Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,090
Akiongea na Darmpya, mchungaji Msigwa amekosoa vikali hatua ya Maalim Seif na Zitto Kabwe kujiunga na serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar, Mchungaji Msigwa amekiita kitendo hicho kama ni flipfloping. Amesema ni kuwachanganya wananchi kutoa misimamo inayokinzana katika jambo lilelile.
Kwa mfano mwezi uliopita Mkuu wa Chama cha ACT Zitto Kabwe alitia saini tamko la pamoja akiwa na Mwenyekiti wa Chadema, na Makamu Mwenyekiti wa Chadema tamko la kutokubaliana na uchaguzi mkuu uliopita, katika tamko hilo walikubaliana pia kutotambua matunda yoyote ya uchaguzi huo, lakini kabla hata vumbi la uchaguzi halijatulia, Zitto kageuka, anatetea ACT kuingia katika serikali waliyoiita haramu hapo mwanzo.
Msigwa anavunja hoja ya Zitto anayedai kuwa kama ukimdai mtu kitu kisha akakupa kidogo basi chukua kidogo hicho kisha endelea kudai, Msigwa anasema hiyo ni hoja mfu, ni sawa na jambazi akuvamie kwa mabunduki akupore kila kitu akubakishikie kitanda kisha kwa kunyenyekea umshukuru jambazi huyo kuwa umemuona ana nia nzuri na wewe!
Pia Mchungaji Msigwa anasema kuwa walichokifanya akina maalimu ni kugawana vyeo tu na wala siyo hoja ya maendeleo, akahoji kuwa je kwani Zanzibar haiwezi kuendekea bila Maalim? Na akahoji pia je Kwa Maalim kuingia kwenye hiyo serikali kunafanikisha vipi uwepo wa tume huru ya uchaguzi na demokrasia ambayo vyama vya upinzani vimekuwa vikipigania? - Msigwa amesema, hapo ishu ni vyeo tu na wala siyo kuadvance mambo ambayo wapinzani walikuwa wakipigania kinyume cha CCM.
Unaweza kuona mahojiano zaidi hapa.
Kwa mfano mwezi uliopita Mkuu wa Chama cha ACT Zitto Kabwe alitia saini tamko la pamoja akiwa na Mwenyekiti wa Chadema, na Makamu Mwenyekiti wa Chadema tamko la kutokubaliana na uchaguzi mkuu uliopita, katika tamko hilo walikubaliana pia kutotambua matunda yoyote ya uchaguzi huo, lakini kabla hata vumbi la uchaguzi halijatulia, Zitto kageuka, anatetea ACT kuingia katika serikali waliyoiita haramu hapo mwanzo.
Msigwa anavunja hoja ya Zitto anayedai kuwa kama ukimdai mtu kitu kisha akakupa kidogo basi chukua kidogo hicho kisha endelea kudai, Msigwa anasema hiyo ni hoja mfu, ni sawa na jambazi akuvamie kwa mabunduki akupore kila kitu akubakishikie kitanda kisha kwa kunyenyekea umshukuru jambazi huyo kuwa umemuona ana nia nzuri na wewe!
Pia Mchungaji Msigwa anasema kuwa walichokifanya akina maalimu ni kugawana vyeo tu na wala siyo hoja ya maendeleo, akahoji kuwa je kwani Zanzibar haiwezi kuendekea bila Maalim? Na akahoji pia je Kwa Maalim kuingia kwenye hiyo serikali kunafanikisha vipi uwepo wa tume huru ya uchaguzi na demokrasia ambayo vyama vya upinzani vimekuwa vikipigania? - Msigwa amesema, hapo ishu ni vyeo tu na wala siyo kuadvance mambo ambayo wapinzani walikuwa wakipigania kinyume cha CCM.
Unaweza kuona mahojiano zaidi hapa.