Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Ninawaomba wana CCM mnaoweka maslahi ya nchi mbele ya Chama mumuulize Mpendwa wetu mgombea wa CCM maswali haya kwa niaba yangu na ya wanachi wengine ili akanushe uvumi unaoenezwa juu yake katika haya yafuatayo.
Maswali ya muhimu.
1. Wapinzani wako wamekuwa wakisema kuwa wewe sio makini na kwa sababu hiyo unaweza kujikuta umesaini jambo hatari kwa taifa. Je kuna ukweli juu ya matukio haya? Kama wewe ni makini na watendaji wako sio makini basi kwa matukio yafuatayo tunaomba utuambie ulichukua hatua gani kuonyesha umakini wako?
a) Ulisaini sheria ya uchaguzi kwa mbwembwe bila ya kuisoma huku ikiwa imechakachuliwa.
b) Ulipokea cheki yenye tarakimu tofauti na maneno kwa shukrani na kukubali kupigwa picha huku ukiionyesha.
C.) Uliwahi kumwita mkurugenzi wa wilaya moja kuja kuchukua gari na alipofika ulikasirika na kushangaa anawezaje kuchukua gari la mkurugenzi mwingine?
d) Ulishangilia kwa makofi riport iliyokuwa ikisomwa mbele yako kuwa shs Bilioni 3 zilitumika kwa matundu ya vyoo vya shule nne kwa matundu manne kila shule kwa gharama ya shs Milioni 700 kwa jumla ya shs Bilioni zaidi ya 3.
e) Uliwainua mikono na kuwaita ni watu safi watuhumiwa wa ufisadi na wengine wakiwa wamefika hata segerea.
f. Ulisaidiwa na serikali ya uingereza kugundua ubadhirifu na wizi wa mabilioni ya Rada na bado mtuhumiwa ndiye mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM Taifa.
2. Uliwaahidi waislamu katika ilani ya CCM ya mwaka 2005 kuwa ungewapatia mahakama ya kadhi. Je Kwa kuwa haiko kwenye ilani waislamu watarajie nini?
3. Je ni nini msimamo wako wa Tanzania kujiunga OIC?
NA YALE MTAKAYONIONGEZEA HAPA CHINI TUWAOMBE WANA CCM WENYE KUTANGULIZA MASLAHI YA TAIFA KULIKO YA CHAMA. OBAMA ALIKATAA KUMPIGIA KAMPENI MGOMBEA WA CHAMA CHAKE HUKO Rhode Island kwa kuwa haamini kama ni mfuasi mzuri wa siasa za chama chao.
Maswali ya muhimu.
1. Wapinzani wako wamekuwa wakisema kuwa wewe sio makini na kwa sababu hiyo unaweza kujikuta umesaini jambo hatari kwa taifa. Je kuna ukweli juu ya matukio haya? Kama wewe ni makini na watendaji wako sio makini basi kwa matukio yafuatayo tunaomba utuambie ulichukua hatua gani kuonyesha umakini wako?
a) Ulisaini sheria ya uchaguzi kwa mbwembwe bila ya kuisoma huku ikiwa imechakachuliwa.
b) Ulipokea cheki yenye tarakimu tofauti na maneno kwa shukrani na kukubali kupigwa picha huku ukiionyesha.
C.) Uliwahi kumwita mkurugenzi wa wilaya moja kuja kuchukua gari na alipofika ulikasirika na kushangaa anawezaje kuchukua gari la mkurugenzi mwingine?
d) Ulishangilia kwa makofi riport iliyokuwa ikisomwa mbele yako kuwa shs Bilioni 3 zilitumika kwa matundu ya vyoo vya shule nne kwa matundu manne kila shule kwa gharama ya shs Milioni 700 kwa jumla ya shs Bilioni zaidi ya 3.
e) Uliwainua mikono na kuwaita ni watu safi watuhumiwa wa ufisadi na wengine wakiwa wamefika hata segerea.
f. Ulisaidiwa na serikali ya uingereza kugundua ubadhirifu na wizi wa mabilioni ya Rada na bado mtuhumiwa ndiye mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM Taifa.
2. Uliwaahidi waislamu katika ilani ya CCM ya mwaka 2005 kuwa ungewapatia mahakama ya kadhi. Je Kwa kuwa haiko kwenye ilani waislamu watarajie nini?
3. Je ni nini msimamo wako wa Tanzania kujiunga OIC?
NA YALE MTAKAYONIONGEZEA HAPA CHINI TUWAOMBE WANA CCM WENYE KUTANGULIZA MASLAHI YA TAIFA KULIKO YA CHAMA. OBAMA ALIKATAA KUMPIGIA KAMPENI MGOMBEA WA CHAMA CHAKE HUKO Rhode Island kwa kuwa haamini kama ni mfuasi mzuri wa siasa za chama chao.