Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,372
Wadau, naangalia Bunge Live kupitia TBC1. Mchungaji msigwa ameuliza swali la kutaka mkakati wa serikali kukabiliana na uharibifu wa mazingira kutokana na wananchi wengi kutumia nishati ya kuni kama chanzo cha nishati ya kupikia. Mchungaji msigwa amesema kuwa kwa takwimu alizonazo ni kuwa Watanzania wanakata wastani wa Ekari 300 kwa siku sawa na Hekta 800. Kwangu nilipata shida sana kumuelewa na nikajiuliza kama kweli Mchungaji Msigwa anajua anachokisema au kuna mtu amemkaririsha.
Nijuavyo ni kuwa Ekari 300 ni sawa na Hekta 121.407. Kwa wale wataalam wa kukokotoa wanaweza wakatusaidia. Hii ni kutokana na ukweli kuwa Hekta moja ni sawa na Ekari 2.5. Hivyo kwa Ekari 300, haiwezi kuwa Hekta 800. Hata kama anaweza kujitetea kuwa alibadili hivyomvipimo bila ya kujijua, Hekta 300 haiwezi kuwa sawa na Ekari 800 bali ni sawa na Ekari 741. Kutokana na ufafanuzi huo, nimemdharau sana mchungaji Msigwa na napata shida kubaini uelewa wake.
Natoa angalizo kwa wanasiasa kutokurupuka kutoa hoja ambazo hawajui undani wake. Ni vema mchungaji Msigwa angeuliza kwanza ili apate ufafanuzi wa hivi vipimo vya Hekta na Ekari ili kukwepa aibu hii iliyomkuta.
Nawasilisha.
Nijuavyo ni kuwa Ekari 300 ni sawa na Hekta 121.407. Kwa wale wataalam wa kukokotoa wanaweza wakatusaidia. Hii ni kutokana na ukweli kuwa Hekta moja ni sawa na Ekari 2.5. Hivyo kwa Ekari 300, haiwezi kuwa Hekta 800. Hata kama anaweza kujitetea kuwa alibadili hivyomvipimo bila ya kujijua, Hekta 300 haiwezi kuwa sawa na Ekari 800 bali ni sawa na Ekari 741. Kutokana na ufafanuzi huo, nimemdharau sana mchungaji Msigwa na napata shida kubaini uelewa wake.
Natoa angalizo kwa wanasiasa kutokurupuka kutoa hoja ambazo hawajui undani wake. Ni vema mchungaji Msigwa angeuliza kwanza ili apate ufafanuzi wa hivi vipimo vya Hekta na Ekari ili kukwepa aibu hii iliyomkuta.
Nawasilisha.