Mdada niliyewahi mkimbia lodge ndiye Hakimu kwenye kesi yangu leo

Ushimen

JF-Expert Member
Oct 24, 2012
36,775
83,955
Ni miaka 12 sasa, huyu mwali tulikutana kwenye usahili katika moja ya makampuni makubwa yaliyowekeza Tanzania.

Kwa bashasha tulitokea kuelewana na tukafahamiana ndani ya muda mfupi, na vijana wana msemo kwamba binti alinielewa baada ya kuonesha kumjali kwa mambo kadhaa.

Baada ya usahili, tukakubaliana twende tukachukue room moja on our way back after interview, na ikawa hivyo.

Basi tulipofika eneo husika tukachukua room na kisha nikamuacha aoge then mie nikazunguka sehem kupata beer chache ili nilegeze misulu ya ubongo.😎

Sasa niliporejea room na kifurushi cha chipsi mayai, nikakuta mwali ameshalala na kajifunika...🤠 Na kwa tamaa zangu ghafla mate yakanijaa mdomoni nikiwaza tendo moja tu 😇 Chap nikamuamsha mwali na nikakimbilia kumfunua shuka ili aamke. Duhhhh ghafla nikaona mwali ametokwa na macho na ghafla akaanza kuunguruma kama Simba na macho yalimtoka mujarab kabisa. 🤥 Wakuu, nilitoka mbio huku nikipiga makelele ya kutafuta msaada na kisha wageni pale lodge wakatoka nje ili kuangalia kulikoni.🤓 Kisha Mhudumu wa lodge akakuja na kitu kama ubani na akachoma kisha mwali akatulia.😜

Baada ya hapo niliondoka na nikatokomea kwenye lodge nyingine na nikajikuta naacha kitambulisho na viatu room kwa yule dada.😂

Sasa bahati mbaya kwake/nzuri kwangu yule mwali hakufanikiwa kuchaguliwa kupata kazi pale na mimi nikawa nimepata, hapo nikaona poa na maisha yakaendelea.☺️

Last week nilipata issue fulani na imefikia hatua ya kupelekwa mahakamani na nikatakiwa kuhudhuria leo kwa pilato. Wakati naingia, ghafla nikajikuta nimekaa mbele ya mwali niliemkimbia lodge (kwasababu alipandisha maruhani), na yeye ndie mtoa maamuzi kwenye kesi yangu.😶

Sasa wakuu naombeni ushauri, nimkaushie ama nijifanye namfananisha ama nimdanganye kwamba tupo mapacha ama nimkumbushe tulipo wahi kuonana?

Maana wakati anasikiliza kesi yetu, alikuwa ananiangalia sana.☹️
 
Ni miaka 12 sasa, huyu mwali tulikutana kwenye usahili katika moja ya makampuni makubwa yaliyowekeza Tanzania.

Kwa bashasha tulitokea kuelewana na tukafahamiana ndani ya muda mfupi, na vijana wana msemo kwamba binti alinielewa baada ya kuonesha kumjali kwa mambo kadhaa.

Baada ya usahili, tukakubaliana twende tukachukue room moja on our way back after interview, na ikawa hivyo.

Basi tulipofika eneo husika tukachukua room na kisha nikamuacha aoge then mie nikazunguka sehem kupata beer chache ili nilegeze misulu ya ubongo.😎

Sasa niliporejea room na kifurushi cha chipsi mayai, nikakuta mwali ameshalala na kajifunika...🤠 Na kwa tamaa zangu ghafla mate yakanijaa mdomoni nikiwaza tendo moja tu 😇 Chap nikamuamsha mwali na nikakimbilia kumfunua shuka ili aamke. Duhhhh ghafla nikaona mwali ametokwa na macho na ghafla akaanza kuunguruma kama Simba na macho yalimtoka mujarab kabisa. 🤥 Wakuu, nilitoka mbio huku nikipiga makelele ya kutafuta msaada na kisha wageni pale lodge wakatoka nje ili kuangalia kulikoni.🤓 Kisha Mhudumu wa lodge akakuja na kitu kama ubani na akachoma kisha mwali akatulia.😜

Baada ya hapo niliondoka na nikatokomea kwenye lodge nyingine na nikajikuta naacha kitambulisho na viatu room kwa yule dada.😂

Sasa bahati mbaya kwake/nzuri kwangu yule mwali hakufanikiwa kuchaguliwa kupata kazi pale na mimi nikawa nimepata, hapo nikaona poa na maisha yakaendelea.☺️

Last week nilipata issue fulani na imefikia hatua ya kupelekwa mahakamani na nikatakiwa kuhudhuria leo kwa pilato. Wakati naingia, ghafla nikajikuta nimekaa mbele ya mwali niliemkimbia lodge (kwasababu alipandisha maruhani), na yeye ndie mtoa maamuzi kwenye kesi yangu.😶

Sasa wakuu naombeni ushauri, nimkaushie ama nijifanye namfananisha ama nimdanganye kwamba tupo mapacha ama nimkumbushe tulipo wahi kuonana?

Maana wakati anasikiliza kesi yetu, alikuwa ananiangalia sana.☹️
Muombe aanze kukuroma tena tena!
 

Similar Discussions

20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom