana tuvamia. Alipotimba sebulen akaanza kwa kusema ilikuwaje mkanizungumzia mimi na hao marafiki (majirani wa dukani) zako?

"Halafu shemeji unajua wewe ni mnafiki sana? Unadhani matendo yako kwa dada siyaoni humu ndani? Ujue shemeji wewe una roho mbaya sana, naishi na wewe kwa kukuvumilia sana?Nlisha kudharau sana.

He he..he! Nlibaki nashangaa sana, kwanza ni mtoto mdogo sana kwangu, ni wa mwaka 98. Mwisho akasema bhana eeh kama vipi andika talaka kwa mkeo mgawane mlivyo chuma kila mtu asepe zake (shemeji huyo)! Hata dada yake hakuwahi kutamka maneno kama haya asee.

Wakuu, mimi nimeamua asepe kwao ifikapo Jumatatu ya tarehe 17, October. Japo mke anakuwa kama anajiuliza sana haya maamuzi yangu.

Pia msaada tafadhali maana nina mawazo sana kuhusu huyu dogo mwenye Degree ya Biashara, halafu pia ndugu lakini sina namna.

Nawasilisha.
 
Mkuu hilo kabila huwa hawapendeki kwa style unayoitumia ! Ungeoa tanga au zanzibar ningekuelewa !! Hili kabila ukiwatandika vibao ndo unakua Romantic !!

Kwanza mke inaonekana ndo ana sauti ndani kuliko wewe ! Kampa mdogo wake ujasiri !! Pia anakaribishaje mgeni wakati wewe na yeye hamjaongea !
Lamba vibao wote kwanza au waondoke kwa muda !!
 
Dah nakosa hata cha kucoment, sema shida inaanzia hapa mlijenga nyumba kwa pamoja na wanajua fika huezi kuachana nae maana unahofia mtagawana mali.

My take; sioi mpaka nijikamilishe mambo yangu ya msingi nyumba, chakula, mavazi na usafiri, ili nikikutana na dhahama kama hii ning'oe toto la mtu meno, kwanza nimesahau sioi ng'oo
Marriage is a scam
 
shida za kutafuta wote from scratch hizo
Dah nakosa hata cha kucoment, sema shida inaanzia hapa mlijenga nyumba kwa pamoja na wanajua fika huezi kuachana nae maana unahofia mtagawana mali.

My take; sioi mpaka nijikamilishe mambo yangu ya msingi nyumba, chakula, mavazi na usafiri, ili nikikutana na dhahama kama hii ning'oe toto la mtu meno, kwanza nimesahau sioi ng'oo
Marriage is a scam
 
Back
Top Bottom