Mchungaji Lwakatare Arudisha Yatima 250 Kwao

MwanaHabari

JF-Expert Member
Nov 9, 2006
442
13
Nimepata Habari kwamba mchungaji Lwakatare ameamua kurudisha Yatima 250 makwao kwa kisingizio kwamba hawezi kuwaangalia pale Tabata. Wanaorudishwa mikoani kwao wakiwemo wale wameathiriwa na HIV. Habari kutoka kwa wafanyakazi pale, plan ya kuwaondoa yatima ni kuandaa nafasi ya majengo ya orphanage kugeuzwa kuwa University.

Naomba kama kuna mtu ana habari zaidi aweze kunisaidia, maana huyu mchungaji there is something fishy going on, na kuchezea maisha ya yatima is something serious, so i am interested kama kweli ni mtu wa kusaidia watu au ana badilisha miradi tu at the expense of the disadvantaged people.
 
Mchungaji Getrude Rwakatare alikuwa maji ya kunde, sasa ametakata kwa pesa na wokovu. Pesa ni shetani, kama ni kweli anawarudisha yatima makwao, then shetani la pesa limesha mwingilia.
Nilipomuona kwenye siasa, nikajua ama anapeleka wokovu bungeni kwenda kuliokoa bunge letu shirikina dhidi ya matukio ya ushirikina, ama uchungaji wake ni wa tamaa ya madaraka.
Aliwahi kuhubiri juu ya utajiri na kusema kusudio la Mungu kwa watu wake ni utajiri katika nchi ya maziwa na asali. Akasisitiza umasikini ni laana.
Hivyo yawezekana hao watoto yatima sasa yaonekana wamelaaniwa, hivyo ameamua kunawa mikono kwa kuwarudisha makwao wakafie mbele.
Tusiseme sana, ngoja tusubiri uthibitisho.
 
makanisa hapa tanzania yamegawanyika kutokana na muhubiri, kama unahitaji misukule basi we nenda ubungo, kama utahitaji utajiri we nenda kwa mama Lwakatare, huyu mama tangu mwanzo alikuwa ameplan kutafuta fedha kwa mgongo wa NGO ambayo itakuwa inaenda sambamba na mambo ya dini na ndo kisa cha kutumia hilo jina la St Mary kwa hiyo hizo shule msingi wake zilikuwa za kusaidia watoto yatima na watu wasio na uwezo katika hiyo NGO yake, lakini pepo la fedha lilipojiinua, akabadilisha mwelekeo na wale wafadhili walipogundua kwamba sasa mama hayupo tena kwenye mstari wakajitoa kumfadhil lakini walikuwa wameshachelewa kwani mama alikuwa tayari keshakuwa na base imara ya kusonga mbele
kama unavyojua walokole awaamini habvari hizo za watakatifu wa kutamkwa(nje ya biblia) sasa huyo mama ilikuaje atumie hilo jina la St Mary, point ni kwamba alikuwa anataka kuwakama hao waliokuwa na fedha na walikuwa wanataka kuwsaidia watu wa dunia ya tatu,
sasa mama yuko siasani hebu tusubiri tuone kitakachoendelea
 
Nyie watu, ni nani mwenye jukumu la kulea yatima? ni Lwakatare?

Jukumu la kulea yatima ni la kwetu sote, kama yeye anarudisha hao yatima makwao tatizo liko wapi? Ningeona vibaya kama angeamua kuwatelekeza, kumbe yeye ametimiza wajibu wake, basi ni kazi yetu sasa kujadili kama tunaweza kuwachukua au la?
Tusiwe mafundi wa kuongea ilihali kumbe hata moyo wa kuwasaidia yatima ndani ya familia zetu hatuwezi.
 
Nyie watu, ni nani mwenye jukumu la kulea yatima? ni Lwakatare?

Jukumu la kulea yatima ni la kwetu sote, kama yeye anarudisha hao yatima makwao tatizo liko wapi? Ningeona vibaya kama angeamua kuwatelekeza, kumbe yeye ametimiza wajibu wake, basi ni kazi yetu sasa kujadili kama tunaweza kuwachukua au la?
Tusiwe mafundi wa kuongea ilihali kumbe hata moyo wa kuwasaidia yatima ndani ya familia zetu hatuwezi.

Point tupu! ni wajibu wetu sote kulea yatima yeye kafanya mpaka hapo alipofika wengine tumsaidie.
 
Nyie watu, ni nani mwenye jukumu la kulea yatima? ni Lwakatare?

Jukumu la kulea yatima ni la kwetu sote, kama yeye anarudisha hao yatima makwao tatizo liko wapi? Ningeona vibaya kama angeamua kuwatelekeza, kumbe yeye ametimiza wajibu wake, basi ni kazi yetu sasa kujadili kama tunaweza kuwachukua au la?
Tusiwe mafundi wa kuongea ilihali kumbe hata moyo wa kuwasaidia yatima ndani ya familia zetu hatuwezi.

Nakiri she has done something on the welfare of orphans than most of us combined..

Tuache kupiga domo na kufanya homework zetu..
 
sasa mama yuko siasani hebu tusubiri tuone kitakachoendelea

Endelea tu kusubiri badala ya kufanya homework yako halafu uone utakachovuna..

JF is my favourite b'coz hapa nadhani ndo haswa unaweza kujua kwa jinsi gani nchi yetu ina watu wa aina gani..

LOL..
 
..... Tusiseme sana, ngoja tusubiri uthibitisho.

Ndo unakumbuka shuka asubuhi?

Usiseme nini wakati umeshamaliza yoote na kuua personality ya mtu bila uthibitisho..

Hawa ndo ma-pundit wa JF..LOL..
 
Hapo ndio natoa sulute kwa wabongo, mtu ameanzisha thread haina data kamili lakini wachangiaji wa kwanza lazima wawe negative bila hata kufikiria. Siwezi shangaa mpingaji saa nyingine hajatoa hata ajira ya house girl home achilia mbali kuwa na watu zaidi ya kumi unawalipa mshahara.

Huyo mama ni mtu wa kupigiwa mfano, kuanzisha biashara na ikasimama bongo kwa zaidi ya miaka 10 unahitaji salute. Kama kurudisha yatima home inawezekana ikawa kwa good reason, manake wafanyakazi wanazalisha na wanarudishwa home itakuwa NGO inayohitaji pesa kutoka kwa wafadhili ambao hivi sasa wanamatatizo ya kiuchumi kwao na hawawezi kutusaidia kama walivyofanya kipindi kilichopita.

Labda mjadala ungehusu namna ya kuwasaidia yatima kama watarudi au Mch. aendelee kukaa nao kwa utaratibu upi, manake wabongo utamaduni wa kusaidia yatima bado ni tatizo, manake mtu anakuwa yatima kwa kufiwa na baba na mama, sasa mjomba, shangazi, jamaa, jirani, wanaukoo, kabira moja, dini, babu au bibi si wapo jamani.

Kupiga soga kila kukicha hakuwezi kulipa bili, mwisho wa siku lazima chakula, maji umeme n.k vilipwe.

Salute Mama Lwakatare kama umeshindwa, wengine waendelee pale ulipofikia. Hii haizuii mapungufu katika utekelezaji.
 
pale sos kituo cha kulea watoto ubungo kuna nafasi 3 ziko wazi za watoto yatima mwanahabari hujasema kama hao watoto wamerudishwa kwa walezi wao au imekuwaje kuwaje au wametelekezwa au wamepelekwa kusoma shule za boarding manake mwanzo wa mwaka huu
 
Ndo unakumbuka shuka asubuhi?

Usiseme nini wakati umeshamaliza yoote na kuua personality ya mtu bila uthibitisho..

Hawa ndo ma-pundit wa JF..LOL..
Kwa vile mtindio ni tatizo la kuzaliwa nalo, si busara kucheka kilema ni kumuombea uponywaji.
Hakuna ubishi juu ya wema wa Mama Rwakatare, kama walivyo baadhi ya matajiri akiwemo Mh. Mengi, ni kweli wanafanya mengi makubwa katika kusaidia watu na jamii yetu, but there is something fishy. Only ones with sixth sense can smell a rat. Achilia issue ya yatima, politics is a dirty game kwa mtu wa Mungu. Mengi anafanya politics za 'the King Maker' kwa kucheza mbali, huyu mama kaingia ndani kufanya nini?. Time will tell. Bwana Asifiwe.Tuwaombee wenye mitindio wapate uponyaji. Tumsifu Yesu Kristu.
 
Kwa vile mtindio ni tatizo la kuzaliwa nalo, si busara kucheka kilema ni kumuombea uponywaji.

Really? Naona umefilisika na kuanza kuichambua hata screen-name!! Haha ha mapundit wa JF kweli ni noma...yaani ni pure bull-crap and incompetent!

Hakuna ubishi juu ya wema wa Mama Rwakatare, kama walivyo baadhi ya matajiri akiwemo Mh. Mengi, ni kweli wanafanya mengi makubwa katika kusaidia watu na jamii yetu, but there is something fishy. Only ones with sixth sense can smell a rat. Achilia issue ya yatima, politics is a dirty game kwa mtu wa Mungu. Mengi anafanya politics za 'the King Maker' kwa kucheza mbali, huyu mama kaingia ndani kufanya nini?.

Nadhani ukiishirikisha akili kidogo kabla ya kuandika utagundua kila mtu ana maisha tofauti pamoja na kwamba ni mtu yuleyule. Anaweza kuwa mchungaji lakini bado ana nafasi mbalimbali ktk jamii. Iwe ni kama mama, kama Mh. mbunge n.k. Hizi ishu za kuingia bungeni hazihusiani na ishu tunayoiongelea ambayo ni ya kijamii kuhusu mayatima. Kama una matatizo na mambo yake ya kisiasa hapa si pahala pake. U-pundit ni pamoja na kuwa na uelewa wa kutofautisha issues..

Sawasawa?

Time will tell

Time will tell iwapo tutautumia muda vizuri na kuacha ujuvi na kuwa watu negetive bila sababu za msingi..

Bwana Asifiwe.Tuwaombee wenye mitindio wapate uponyaji. Tumsifu Yesu Kristu.

Jesus The Masih ataendelea kupewa sifa yake hususan na watu wanyenyekevu wasiowazulia wengine na wenye kujua wajibu wao ktk jamii.
Hali kadhalika tuzidi kuwaombea wale wenye mitindio ya kujitakia ..

Ameen..

Kibwagizo: Heaven is Hotter than Hell
 
Really? Naona umefilisika na kuanza kuichambua hata screen-name!! Haha ha mapundit wa JF kweli ni noma...yaani ni pure bull-crap and incompetent!



Nadhani ukiishirikisha akili kidogo kabla ya kuandika utagundua kila mtu ana maisha tofauti pamoja na kwamba ni mtu yuleyule. Anaweza kuwa mchungaji lakini bado ana nafasi mbalimbali ktk jamii. Iwe ni kama mama, kama Mh. mbunge n.k. Hizi ishu za kuingia bungeni hazihusiani na ishu tunayoiongelea ambayo ni ya kijamii kuhusu mayatima. Kama una matatizo na mambo yake ya kisiasa hapa si pahala pake. U-pundit ni pamoja na kuwa na uelewa wa kutofautisha issues..

Sawasawa?



Time will tell iwapo tutautumia muda vizuri na kuacha ujuvi na kuwa watu negetive bila sababu za msingi..



Jesus The Masih ataendelea kupewa sifa yake hususan na watu wanyenyekevu wasiowazulia wengine na wenye kujua wajibu wao ktk jamii.
Hali kadhalika tuzidi kuwaombea wale wenye mitindio ya kujitakia ..

Ameen..

Kibwagizo: Heaven is Hotter than Hell
Give a dog a bad name... I thought Mtindiowaubongo was just a name, now I know your really Mtindio. God Bless you.
 
Give a dog a bad name... I thought Mtindiowaubongo was just a name, now I know your really Mtindio. God Bless you.

Bua ha ha ..

Vi-pundit uchwara vya JF..! Nachelea kuendelea kukupa maarifa maana hujui hata tofauti ya reality/metaphor etc


Kaazi kwelikweli..
 
Nimepata Habari kwamba mchungaji Lwakatare ameamua kurudisha Yatima 250 makwao kwa kisingizio kwamba hawezi kuwaangalia pale Tabata.

- Habari haijkaaa sawa, na hata ikiwa sawa hakuna tatizo mkuu kuwatunza watoto orphans ni ishu ya taifa na sisi wote sio ya Mama Rwakatare tu, tufikiri au kuuliza kabla ya kurukia JF.
 
- Habari haijkaaa sawa, na hata ikiwa sawa hakuna tatizo mkuu kuwatunza watoto orphans ni ishu ya taifa na sisi wote sio ya Mama Rwakatare tu, tufikiri au kuuliza kabla ya kurukia JF.

I think watu mna miss point, Orphans ndiyo wanatunzwa na Taifa Lote, lakini kuwarudisha tu kwao kisa unataka kuanzisha University, I am concerned with that notion. I have confirmed this story already na baadhi wanaorudi hawana ndugu huko kwao, dont think sihusiki na kulea yatima, ila ukiwatreat kama comodities tu kuendeleza miradi yako, dont do it in the first place (you cant downsize orphans!!)...these are fragile people especially the sick ones that need more care than others....

I posted it here to find out if anyone knows more about the issue, what happens to them, maybe I can help with some rather than just have them bussed somewhere where they have no hope in sight...
 
Siri iliyokuwepo ni kuwa washughulikiaji wa Makanisa yote hapa nchini wanapokea misaada kutoka nchi za nje ,ili kueneza neno,tofauti na misikiti ambayo haiendeshwi kimisaada,japo ipo baadhi inayopokea misaada lakini ni michache sana,vile vile walimu wa makanisa ambao ni mapadre na wenginetele wao wanapokea mishahara au fedha kutoka katika mashirika ya Kikristo tofauti na vyuo vya kiislamu ambavyo vimejaa mitaani au hata vingine huwemo majumbani na vinajiendesha kivyakevyake ,sidhani kama kuna elimu ya kikiristo inayotolewa majumbani au kuna mtu labda amejitolea awe anafundisha ukristo nyumbani ,kwa kweli mimi sijaona au sijasikia kuwepo kwa kitu hicho

Hivho tatizo la kuanguka kwa uchumi duniani halikuyaacha makanisa yanayofadhiliwa kwa misaada na tatizo hilo limesababisha kwa fedha kuchelewa na pengine kukosekana kabisa na kuanzisha sokomoko katika makanisa mengi si hapa Tanzania tu bali dunia nzima na ndilo tatizo hilo lilivyokosesha fedha za kuwahudumikia mayatima hao.
Kinachotakiwa ni kwa wakirto wenyewe waliopo Tz kuondoa tofauti zao na kusaidiana kwa wale wenye uwezo ili kuirudisha huduma hiyo.

Hata kwa wenye uwezo kuchangia kwa kila mwezi kama ada ambayo Waisilamu tunakuwa na kawaida kuwachangisha watoto wanaosomeshwa majumbani kwa kila mwezi mtoto anahitajika kutoa kiasi fulani ili kuendesha chuo.
 
Siri iliyokuwepo ni kuwa washughulikiaji wa Makanisa yote hapa nchini wanapokea misaada kutoka nchi za nje ,ili kueneza neno,tofauti na misikiti ambayo haiendeshwi kimisaada,japo ipo baadhi inayopokea misaada lakini ni michache sana,vile vile walimu wa makanisa ambao ni mapadre na wenginetele wao wanapokea mishahara au fedha kutoka katika mashirika ya Kikristo tofauti na vyuo vya kiislamu ambavyo vimejaa mitaani au hata vingine huwemo majumbani na vinajiendesha kivyakevyake ,sidhani kama kuna elimu ya kikiristo inayotolewa majumbani au kuna mtu labda amejitolea awe anafundisha ukristo nyumbani ,kwa kweli mimi sijaona au sijasikia kuwepo kwa kitu hicho

Hivi unajua unachoongelea au basi tu imepatikana nafasi ya kuosha kinywa na wewe unaitumia.

Eti makanisa yanaendeshwa kwa misaada.. Nenda kwenye makanisa usikilize watu wanavyotoa michango na uhakikishe kwenye vitabu vyao vya fedha..usiandikie mate wakati wino upo. Ukishamaliza hiyo kazi uje na sampling distribution yenye kuonesha sasa kama hypothesis yako ni sahihih au la ..

By the way ile ndoa yetu ya ki-fiftini youro gerl vipi maendeleo?
 
I think watu mna miss point, Orphans ndiyo wanatunzwa na Taifa Lote, lakini kuwarudisha tu kwao kisa unataka kuanzisha University, I am concerned with that notion. I have confirmed this story already na baadhi wanaorudi hawana ndugu huko kwao, dont think sihusiki na kulea yatima, ila ukiwatreat kama comodities tu kuendeleza miradi yako, dont do it in the first place (you cant downsize orphans!!)...these are fragile people especially the sick ones that need more care than others....

I posted it here to find out if anyone knows more about the issue, what happens to them, maybe I can help with some rather than just have them bussed somewhere where they have no hope in sight...

- Anaye-miss the point ni wewe mkuu, maana kwanza hii habari haina uhakika na hata ikiwa na uhakika unaulizwa ni sheria ipi ya jamhuri iliyovunjwa na Mama Rwakatare mpaka ukarukia hapa JF na kujaribu kumuharibia jina?

- Wewe kama una ubavu kwa nini usiwachukue hao watoto? Yeye amefika mahali ameamua kwenda njia tofauti sasa what is wrong with that? Labda ufafanue zaidi mkuu bado hueleweki eti? Unless un some personal ishus na huyu mama, au?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom