johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,598
- 141,414
Mchungaji Lusekelo aka mzee wa Upako amesema ni sahihi kabisa serikali kuzuia mikutano ya kisiasa wakati huu.
Lusekelo anasema chukulia mfano Chadema waliopata kura milioni 6 na ushee wakiruhusiwa kufanya mkutano na hawa wapiga kura wao wote wakaingia barabarani....je kutakuwa na amani hapo?
Kadhalika mchungaji Lusekelo ameiomba serikali kupiga marufuku mambo ya bongo movie kwani yanakwenda kinyume na utamaduni wetu na yanachochea uharibifu wa maadili.
Ametolea mfano watoto wadogo kushirikishwa kwenye sinema kinyume na sheria.
Mchungaji Lusekelo alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kutoka media mbali mbali Kanisani kwake ubungo, jijini Dsm.
Source Star tv
My take; Zile kura milioni 6 ni za Chadema au Lowassa?!?
Maendeleo hayana vyama!
Lusekelo anasema chukulia mfano Chadema waliopata kura milioni 6 na ushee wakiruhusiwa kufanya mkutano na hawa wapiga kura wao wote wakaingia barabarani....je kutakuwa na amani hapo?
Kadhalika mchungaji Lusekelo ameiomba serikali kupiga marufuku mambo ya bongo movie kwani yanakwenda kinyume na utamaduni wetu na yanachochea uharibifu wa maadili.
Ametolea mfano watoto wadogo kushirikishwa kwenye sinema kinyume na sheria.
Mchungaji Lusekelo alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kutoka media mbali mbali Kanisani kwake ubungo, jijini Dsm.
Source Star tv
My take; Zile kura milioni 6 ni za Chadema au Lowassa?!?
Maendeleo hayana vyama!