Mchungaji wangu ni heri utubu kwani uliyonifanyia yatakupeleka motoni.

Huyo binti alikuwa hakupendi kabisa hivyo akaungana na mchungaji kukuziba kinywa kidiplomasia tu. Shukuru Mungu hukumuoa kwani ungechapiwa siku hiyo ya sendoff
 
"MUNGU KWANZA, MENGINE BAADAE?"

kwanza pole ndugu yang ktk iman, pili kumbuka mchungaji ni binadam kama ulivyo wewe, isimhukum kana kwamba yy ni malaika.. hiyo haikuwa ridhiki yako naamini kuna wako yupo njiani, hivi huyo mwanamke hana hata akiri ya kujiuliza kuwa kwa nini karata itoke kwako hadi kwa mtoto wa mchungaji ndani ya mda mfupi? pia hana busara ya kujiongeza kuwa kuna figisu, me naamin hata huyo mdada hakuwa na mapenzi ya dhati kwako, na kama angekuwa na mapenzi ya dhati kwako basi mngeamua kwenda kupima nae sehem nyingine, hiyo ndio ingekuwa siraha bora ya kumuumbua huyo pastor.

piga window10 mambo yote yanayomhusu huyo mdada, na maisha yasonge.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama wiki tatu zilizopita niliandika Uzi ululioelezea namna nilivyopata mchumba wangu kwenye kanisa moja la kisabato na jinsi mchungaji alivyotuandikia barua ili tukampe daktari ili tupime UKIMWI kama maandalizi ya ndoa yetu mimi na huyo mchumba wangu.

Pia nilieleza zaidi kuwa baada ya kupima katika hospital moja inayomilikiwa kanisa la kikatoliki na baadaye tukapewa bahasha yenye majibu ili tukampe mchungaji kwa sharti la kutokuifungua.

Nafikili mnakumbuka kuwa baada ya kumpa mchungaji bahasha ile aliomba wazazi wetu waje na akawaambia eti Mimi nimeathirika na mwenzangu mzima hivyo ndoa hakuna.

KUMBE UKWELI NI KWAMBA:
Mchungaji wangu alinifanyia hujma ili nisiweze kufunga ndoa na binti yule kwa kile kinachoaminika kwamba mchumba wangu yule alikuwa na mahusiano na mtoto wa huyo mchungaji wa kisabato kwa muda mrefu bila mimi kujua.

Na jumamosi iliyopita ndoa yao imetangazwa kanisani huku na mimi nikishuhudia hadharani, imeniuma sana.

Kwa hiyo mchungaji wangu akishirikiana na dokta wa kikatoliki walinifanyia hujma ya kunisingizia nina UKIMWI ili tu kunitenganisha na mchumba wangu ili tu mtoto wa mchungaji aweze kumuoa mchumba wangu huyo.

Hii kitu imenisikitisha sana na nimeamini wachungaji wengi ni feki sana na ni watenda dhambi wakubwa sana.

Baba wa aliyekuwa mchumba wangu amenisimulia kila kitu kilichokuwa kimepangwa na mchungaji huyo. Ni dhambi sana.

Ni bora utubu tu mchungaji umetenda dhambi sana.
Huyu Mchungaji sio mmoja wa wale Wasabato masalia waliotaka kwenda kupeleka NENO la Mungu Israel, bila kuwa na passport?

Hakika huyo atakuwa ndiye alikuwa Kiongozi wao. Anyway, bila shaka kwa Udhalimu alokufanyia NDOA hiyo kamwe HAITADUMU.......


Sent using Jamii Forums mobile app
 
UISLAAM HAURUHUSU HATA KUTANGAZA HADHARANI KUWA HUYU BINTI NI BIKRA...

Sent using Jamii Forums mobile app
Siyo uislam tu hata kwa mpagani hawezi akasimama kwenye hadhira ya watu na kuanza kupaza sauti kwamba “huyu binti ni bikra huyu binti ni bikra” huko ni kujikweza kidini tena kishamba.

Shida mnajishusha sana kwa waarabu siku hiyo humu kuna pimbi mmoja naye akani-quote kuniambia eti mwarabu amemfundisha mtu mweusi kunawa mævi,yaani mwarabu alimshika mtu mweusi mkono akamfundisha wakati utashi wa kawaida wa binadam unampa uwezo wa kujifunza mambo madogo madogo kama hayo.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Bora umenyang'anywa huyo mke, hujitambui. Majibu mliyopewa na ya kwenu au ya mchungaji? Wewe hujui kusoma huo ni utii wa kisoro.
 
Pole Sana kaka it seems wewe ni mpole Sana ndio maana wamekuchezea huo mchezo.
If it was me najaribu kufikiria sipati picha labda may be huyo binti hakupendi ndio maana ameshiriki kwenye Hilo tukio.
Kama kweli anakupenda hapo ingekua Mimi hiyo ndoa ingehailishwa trust me.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulikuwa mjinga Kiasi kwenda kupima moja kwa moja sehemu uliyo ambiwa?

Kipimo cha Ukimwi ni Dakika 20

Wajuzi wa mambo huwa tunaenda pembeni kwanza chocho tunapima mara tatu tatu tunajiridhisha ndio tuna rudi kwa waulimwengu kwa mbwembwe zote
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom