Heci
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 3,458
- 5,773
Mchungaji Owdencalm Mpayo amefariki dunia alasiri ya leo katika hospital ya Rufaa Mbeya alikokuwa amelazwa kwa ajili ya matibu.
Wakati wa uhai wake, Mchungaji Owdencalm Mpayo aliwahi kuhudumu kwenye nafasi mbalimbali za uongozi wa kiroho.
Mchungaji Owdencalm Mpayo ameshawahi kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Kiroho la NEW LIFE MINISTRY ambapo walikuwa wakizunguka nchi mbalimbali kushudia, kufundia kanuni nne za kiroho na kuonuesha sinema za maisha ya Yesu.
Pia Mchungaji Owdencalm Mpayo amewahi kuwa Kiongozi Mkuu wa kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi.
Marehemu ameacha mke, watoto watatu na wajukuu saba.
Watoto wa Mchungaji Owdencalm Mpayo ni Elihuruma Mpayo wa Swissport, Isaac Mpayo wa ITV RADIO ONE, na Rebecca Mpayo.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa.