#COVID19 Mchungaji Gwajima ni wa kukamatwa na kufunguliwa kesi ya Uchochezi, Uhaini na Ugaidi

Wewe hujasoma watu kuganda damu au kufa,au hedhi kubadilika hedhi baada ya kuchanjwa?

Haya hebu tujuze long term side effects za chanjo?
Tujuze kwanini consent form inaeleza serikali haitahusika kwa lolote likimpata mgonjwa?
Hizo ni rare case hata hapa bongo kuna watu tukitumia dawa flani inaleta reactions mbaya it's normal, hata chanjo za tb, surua, polio huwa tunaxhomwa ila kuna saa Zina react negative kwa baadhi ya watu. Hafu hyo reaction ya wachache isiwe sababu eti chanjo ni mbaya mbona hata pnv, azuma nazo hudunda kwa baadhi ya watu na kwingine hufanya vizuri.
 
Hizo ni rare case hata hapa bongo kuna watu tukitumia dawa flani inaleta reactions mbaya it's normal, hata chanjo za tb, surua, polio huwa tunaxhomwa ila kuna saa Zina react negative kwa baadhi ya watu. Hafu hyo reaction ya wachache isiwe sababu eti chanjo ni mbaya mbona hata pnv, azuma nazo hudunda kwa baadhi ya watu na kwingine hufanya vizuri.
Hofu lazima iwepo inapohusisha RNA na DNA lol.
 
Napenda kutoa Rai kwa Vyombo vya Ulinzi na usalama kumkamata mara moja Mh Gwajima, kumuhoji na kumshitaki kwa counts tatu za msingi.Sitaki kuzungumzi hotuba ya Mch Gwajima kanisani kwake juzi, kwani si jambo geni humu na litaunganisha uzi na nyuzi zingine kama hizo. Mods Nakimbilia moja kwa moja kwenye hoja kuu ya Uzi huu.

Kwa muelekeo wa kamati ya Mh. Samia na ushauri wake, na kwa maamuzi ya serikali kuhusu kuchanjwa. Sote tuna imani wataalamu wetu wa afya wameshirikishwa vya kutosha, pia tunaamini vyombo vyetu vya usalama nikimaanisha idara ya Usalama wa Taifa wameshafanya Upembuzi yakinifu na juu ya tuhuma hizi za chanjo ya Covid kuwa hatari kwa maisha yetu. Kwa hiyo mpaka chanjo inaingia maana yake "there is no doubt about it" . Lakin tunafahamu hata itakapoingia itachunguzwa pia na kuthibitishwa zaidi.

Kimantiki ninashauri Mch Gwajima afunguliwe kesi 3 za msingi ambazo ni Uchochezi, Uhaini na Ugaidi kwa jinsi nilivyojifunza muundo wa siasa zetu.

Shitaka la kwanza la uchochezi liko Clear kuwa ana"mislead " wananchi kwa kupotosha kitu ambacho hajafanyia utafiti kitaalamu maana alitakiwa aje na ripoti yake ya uchunguzi kitaalamu tungemuelewa. Gwajima ni mbunge na ni kiongozi wa kiroho hivyo ana ushawishi mkubwa sana. Inavyoonekana anatumia ushawishi wake kuwagawa watanzania, kuwafanya Raia kupinga maamuzi ya serikali, anaingilia masuala nyeti ya afya za watanzania. Hebu tujiulize ikitokea Bagonza akapinga Chanjo ya Surua, Bakwata wakapenga ya Pepopunda, Makamba akapinga ya Polio itakuwaje huko Mbele. Nauona huu ni uchochezi kabisa.


Kwanini afunguliwe kesi ya Uhaini, ni kwa sababu anaingilia Muenendo wa Rais, viongozi wakuu wa serikali na vyombo vya usalama vya nchi. Kwa kauli yake Gwajima anaamuru maaskari, makachero na maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama wasichanjwe huku akiwatishia kuwa watadhurika. Hii litawafanya wao kukwepa au kupinga amri hii na hapa Gwajima atakuwa "accessory after the fact" ya uhaini huu wa Askari wetu. Lingine ni kutuhakikishia kuwa Viongozi wakuu wa serikali akiwamo Rais watadhurika ama hata kufa baada ya kutumia Chanjo hii. Gwajima anapaswa kuhojiwa na kuiambia Serikali ametoa wapi taarifa hizi za Rais kudhurika kama akitumia hii chanjo. Itakapokuja kutokea isije ikaonekana alikuwa na maono ama vip. Iisje maadui zetu wakapata mwanya huohuo wa maneno ya Gwajima kumdhuru Rais wetu mpendwa.

La mwisho Gwajima napaswa kupewa kesi ya Ugaidi ama kuhusishwa na huu ugaidi ama kuwa shahidi wa muhimu wa njama za ugaidi anaousemea yeye against taifa letu. Gwajima anajua ama ana taarifa za watanzania Mamilioni kudhurika ama hatimaye kufa kwa matumizi ya dawa hizi. Anaaswa kukamatwa na kuhojiwa kwa habari hizi. Nevertheless kama si kweli kesi ya ugaidi inamuhusu. Huu ni ugaidi wa kifikra na mawazo ya watanzania ikiwemo kuwatia hofu "Terror -> Terrorism" .

Nitoe Rai jwa vyombo vya ulinzi na usalama kumchukulia hatua Askofu Gwajima, tuache yale ya watu kusema Mkuu fulani anaumwa, mkuu fulani atafariki na wakachekewa hatimaye inakuwa kweli then wanaitwa manabii.



Na pindi ikitokea hii chanjo kuna mtu amedhurika , Mtuhumiwa wa kwanza awe Gwajima. Ikitokea Covid ikatupiga zaid sababu ya kutochanjwa Gwajima anatakiwa ashitakiwe pia kwa kutufanya tupingane na WHO .

Kazi na iendelee!..
Naunga mkono. Huyu Gwajima akamatwe ili awataje hao anatuhumu wamepewa pesa na Bill Gates na kuthibitisha.
 
Mawazo hayapigwi rungu! Ni vizuri kumkosoa kwa hoja na kwa tafiti zilizothibitishwa kisayansi na wataalamu!
Kumnyamazisha wakati anatoa hoja kwa kile anachoamini ni kumwonea!
 
Dah! Hiyo aya ya pili kutoka mwisho mbona ya kibabe sana...

Watu wakidhurika kwa chanjo (wakichanjwa) akamatwe ashtakiwe na hata watu wakidhurika kwa corona (wasipochanjwa) akamatwe pia!
 
Mawazo hayapigwi rungu! Ni vizuri kumkosoa kwa hoja na kwa tafiti zilizothibitishwa kisayansi na wataalamu!
Kumnyamazisha wakati anatoa hoja kwa kile anachoamini ni kumwonea!
Hakuna hoja ya msingi anatoa. Hajatoa hoja yoyote ya kisayansi yenye ushahidi.

Mbaya zaidi anatuhumu watu kupewa pesa ili waruhusu chanjo. Awataje hao watu vinginevyo huu anaofanya ni uchochezi. Anatakiwa kushughulikiwa kwa mujibu wa taratibu za CCM na serikali. Hatuwezi kuwa na viongozi wa namna hii. Ndio,mbunge ni kiongozi. Unakuwaje na kiongozi ambaye qnapinga maamuzi ya serikali ya chama chake na kidhalilisha viongozi kwa tuhuma za kutunga?
 
Nadhani wa kuonea huruma ni wale ambao maamuzi yao ni ya kuambiwa na mtu na sio kutoka kwenye fikra zao..., Ukizingatia yule anayewaambia sio mtaalamu wa kile anachowaambia...
 
Hakuna hoja ya msingi anatoa. Hajatoa hoja yoyote ya kisayansi yenye ushahidi.

Mbaya zaidi anatuhumu watu kupewa pesa ili waruhusu chanjo. Awataje hao watu vinginevyo huu anaofanya ni uchochezi. Anatakiwa kushughulikiwa kwa mujibu wa taratibu za CCM na serikali. Hatuwezi kuwa na viongozi wa namna hii. Ndio,mbunge ni kiongozi. Unakuwaje na kiongozi ambaye qnapinga maamuzi ya serikali ya chama chake na kidhalilisha viongozi kwa tuhuma za kutunga?
Unajuaje? You never know huenda ana ushahidi wa kutosha kwa kile anachosema.
 
Aliyeanza kutugawa ni Samia ambaye amejifanya kama hakuwa kwenye serikali ya Magu. Lakini pia hao unaowaita wataalamu wetu hebu tupe uthibitisho ni lini na wapi walifanya utafiti na kuona hizo chanjo zipo salama?

Ziko wapi scientific research zao zinazonesha chanjo inayogusa DNA/RNA ipo salama? Kama walishindwa hata kutengeza case scenarios za kupima ubora wa vifaa vya kupimia corona hadi Mh. Magu akatumia janja yake na kukuta mapapai yana corona, je leo huo uwezo wa kupima ubora wa chanjo wameuotoa wapi?

Hizo chanjo wamezijaribisha kwenye nini na wakapata uhakika kuwa taifa lipo salama na kile wanachokipokea kutoka ulaya na marekani ni chanjo salama na siyo bio-wepon?
Its very sad yani. Africa sijui tutajiamini lini.
 
Tumechanjwa chanjo nyingi sembuse hii ya covid-19 acheni kutisha watu kwa kulishwa matango pori na huyo gwajizo
Rejea hapo kwenye kuhusisha DNA na RNA, sio issue ndogo. Matokeo yake yaweza kuwa vituko... yani tunakuwa genetically modified organism!!!!. Anyway watu hawana utu.
 
..Gwajima anadai kanisa lake lina waumini milioni 2.9. Huenda serikali na CCM wanamuogopa kwasababu hiyo.
Kanisa lenyewe kama banda langu la kufugia kuku
IMG_20201103_153332.jpg
 
Napenda kutoa Rai kwa Vyombo vya Ulinzi na usalama kumkamata mara moja Mh Gwajima, kumuhoji na kumshitaki kwa counts tatu za msingi.Sitaki kuzungumzi hotuba ya Mch Gwajima kanisani kwake juzi, kwani si jambo geni humu na litaunganisha uzi na nyuzi zingine kama hizo. Mods Nakimbilia moja kwa moja kwenye hoja kuu ya Uzi huu.

Kwa muelekeo wa kamati ya Mh. Samia na ushauri wake, na kwa maamuzi ya serikali kuhusu kuchanjwa. Sote tuna imani wataalamu wetu wa afya wameshirikishwa vya kutosha, pia tunaamini vyombo vyetu vya usalama nikimaanisha idara ya Usalama wa Taifa wameshafanya Upembuzi yakinifu na juu ya tuhuma hizi za chanjo ya Covid kuwa hatari kwa maisha yetu. Kwa hiyo mpaka chanjo inaingia maana yake "there is no doubt about it" . Lakin tunafahamu hata itakapoingia itachunguzwa pia na kuthibitishwa zaidi.

Kimantiki ninashauri Mch Gwajima afunguliwe kesi 3 za msingi ambazo ni Uchochezi, Uhaini na Ugaidi kwa jinsi nilivyojifunza muundo wa siasa zetu.

Shitaka la kwanza la uchochezi liko Clear kuwa ana"mislead " wananchi kwa kupotosha kitu ambacho hajafanyia utafiti kitaalamu maana alitakiwa aje na ripoti yake ya uchunguzi kitaalamu tungemuelewa. Gwajima ni mbunge na ni kiongozi wa kiroho hivyo ana ushawishi mkubwa sana. Inavyoonekana anatumia ushawishi wake kuwagawa watanzania, kuwafanya Raia kupinga maamuzi ya serikali, anaingilia masuala nyeti ya afya za watanzania. Hebu tujiulize ikitokea Bagonza akapinga Chanjo ya Surua, Bakwata wakapenga ya Pepopunda, Makamba akapinga ya Polio itakuwaje huko Mbele. Nauona huu ni uchochezi kabisa.


Kwanini afunguliwe kesi ya Uhaini, ni kwa sababu anaingilia Muenendo wa Rais, viongozi wakuu wa serikali na vyombo vya usalama vya nchi. Kwa kauli yake Gwajima anaamuru maaskari, makachero na maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama wasichanjwe huku akiwatishia kuwa watadhurika. Hii litawafanya wao kukwepa au kupinga amri hii na hapa Gwajima atakuwa "accessory after the fact" ya uhaini huu wa Askari wetu. Lingine ni kutuhakikishia kuwa Viongozi wakuu wa serikali akiwamo Rais watadhurika ama hata kufa baada ya kutumia Chanjo hii. Gwajima anapaswa kuhojiwa na kuiambia Serikali ametoa wapi taarifa hizi za Rais kudhurika kama akitumia hii chanjo. Itakapokuja kutokea isije ikaonekana alikuwa na maono ama vip. Iisje maadui zetu wakapata mwanya huohuo wa maneno ya Gwajima kumdhuru Rais wetu mpendwa.

La mwisho Gwajima napaswa kupewa kesi ya Ugaidi ama kuhusishwa na huu ugaidi ama kuwa shahidi wa muhimu wa njama za ugaidi anaousemea yeye against taifa letu. Gwajima anajua ama ana taarifa za watanzania Mamilioni kudhurika ama hatimaye kufa kwa matumizi ya dawa hizi. Anaaswa kukamatwa na kuhojiwa kwa habari hizi. Nevertheless kama si kweli kesi ya ugaidi inamuhusu. Huu ni ugaidi wa kifikra na mawazo ya watanzania ikiwemo kuwatia hofu "Terror -> Terrorism" .

Nitoe Rai jwa vyombo vya ulinzi na usalama kumchukulia hatua Askofu Gwajima, tuache yale ya watu kusema Mkuu fulani anaumwa, mkuu fulani atafariki na wakachekewa hatimaye inakuwa kweli then wanaitwa manabii.



Na pindi ikitokea hii chanjo kuna mtu amedhurika , Mtuhumiwa wa kwanza awe Gwajima. Ikitokea Covid ikatupiga zaid sababu ya kutochanjwa Gwajima anatakiwa ashitakiwe pia kwa kutufanya tupingane na WHO .

Kazi na iendelee!..
Haya maneno ya Gwajima ange yasema Sheikh Ponda, au Mch. Msigwa muda huu wange kuwa Segerea kwa kesi ya uhujumu uchumi. Kwa Ccm watatoleana matamko tuu.
 
Rejea hapo kwenye kuhusisha DNA na RNA, sio issue ndogo. Matokeo yake yaweza kuwa vituko... yani tunakuwa genetically modified organism!!!!. Anyway watu hawana utu.
Mpaka we na Gwaji mjue jinsi DNA na RNA zinavo fanya kazi mwilini
 
Back
Top Bottom