Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna alichokikimbia hiko vinginevyo asingerudi na kuhangaikia kutafuta nafasi za uwakishi wa vitogoji jumuiya ya wazazi.
Kuna alichokikimbia hiko vinginevyo asingerudi na kuhangaikia kutafuta nafasi za uwakishi wa vitogoji jumuiya ya wazazi.
Yaani yeye ndo kafanya hayo afu mnavilaumu vyombo vya habari! JE WALIMKAMATA WAKAMLETEA HAO MABINTI WAKAMUWEKEA BASTOLA KICHWANI KISHA WKAMLAZIMISHA ATABASAMU WAKAMPIGA PICHA!!???????, AU HIZO PICHA ZAKE WAMEZIPATAJE????
Ngoja aje hapa na alivyo bingwa wa kulipuka sijui itakuaje. Lakini me nashangaa namna RiziOne anavyo mshinda akili. RiziOne anawekeza though kwa magumashi. Huyu jibaba anauza sura.
Ngoja aje hapa na alivyo bingwa wa kulipuka sijui itakuaje. Lakini me nashangaa namna RiziOne anavyo mshinda akili. RiziOne anawekeza though kwa magumashi. Huyu jibaba anauza sura.
Mwenye elimu ya meli ndiyo huyu...
Plus degree mbiliMwenye elimu ya meli ndiyo huyu...
WIVU unakusumbua
Na Sifael Paul
WILLIAM Malecela a.k.a Le Mutuz ambaye anatajwa kuwa ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe Bongo, John Malecela ambaye anadaiwa kuwa ni funga kazi kwa kupenda kupiga picha na wanawake wazuri kila anapokuwa, Amani limemfuatilia hatua kwa hatua na sasa linafunguka.
Kwa mujibu wa mapicha yake mazuri yaliyopo mitandaoni, asilimia 90 zinamuonesha Le Mutuz akiwa na wanawake wazuri wa kada mbalimbali.
WAMO MASTAA
Mbali na wanasiasa wenzake, Le Mutuz aliyegombea ubunge wa Afrika Mashariki kwa leseni ya CCM hivi karibuni lakini kura hazikutosha, anaonekana kwenye picha nyingi zisizo na idadi akiwa na mastaa mbalimbali wakiwemo waigizaji na wanamuziki wenye majina makubwa Bongo.
NI KILA MAHALI?
Katika picha hizo, Le Mutuz anaonekana akiwa sehemu mbalimbali hasa kwenye kumbi za starehe, baa, migahawani, viwanjani, nyumbani na ufukweni, vyote jijini Dar es Salaam.
ETI NI MAMBO YA KUTOKLEZEA
Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa Le Mutuz, jamaa huyo mwenye sivii ya kuishi nchini Marekani kwa muda mrefu amekuwa akiwakaribisha warembo hao kwenye mtandao wake (jina tunalo) kwa kutundika picha hizo na kuwataka waingie humo kujiona walivyotoklezea.
BAADHI YA MASTAA NI HAWA
Baadhi ya mastaa wanaoonekana na mutu mukubwa huyo na kusababisha minongono kwa kuwa zina mapozi tata ni pamoja na Wema Isaac Sepetu, Jacqueline Wolper Masawe, Jokate Mwegelo, Miss Tanzania 2011, Salha Israel, Judith Wambura Mbibo Lady Jaydee na warembo wengine kibwena wasiokuwa na majina.
WAMO MARAFIKI WA FACEBOOK
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, inaelezwa kuwa, Le Mutuz huwa anawasiliana na warembo ambao ni marafiki zake katika mtandao wa kijamii wa Facebook ambapo hukutana nao na kupiga picha ili kuziweka mtandaoni kwake.
MSHANGAO!
Kwa mujibu wa maoni ya watu wanaotembelea mtandao wake wanashangazwa na ishu hiyo huku wakihoji mbona anafanya na mademu tu, tena wazuri?
LENGO NI NINI?
Ili kupata undani wa kwa nini Le Mutuz anafanya hivyo, Amani lilifanya jitihada za kupata kupitia kilongalonga chake cha kiganjani lakini hakupatika, hata hivyo jitihada za kumpata zinaendelea.
Wadau wengi hapa JF tunamfahamu kutosha William Malecela kwa michango mizuri na kuleta mada za udadisi katika kujenga jamii yetu. Ni mdau mwenzetu na ni mmja kati ya wadau wa mwanzoni kabisa waliojitahidi kuchangia mada mbalimbali hapa Jamii forums.
Uvumilivu wake katika kujadili mada pamoja na kuonyesha ustahimilivu hata tunapomkosoa au kuwa kinyume cha itikadi anazoamini ambayo ni haki yake ya free speach ni funzo tosha wangu na kwa wengi.
Kilichonishtua ni Gazeti moja hilo pichani kuweka habari ambazo sidhani kama yeye binafsi zitamfurahisha pamoja na familia yake. Kwa walio karibu naye wajaribu kumpa moyo na subira kwani maisha ni safari na binadamu ni kinyonga, kwani akiwa na sikio sikivu ipo siku magazeti haya haya yataandika mazuri tu juu yake.
Tukumbuke ameshapata nafasi kadhaa katika Chama cha Mapinduzi kuwa mwakilishi na vyeo vingine na bado anatarajia kupanda taratibu, mambo kama haya nisingefurahia kutokea kwake kwani yanaweza kuwa kihuzi katika kupanda hatua nyingine zaidi kufikia matarajio yake. Papo kulinda heshima ya jna la Malecela John.
dah nimeipenda pic yakoNisingekua natumia phone ningekugongea like ya hatariii mkuu
Yaaani hili jamaa bana sasa linamrembulia nani macho
we agent wake nini? yeye mwenyewe anafurahia, angalia post zake za nyuma akijisifia kupiga picha na warembo na kula maisha.