Mdhibiti na Mkaaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG),asipopewa meno ripoti zake kila mwaka zitakuwa ni kazi bure tu

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Sifa kubwa ya sisi watanzani(sio wote) ni kutumia muda mwingi na nguvu nyingi katika kulalamika huku tukitumia muda mchache na nguvu kidogo katika kupambana na chanzo /vyanzo vya malalamiko yetu.

Kwa mfano,leo hii kilio kikubwa cha watanzania wengi kuanzia wasomi, wanasiasa,wanaharakati,viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla,ni kupatikana kwa katiba mpya itakayokidhi mahitaji ya wakati tulionao leo.

Hata hivyo,ni bahati mbaya sana kuona tunatumia muda mwingi na nguvu nyingi kulalamikia matatizo yanayotokana na katiba hii ya sasa huku tukitumia muda kidogo,juhudi kidogo na nguvu kidogo kudai upatikana wa katiba mpya.

Kwa kasumba na tabia yetu ile ile,hivi sasa tunatumia muda mwingi na nguvu nyingi kuchambua ripoti ya CAG na kulalamikia madudu yaliyoibuliwa katika hiyo ripoti huku tukitumia muda mchache na nguvu kidogo kuhakikisha huyu CAG anapewa meno ya kisheria ya kuweza kuchukuta hatua pale inapobidi na tunasahau ripoti hizi kila mwaka huwa zinasheheni madudu chungu nzima.

Labda tujiulize,hivi sisi watanzania tunawaza sawa sawa?

Je,tunajipanga vipi kuhakikisha madudu haya hayajirudii?

Hivi mwakani ripoti ikitoka na ikawa mbaya kuliko hii ya sasa,tukiendelea kulalamika tutakuwa ni watu tunaowaza sawa sawa?

Mfano.Tumesikia wakati fulani(taarifa zisizo rasimi) kuwa bajeti ya CAG ilikuwa imeminywa na kuwa kikwazo katika utendaji wake.

Binafsi najiuliza,kama kweli Bajeti yake iliminywa,tunachukua hatua gani ili kuondoa tatizo hili?

Je,tunasubiri iminywe tena ili tuendelee kulalamika na kulaumu?

Binafsi kwa kutambua kazi nzuri ya CAG na ili kumuwesha afanye kazi zake kwa ufanisi zaidi na bila kutegemea fedha kutoka serikalini, nilishauri kupitia hapa JamiiForums kuwa sheria inayounda ofisi ya CAG ifanyiwe marekebisho na kumuwezesha CAG awe anapata fedha za kuendeshea ofisi yake moja kwa moja kwa kupitia tozo maalumu itakayotozwa kutoka kwenye baadhi ya biashara au huduma zitakazooneka zinafaa kama ilivyo kwa Ewura, REA,n.k. na si kusubiri mafungu kutoka serikali na hii ni kutokona na umuhimu wa chombo hiki kwa umma.

Vile vile namshauri CAG nae atoe mapendekezo ya aina hii kwa serikali na hata kwa kamati husika za Bunge na kwa kufanya hivyo atakuwa ametimiza wajibu wake na kunawa mikono.

Niwaambie tu bila kumpa meno ya kisheria CAG,mwaka huu tutajadili ripotI yake kwa mihemuko na mwakani yatajirudia haya haya na tena yanaweza hata kuzidi.

Albert Einsteni aliwahi sema: "insanity is doing the same thing over and over again and expecting different results."

Tujiuluze kama hii definition by Albert Einstein haituhusu.
 
Mkuu kwani hujui anaetafuna pesa kuliko wengine, Humjui ? Aaah salary slip si yule
Apewe meno ya kisheria kusimamisha watu kazi wanaopata hata chafu bila kujali aliewateua mfano kwa ofisa wa serilali ambae taasisi anayoisimamia inapata hati chafu kwa miaka miwili mfululizo au hata kutoa onyo kwa barua.

Kwa mfano sheria imgewaza kutamka kuwa mtu anapopewa barua ya onyo mara mbili au hata chafu zaidi ya mbilI basi automatically anatakiwa kuondolewa katika nafasi yake au kuchunguzwa..

Labda tujiulixe kuna logic gani kukabidhi hati chafu then mambo yanakuwa yameisha au mpaka kusubiri mamlaka yake ya uteuzi ndio iamue kuchukua hatua?
 
Apewe meno ya kisheria kusimamisha watu kazi wanaopata hata chafu bila kujali aliewateua mfano kwa ofisa wa serilali ambae taasisi anayoisimamia inapata hati chafu kwa miaka miwili mfululizo au hata kutoa onyo kwa barua.

Sasa kuna logic gani kukabidhi hati chafu then mambo yanakuwa yameisha au mpaka kusubiri mamlaka yake ya uteuzi ndio iamue kuchukua hatua.
Lengo la Public Risk Management hata CAG mwenyewe haelewi lengo la Public risk management

Kwanza CAG wetu kuna mambo anafanya vizuri hasa kwenye kureview Risk assessment process na kugundua mapungufu na pia kwenye kuangalia vyanzo hatarishi yaani identification anajitahidi sana sana ingawa Mimi sio Auditor Au accounting officer

Nini afanye CAG na sio yeye peke yake haya mambo ni jumuishi au kule kwetu ulaya wanasema ni Intergrated yanahusisha kuanzia PS yaani Katibu wa hazina huyu permanent treasury yeye ndie muhusika namba moja

Namba mbili ni hizi council boards za halmashauri au regional secretariat plus accounting officers hawa wote ilibidi wasaidie mambo yasiharibike

Mkuu hii inshu nitaeleza nipo safarini, nitatoa ushauri nini kifanyike kupunguza haya maulaji
 
Apewe meno ya kisheria kusimamisha watu kazi wanaopata hata chafu bila kujali aliewateua mfano kwa ofisa wa serilali ambae taasisi anayoisimamia inapata hati chafu kwa miaka miwili mfululizo au hata kutoa onyo kwa barua.
Mkuu huna hata basics za accounts na book keeping,unaongelea kwenye mtizamo wa kisiasa tu na kulia lia kwingi
Audit query sio lazima izue diciplinary action
Inawezekana ikawa ni umbumbumbu wa wahasibu au ni kweli watu wamepiga kama Mbowe alivyoiba B2 za chadema.
Ndio maana Utou ameshauri audit query ijibiwe kwa nyaraka,halafu CAG akiridhika anatoa statement ya kuridhika,akikataa ndipo diciplinary action inaweza kuwa considered
 
Mkuu huna hata basics za accounts na book keeping,unaongelea kwenye mtizamo wa kisiasa tu na kulia lia kwingi
Audit query sio lazima izue diciplinary action
Inawezekana ikawa ni umbumbumbu wa wahasibu au ni kweli watu wamepiga kama Mbowe alivyoiba B2 za chadema.
Ndio maana Utou ameshauri audit query ijibiwe kwa nyaraka,halafu CAG akiridhika anatoa statement ya kuridhika,akikataa ndipo diciplinary action inaweza kuwa considered
Mbona tumeona Magu kasimamisha wakurugenzi kwa kupata hati chafu na mkashangilia na kusifu?Acha kuwa mnafiki!
 
ukimpa kazi ya yakuhukumu na kutoa adhabu itakubidi utafute chombo kingine cha kuibua madudu pekee.CAG ameshaibuia madudu ni kazi ya Serikali kuyashughulikia madudu..yakiwemo yale yaliyoubuliwa ndani ya Chadema
 
ukimpa kazi ya yakuhukumu na kutoa adhabu itakubidi utafute chombo kingine cha kuibua madudu pekee.CAG ameshaibuia madudu ni kazi ya Serikali kuyashughulikia madudu..yakiwemo yale yaliyoubuliwa ndani ya Chadema
Una mimba ya Chadema
 
ukimpa kazi ya yakuhukumu na kutoa adhabu itakubidi utafute chombo kingine cha kuibua madudu pekee.CAG ameshaibuia madudu ni kazi ya Serikali kuyashughulikia madudu..yakiwemo yale yaliyoubuliwa ndani ya Chadema
Kwahiyo tuwe tunasubiri mpaka Raisi aamue kuchukua hatua na asipoamua basi hatuna la kufanya.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Anachohitaji CAG ni full access ya kule kunakohitaji kukaguliwa kwa maslahi ya nchi na jambo lingine la msingi ulilosema la bajeti ambayo sio tegemezi!

Suala la "meno" lipo kwenye taasisi zingine...

Leo hii kwa mfano; kinacho-trend ni suala la CAG na ukaguzi wa migodi. Kimsingi hapa ni CAG kukosa access ya kukagua migodi.

Hoja kwamba hii ni migodi binafsi ni hoja isiyo na msingi kwa sababu kutokana na sheria zetu, kampuni za madini huwa hazilipi baadhi ya kodi hadi zirudishe baadhi ya gharama za uwekezaji!

Sasa tutafahamu vipi ikiwa wanachorekodi kwenye vitabu vyao ni sahihi kama CAG hana access ya kuwakagua?!

Matokeo yake ndo haya, ni kawaida kwao kutangaza wamepata hasara.

Tukija suala la meno; sheria ipo wazi!

CAG anakagua na baada ya hapo anaingia TAKUKURU na Director of Criminal Investigation... DCI.

Endapo alichokiona CAG kina harufu ya rushwa, hapo alitakiwa TAKUKURU anaingia moja kwa moja! Aidha, kama alichokiona CAG kina harufu ya wizi; hapo hapo DCI anatakiwa kuingia!

Tatizo la kwanza: Je, kuna coordinated efforts kati ya CAG kwa upande mmoja na TAKUKURU kwa upande mwingine au hadi wasikie rais anatangaza fulani akamatwe!!

That's one but two, je kuna clear framework kati ya hizi taasisi 3?!

Kwamba, pindi CAG anapopata findings zake; hapo hapo anatengeneza ripoti mbili za ziada... moja kwa DCI kwa zile findings zenye harufu ya wizi na ya pili kwa TAKUKURU kwa zile findings zenye harufu ya rushwa/ufisadi!

By default, DCI na TAKUKURU walitakiwa moja kwa moja kupokea kijiti cha CAG!

Lakini kwa upande mwingine; jambo lingine la kuangalia hapo ni autonomy aliyonayo DCI na TAKUKURU kwenye kupokea kijiti cha CAG!

Kwamba, baada ukaguzi; CAG amegundua matumizi yanayoashiria ubadhirifu pale Magogoni!

Je, hapo TAKUKURU atakuwa na nguvu ya kuingia Ikulu kuchunguza kiini cha ubadhirifu ulioripotiwa na CAG?!

Kwamba, uchunguzi wa CAG umegundua harufu ya wizi Mambo ya Ndani; sasa je; DCI atakuwa na ubavu wa kwenda kutafuta umbeya kwenye ofisi ya bosi wake?!

To sum up; ni kwa kiasi gani DCI na Mkurugenzi wa TAKUKURU wanalindwa na sheria kama ambavyo analindwa CAG!

Pili; ni kwa kiasi gani DCI na TAKUKURU wanawajibika automatically na findings za CAG!

Huo ni upande mmoja lakini pia kuna TRA. Sina hakika ikiwa hawa nao wana-act pasipo na shuruti linapokuja suala la ripoti ya CAG.

Kwa mfano, ukisoma Ripoti ya CAG ya hivi sasa; kuna mahali alipoonesha ukwepaji kodi wa takribani Sh. 15 Billion ambazo ni msamaha wa mafuta yaliyopaswa kutumika kwenye migodi!

Ajabu ni kwamba, according to CAG, mafuta hayakutumika migodini!

Kimsingi; hapo kuna harufu ya ukwepaji wa wazi wa kodi ambao mamlaka husika; yaani TRA walitakiwa kuanzia hapo kuchukua zaidi ya 15 billion yetu!

Mfano kama huo, according to CAG, upo pia kwa bidhaa zinazosafirishwa kwenda nje; yaani goods on transit!

So, kwavile haiwezekani CAG afanye ukaguzi halafu hapo hapo afanye kazi za kipolisi na kimahakama; muhimu ni kuwa na coordinated efforts kati ya CAG kwa upande mmoja na DCI + TRA na TAKUKURU kwa upande mwingine.

Hawa wanastahili sio tu kupewa meno bali ulinzi wa kikatiba utakaowawezesha kupokea kijiti cha CAG bila ya uoga!

Aidha, iwe wazi kwamba kumalizika kwa kazi ya CAG kuwe ni dakika 45 za mchezo (by law), na dakika 45 zingine zinamaliziwa na DCI + TAKUKURU + TRA.
 
Anachohitaji CAG ni full access na bajeti isiyoyumba...

Suala la "meno" lipo kwenye taasisi zingine...

Nitafafanua
Hizo taasisi zingine ziko chini ya mtu mmoja ambae ndio anaonekana ndio mtoa maagizo.Tunataka CAG awe walau na madaraka fulani maana yeye hata kufukuzwa si rahisi.Hao wengine hawana ubavu.
 
Mbona tumeona Magu kasimamisha wakurugenzi kwa kupata hati chafu na mkashangilia na kusifu?Acha kuwa mnafiki!
Haaahaaaa umenifurahisha maana umemjibu vizuri na unafki wake..... Yaani kabombe anashauri kwa CAG akitoa ripoti mpaka nyaraka zijibiwe na wahusika ndio hatua zichukuliwe ila kwa magufuli hapana yeye akipewa ripoti tu atumbue alafu wapige vigeregere ???
 
Hizo taasisi zingine ziko chini ya mtu mmoja ambae ndio anaonekana ndio mtoa maagizo.Tunataka CAG awe walau na madaraka fulani maana yeye hata kufukuzwa si rahisi.Hao wengine hawana ubavu.
Nimefafanua yote hayo, including suala la autonomy na ulinzi wa kisheria na nafasi ya kila mmoja
 
Sifa kubwa ya sisi watanzani(sio wote) ni kutumia muda mwingi na nguvu nyingi katika kulalamika huku tukitumia muda mchache na nguvu kidogo katika kupambana na chanzo /vyanzo vya malalamiko yetu.

Kwa mfano,leo hii kilio kikubwa cha watanzania wengi kuanzia wasomi, wanasiasa,wanaharakati,viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla,ni kupatikana kwa katiba mpya itakayokidhi mahitaji ya wakati tulionao leo.

Hata hivyo,ni bahati mbaya sana kuona tunatumia muda mwingi na nguvu nyingi kulalamikia matatizo yanayotokana na katiba hii ya sasa huku tukitumia muda kidogo,juhudi kidogo na nguvu kidogo kudai upatikana wa katiba mpya.

Kwa kasumba na tabia yetu ile ile,hivi sasa tunatumia muda mwingi na nguvu nyingi kuchambua ripoti ya CAG na kulalamikia madudu yaliyoibuliwa katika hiyo ripoti huku tukitumia muda mchache na nguvu kidogo kuhakikisha huyu CAG anapewa meno ya kisheria ya kuweza kuchukuta hatua pale inapobidi na tunasahau ripoti hizi kila mwaka huwa zinasheheni madudu chungu nzima.

Labda tujiulize,hivi sisi watanzania tunawaza sawa sawa?

Je,tunajipanga vipi kuhakikisha madudu haya hayajirudii?

Hivi mwakani ripoti ikitoka na ikawa mbaya kuliko hii ya sasa,tukiendelea kulalamika tutakuwa ni watu tunaowaza sawa sawa?

Mfano.Tumesikia wakati fulani(taarifa zisizo rasimi) kuwa bajeti ya CAG ilikuwa imeminywa na kuwa kikwazo katika utendaji wake.

Binafsi najiuliza,kama kweli Bajeti yake iliminywa,tunachukua hatua gani ili kuondoa tatizo hili?

Je,tunasubiri iminywe tena ili tuendelee kulalamika na kulaumu?

Binafsi kwa kutambua kazi nzuri ya CAG na ili kumuwesha afanye kazi zake kwa ufanisi zaidi na bila kutegemea fedha kutoka serikalini, nilishauri kupitia hapa JamiiForums kuwa sheria inayounda ofisi ya CAG ifanyiwe marekebisho na kumuwezesha CAG awe anapata fedha za kuendeshea ofisi yake moja kwa moja kwa kupitia tozo maalumu itakayotozwa kutoka kwenye baadhi ya biashara au huduma zitakazooneka zinafaa kama ilivyo kwa Ewura, REA,n.k. na si kusubiri mafungu kutoka serikali na hii ni kutokona na umuhimu wa chombo hiki kwa umma.

Vile vile namshauri CAG nae atoe mapendekezo ya aina hii kwa serikali na hata kwa kamati husika za Bunge na kwa kufanya hivyo atakuwa ametimiza wajibu wake na kunawa mikono.

Niwaambie tu bila kumpa meno ya kisheria CAG,mwaka huu tutajadili ripotI yake kwa mihemuko na mwakani yatajirudia haya haya na tena yanaweza hata kuzidi.

Albert Einsteni aliwahi sema: "insanity is doing the same thing over and over again and expecting different results."

Tujiuluze kama hii definition by Albert Einstein haituhusu.
CC: pascal Mayala
 
Back
Top Bottom