BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 421
- 1,048
Wadau salama, leo nimekutana na hili andiko, tusome mtazamo wa mwenzrtu kuhusu kile wanachojadili wabunge...
WANAYOJADILI WABUNGE KWENYE GROUP LAO LEO KUTWA NZIMA
Na Thadei Ole Mushi
Wabunge wa CCM leo kwenye Group lao la kibunge wamejadili na kukusudia kupeleka hoja bungeni wapewe privilege ya magari yao kuwa na Special number.
Sababu kubwa ya kutaka hilo ni kuwa wanasema matrafiki wanawasumbua sana njiani na hawataki usumbufu huo. Kuna mambo kadhaa nayaona hapa:-
1. Tayari wameshajiona kuwa hao ni Raia Special nchini.Yaani wanajiondoa kwenye kuwa mwananchi wa kawaida kuwa VVIP. Wanataka kujitofautisha na wananchi wa kawaida.
2. Trafiki hawezi kukusimamisha kama huna makosa, tafsiri ya maombi haya ni kutaka kuhalalisha kufanya makosa.
3. Kila kundi likiomba Special number hapo barabarani kutakuwa ni vurugu tupu.
4. Nafikiri badala ya kujiombea wao Special number wangetuombea Sisi waalimu na Madaktari ambao huwa wanawahi shughuli nyeti za kijamii. Hebu fikiria Daktari anayemuwahi Mgonjwa asife anasimamishwa halafu mbunge anayekwenda kwa Mchepuko wake hasimamishwi.
5. Wabunge kwenye group siku nzima wanajadili kupewa Plate number Special wanaacha kubangua bongo wanaishauri vipi Serikali kutatua tatizo la mafuta ya kula na ya Petrol nchini ambayo yamepandisha vya kutosha maisha ya wananchi.
Wana Privilege nyingi sana hasa maslahi yao lakini hawajaridhika wanajipigania binafsi kuliko kuwapigania wananchi. Hivi ndivyo wanavyolamba Asali ambayo ni kodi yangu mimi na wewe.
1. Mbunge hulipwa mshahara kwenye scale ya LSS (P) 2 ambayo mshahara wake ni Shilingi 4,600,000.
2. Atalipwa posho ambazo kwa Mwezi hufikia Shilingi 8,292,000 katika mchang'anuo ufuatao.
✓Atalipwa posho Kwa ajili ya mafuta ya gari yake Shilingi 3,750,000.
✓Atalipwa Posho Kwa ajili ya Matengenezo ya Gari yake Shilingi 1,500,000.
✓Atalipwa Posho inayoitwa (Posho ya Mbunge na matumizi mengine jimboni) Shilingi 1,000,000.
✓ Atalipwa Posho ya kujikimu ya siku 10 kama atajisikia kwenda Jimboni Shilingi 450,000.
✓ Atalipwa Posho ya kujikimu kwa Wasaidizi wake watatu Kwa siku kumi atakazokuwa jimboni Shilingi 900,000 hapa kama atajisikia kwenda Jimboni au kwa mchepuko Dar 😂
✓ Atalipwa Posho ya watumishi watatu kama atajisikia kuajiri (Mhudumu wa Ofisi yake, Katibu wake, na Dereva) katika mchang'anuo ufuatao.
3.Katibu wake Shilingi 352,000 Mhudumu 170,000, Dereva 170,000. Jumla Shilingi 692,000. Hapa ni kama atajisikia kuajiri sio lazima.
Jumla ya Fedha zote zinafika Shilingi 12,892,000.Fedha hizi zote zinaingia kwenye account yake Mbunge.
Hii ni nje ya Posho za vikao vya Bunge.
2. Katika vikao vya budget mathalani Mbunge hulipwa Shilingi 240,000 kama sitting allowance, Shilingi 120,000 kama posho ya kujikimu kwa hiyo kwa siku ni Shilingi 360,000.
Bunge la budget pamoja na vikao vya Kamati kwa kalenda ya Bunge la budget la 2021/2020 lilianza na vikao vya Kamati Tarehe 6 march na kuendelea na Bunge lenyewe lililoisha June 30. Jumla ya siku zote ukitoa Jumapili ni siku 97 hizi siku ukizidisha mara 360,000 anazopata kwa siku unapata jumla ya Shilingi 34,920,000. Hii ni Fedha ya Bunge la budget tu. Hapa sijajumlisha na posho za Vikao vya bunge la mwezi wa 11.
Sifa kubwa ya kuwa Mbunge ni kujua kusoma na Kuandika. Nisaidie ku share kila mwananchi aone anachojadili mbunge wake leo.
Ole Mushi
0712702602.
***************
WANAYOJADILI WABUNGE KWENYE GROUP LAO LEO KUTWA NZIMA
Na Thadei Ole Mushi
Wabunge wa CCM leo kwenye Group lao la kibunge wamejadili na kukusudia kupeleka hoja bungeni wapewe privilege ya magari yao kuwa na Special number.
Sababu kubwa ya kutaka hilo ni kuwa wanasema matrafiki wanawasumbua sana njiani na hawataki usumbufu huo. Kuna mambo kadhaa nayaona hapa:-
1. Tayari wameshajiona kuwa hao ni Raia Special nchini.Yaani wanajiondoa kwenye kuwa mwananchi wa kawaida kuwa VVIP. Wanataka kujitofautisha na wananchi wa kawaida.
2. Trafiki hawezi kukusimamisha kama huna makosa, tafsiri ya maombi haya ni kutaka kuhalalisha kufanya makosa.
3. Kila kundi likiomba Special number hapo barabarani kutakuwa ni vurugu tupu.
4. Nafikiri badala ya kujiombea wao Special number wangetuombea Sisi waalimu na Madaktari ambao huwa wanawahi shughuli nyeti za kijamii. Hebu fikiria Daktari anayemuwahi Mgonjwa asife anasimamishwa halafu mbunge anayekwenda kwa Mchepuko wake hasimamishwi.
5. Wabunge kwenye group siku nzima wanajadili kupewa Plate number Special wanaacha kubangua bongo wanaishauri vipi Serikali kutatua tatizo la mafuta ya kula na ya Petrol nchini ambayo yamepandisha vya kutosha maisha ya wananchi.
Wana Privilege nyingi sana hasa maslahi yao lakini hawajaridhika wanajipigania binafsi kuliko kuwapigania wananchi. Hivi ndivyo wanavyolamba Asali ambayo ni kodi yangu mimi na wewe.
1. Mbunge hulipwa mshahara kwenye scale ya LSS (P) 2 ambayo mshahara wake ni Shilingi 4,600,000.
2. Atalipwa posho ambazo kwa Mwezi hufikia Shilingi 8,292,000 katika mchang'anuo ufuatao.
✓Atalipwa posho Kwa ajili ya mafuta ya gari yake Shilingi 3,750,000.
✓Atalipwa Posho Kwa ajili ya Matengenezo ya Gari yake Shilingi 1,500,000.
✓Atalipwa Posho inayoitwa (Posho ya Mbunge na matumizi mengine jimboni) Shilingi 1,000,000.
✓ Atalipwa Posho ya kujikimu ya siku 10 kama atajisikia kwenda Jimboni Shilingi 450,000.
✓ Atalipwa Posho ya kujikimu kwa Wasaidizi wake watatu Kwa siku kumi atakazokuwa jimboni Shilingi 900,000 hapa kama atajisikia kwenda Jimboni au kwa mchepuko Dar 😂
✓ Atalipwa Posho ya watumishi watatu kama atajisikia kuajiri (Mhudumu wa Ofisi yake, Katibu wake, na Dereva) katika mchang'anuo ufuatao.
3.Katibu wake Shilingi 352,000 Mhudumu 170,000, Dereva 170,000. Jumla Shilingi 692,000. Hapa ni kama atajisikia kuajiri sio lazima.
Jumla ya Fedha zote zinafika Shilingi 12,892,000.Fedha hizi zote zinaingia kwenye account yake Mbunge.
Hii ni nje ya Posho za vikao vya Bunge.
2. Katika vikao vya budget mathalani Mbunge hulipwa Shilingi 240,000 kama sitting allowance, Shilingi 120,000 kama posho ya kujikimu kwa hiyo kwa siku ni Shilingi 360,000.
Bunge la budget pamoja na vikao vya Kamati kwa kalenda ya Bunge la budget la 2021/2020 lilianza na vikao vya Kamati Tarehe 6 march na kuendelea na Bunge lenyewe lililoisha June 30. Jumla ya siku zote ukitoa Jumapili ni siku 97 hizi siku ukizidisha mara 360,000 anazopata kwa siku unapata jumla ya Shilingi 34,920,000. Hii ni Fedha ya Bunge la budget tu. Hapa sijajumlisha na posho za Vikao vya bunge la mwezi wa 11.
Sifa kubwa ya kuwa Mbunge ni kujua kusoma na Kuandika. Nisaidie ku share kila mwananchi aone anachojadili mbunge wake leo.
Ole Mushi
0712702602.
*************************