Kifaru86
JF-Expert Member
- Apr 22, 2017
- 1,734
- 3,802
Leo wakati nimefungulia redio kuna mchungaji alikuwa anafundisha maswala ya mke mwema na mume mwema anaitwa Mchungaji Peter.
Moja kati ya vitu alivyovizungumza upande wa wadada ya kwamba mwanadada yeyote anaetafuta mchumba au mume ambae tayari ana mafanikio yaani ana nyumba, mali na magari ana SAFARI NDEFU katika maisha yake ya sasa na baadae uko anapoelekea.
Aliendelea kwa kusema ukiona mwanaume yeyote tayari ana mafanikio ya kumiliki mali na vitu vyote unavyomuona navyo kabla ya kumiliki hizo mali kipindi akiwa hajamiliki hizo mali tayari alishakuwa na mchumba wake ambae alimsapoti mpaka kufikia hatua hiyo hivyo mwanaume huyo anajua alipoanzia na alipotokea.
Aliendelea kwa kusema mwanadada yeyote ambae hadi sasa anasubiri mchumba ambae tayari ana mafanikio atambue ya kwamba SAFARI yake ni ndefu sana na mwisho wa siku atajikuta amefika sehemu ambayo hajaitambua yupo wapi na amefikaje huko alipo.
Hiyo ni kwa kifupi hayo ni maneno ya mchungaji sijui mnayazungumziaje.
Moja kati ya vitu alivyovizungumza upande wa wadada ya kwamba mwanadada yeyote anaetafuta mchumba au mume ambae tayari ana mafanikio yaani ana nyumba, mali na magari ana SAFARI NDEFU katika maisha yake ya sasa na baadae uko anapoelekea.
Aliendelea kwa kusema ukiona mwanaume yeyote tayari ana mafanikio ya kumiliki mali na vitu vyote unavyomuona navyo kabla ya kumiliki hizo mali kipindi akiwa hajamiliki hizo mali tayari alishakuwa na mchumba wake ambae alimsapoti mpaka kufikia hatua hiyo hivyo mwanaume huyo anajua alipoanzia na alipotokea.
Aliendelea kwa kusema mwanadada yeyote ambae hadi sasa anasubiri mchumba ambae tayari ana mafanikio atambue ya kwamba SAFARI yake ni ndefu sana na mwisho wa siku atajikuta amefika sehemu ambayo hajaitambua yupo wapi na amefikaje huko alipo.
Hiyo ni kwa kifupi hayo ni maneno ya mchungaji sijui mnayazungumziaje.