Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,792
Siasa zitawachonganisha... Msigwa ni mwanasiasa na yuko kwa maslahi ya wengi hivyo press conference ile ilikuwa muhimu hasa baada ya kuzushiwa kuhamia CCM... Wewe kama mwana ndugu ulikuwa na nafasi muhimu ya kulitatua hili kifamilia kuliko kuja huku na kumsema
Jr
Nimemsikiliza kwa makini ndugu yangu PETER MSIGWA kwenye hotuba yake na vyombo vya habari ambapo yeye na viongozi wengine wa Chadema waliokuwa gerezani wameachiwa huru baada ya kulipa faini.
Kilichonishangaza ni MSIGWA kushindwa kutambua mchango wetu wa kifedha uliokuwa unaratibiwa na kaka yake, BERNET MSIGWA ambapo kwa ndugu wa huku Iringa tulifanikiwa kukusanya jumla ya milioni 2 na baadae alikwenda kuomba msaada kwa mwanafamilia mwenzetu Mhe. Rais JOHN MAGUFULI ambaye alijitolea sh. milioni 38.
MSIGWA kwa kutanguliza maslahi ya Chadema umeikana michango yetu wanandugu, eti kwa sababu wakati kaka yake BERNET anashughulika kukutoa gerezani aliambatana na POLEPOLE ambaye kutokana na Mhe. Rais kutingwa na Majukumu alimuagiza ashirikiane nae.
Ndugu yetu PETER kumbuka kuna maisha baada ya Siasa, kuna muda utastaafu Siasa, utapata misiba(japo siombei hilo)na hata kufariki dunia, sisi ndugu zako ndio tutakaowajibika kukusitiri na kusaidia familia utakayoiacha Chadema hawata kuwa na wewe tena.
Ni raia yangu utajitokeza kwa wanandugu kuomba msamaha juu ya jambo hilo, ikumbukwe kwa mila na desturi zetu za kihehe mafadhaiko uliyosababisha kwetu yanaweza kukusababishia laana ya kushindwa ubunge kwenye uchaguzi na kufukuzwa uanachama na Chadema.
Ndimi ndugu yako,
Luvanda Ngurusavangi Msigwa
Igumbilo, Iringa.
Jr