Mdahalo wa Twaweza kuhusu Utafiti unaohusu Vipaumbele, Utendaji na Siasa nchini Tanzania

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138


Jiunge nasi kufuatilia kinachoendelea kwenye Mdahalo kuhusu matokeo ya utafiti wa Twaweza > Utafiti wa TWAWEZA: Rushwa imepungua lakini hali ya maisha imezidi kuwa ngumu ambao unazinduliwa LIVE kutoka hapa Makumbusho ya Taifa (Posta, Mkabala na Chuo cha IFM).

Je, wananchi wana maoni gani kuhusu vipaumbele vya Serikali, utendaji wake na siasa nchini?

Wazungumzaji waalikwa ni wanasiasa mashuhuri nchini ambao ni;

1. Nderakindo Keesy - NCCR
2. Zitto Kabwe - ACT
3. Tundu Lissu - CHADEMA
4. Humphrey Polepole - CCM

Ungana nasi mpaka mwisho.

--------------

H. Polepole(CCM): Kiwango cha kukubalika kwa Rais Magufuli(71%) ni juu ya wastani wa kukubalika kwa marais wengine Afrika

Dr. Nderakindo Kessy(NCCR): Mfumo wa uongozi uliowekwa na wananchi(Katiba) ni muhimu zaidi kwani kiongozi atafanya anachotakiwa kufanya

Dr. Nderakindo Kessy: Wananchi wanaposema rushwa si tatizo wanazungumzia rushwa ndogondogo, rushwa kubwa za kitaifa bado zipo

Dr. Nderakindo: Umaarufu wa vyama vya siasa umeshuka sababu vyama vimefungwa midomo, umaarufu wa vyama ni kupiga domo

H. Polepole: Katiba haitakiwi kuwa hoja ya Vyama vya Siasa kujipatia umaarufu - Katiba ni suala la wananchi

Polepole: Huwezi kuzungumza Katiba ukiwa na mikono michafu - CCM tunasafisha mikono yetu kabla ya kuzungumzia Katiba

Polepole: Wenye mikono michafu wengi wako Upinzani kwa sasa, hata suala la Madini ni wao wanapinga

Polepole: Wapinzani kulalamika kufungwa midomo sio kweli, wana ruhusa ya kuandamana kwenye majimbo yao lakini hawafanyi hivyo

Dr. Kessy(NCCR): Hakuna chama kinachoitwa upinzani; si sawa kusema kila linalofanywa na chama kimoja kimefanywa na 'Upinzani'

Ado Shaibu(ACT): Ni taratibu za wapi zinazosema kuwa chama ni sharti kinawe mikono ndipo Katiba ishughulikiwe?
 
Tundu Lissu haoni aibu Kutembea na kuonekana mbele za Watu? Kwanini asingesubiri hali ya hewa aliyoichafua iondoke kwanza!

Cheki Mzungu alivyokua mdogo!
IMG_20170614_203054_048.JPG
 
Tukubali Tafiti Pale atakaposema CHADEMA imeshuka umaarufu

63% of the citizens feel closer to @ccm_tanzania than to any other party. [HASHTAG]#SautiZaWananchi[/HASHTAG].
 
hhizi tafiti za kuipa kiki sisiem na kuwapa wahojiwa simu haikubaliki katika maadili ya tafiti
 
Mjadala mpana inatakiwa,Twaweza wanatwambia kule watoto wetu wanakosoma,elimu wanayopata hairidhishi ,pia wanasema hata mahospitalini tunakotibiwa hali ni mbaya na pia hata hali ya upatikanaji wa maji ni tete

Nini kimeshusha wakati awamu ya nne, juzi tu,haya mambo yalikuwa na afadhali?

IMG_20170615_125815.png
 
Tundu Lissu haoni aibu Kutembea na kuonekana mbele za Watu? Kwanini asingesubiri hali ya hewa aliyoichafua iondoke kwanza!

Cheki Mzungu alivyokua mdogo!
View attachment 524346
naona mzungu anacheka kicheko cha kinafiki hapo baada ya kumsikia mwenyeji wake akiitikia YES mahali alipotakiwa kusema NO.

wazungu wakikupatia noma!!
 
Back
Top Bottom