Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.

Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.

Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.

Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.

Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!
 
Safi sana
images%20-%202020-03-11T195221.449.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ah ah lete picha babu, yoi know pics speaks louder than words. walimchukulia msigwa kisport sport, wameula wa chuya.

Ameziheshimu jitihada za wananchi walochanga ili kuwaweka guru,

asante sana Mh msigwa
Habari,

Hii ni baada ya Polepole na team yake ya Lumumba kujaribu kutafuta Kiki ya kisiasa kupitia hukumu ya viongozi wa Chadema.

Naona walizidiwa akili, documents za ushahidi wa malipo Chadema wamezitoa lakini ccm hawajazitoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.

Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.

Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.

Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.

Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!
Matumizi mabovu ya mamlaka na Mali za umma.Magari ya serikali ya nini huko na Polepole ni kiongozi wa chama au?
Hongera Mch.Msigwa,huo ndiyo uzalendo unaotakiwa,siyo hao waigizaji.Hii inaonyesha mikakati iliyoandaliwa kupitia kesi hii na hukumu yake.Wameshindwa na kulegea.Aibuuu!
 
Back
Top Bottom