Mchungaji Msigwa akiri kumsingizia Kinana ujangili, amwangukia na kumwomba radhi

Mchungaji Msigwa ni muongo. Amekiri mwenyewe hadharani. Katika kitabu cha Ufunuo kwenye biblia imeandikwa " Waongo wote sehemu yao ni katika ziwa lile liwakalo moto na kiberiti".

Mbowe , waumini wako na watanzania kwa jumla wawe makini na wewe maana wewe ni MUONGO

Je ulidanganya bure au kwa maslahi ya wawindaji wako waliokuwa wanakuhonga mara kwa mara?

Jela sio mchezo. Msigwa toka atoke Segerea amekuwa muoga sana. Ametekeleza amri ya mahakama bila shida. Ameamua asikate rufaa ili amalizane na kesi hii akiwa bado Mbunge maana kuja kupambana na kesi ukiwa mtaani bila posho ni BALAA KUBWA.

MUNGU HAMFICHI DHALIMU. Asanthe Mzee Kinana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona bwana mkubwa alisema UONGO kuwa vichwa vya treni alivyovikuta bandarini vilikuwa havina mwenyewe?

Wakati ukweli ni kwamba vichwa hivyo vilinunuliwa na serikali ya JK?

Bwana mkubwa mpaka leo hajakiri UONGO wake.
 
Mie sio mwanasiasa ila katu katika Maisha yangu sitaweza kuamini anachosema mwanasiasa. Hiyo nilishajiapia. Jana kilio cha Mh. Lijualikali nacho ni cha uongo wa mchana kweupe. CCM msimpe nafasi ya kugombea chama kina wengi tu Zaidi yake
 
Kuomba radhi ni uungwana japo ilitakiwa afanye hivyo kabda ya hukumu ya mahakama kuu.

Hii pia inatoa taswira kwamba madai mengi ya wanasiasa yanakua ya uongo kwa ajili ya malengo ovu au kupata umaarufu wa kisiasa. Bahati mbaya sana malengo yao hayo huumiza watu kwa kuwavunjia heshima zao katika jamii, heshima ambazo wengine wamejijengea kwa miaka mingi
Si ya uongo kumzushia mtu muelewa ujue utapambana na mahakama ukiona kimya kuna harufu ya ukweli ila ili ujue siasa inatakiwa uwe na upeo mkubwa sana wa akili hapo siasa imechukua mkondo wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vua gwanda vaa gamba hali ya kisiasa inayoendelea ndani ya CDM inadhihirisha wazi kuwa bado CCM itaendelea kuwapo madarakani kwa miaka mingi sana.

Kauli ya Mh Msigwa inadhihirisha kuwa kauli nyingi za akina TL, ZZK na wengineo ni kwa lengo la kujijengea umaarufu wao kisiasa na wala si kwa ajili ya mama Tanzania naungana na Jobu Ndugai yawezeka next time upande ule ukawa na mbunge mmoja.

Awaombe radhi pia na BAVICHA aliowaaminisha uongo huo na kuwajaza hiyo sumu kwa muda mrefu. Hakika safari ya anguko la CDM limefika mwisho toka lilipoanza safari yake 2015
 
..mbona bwana mkubwa alisema UONGO kuwa vichwa vya treni alivyovikuta bandarini vilikuwa havina mwenyewe?

..wakati ukweli ni kwamba vichwa hivyo vilinunuliwa na serikali ya JK?

..bwana mkubwa mpaka leo hajakiri UONGO wake.
Hakusema yeye ila aliambiwa hivyo na watu wa Bandari kutokana na kukosekana kwa nyaraka za mzigo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom