Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Baada ya kufanya bidii za maksudi kutaka kujua sakata hili la shambulizi la Mwenyekiti Wa Jumuia ya Madaktari TZ, Dr. Steve Ulimboka pamoja Na madai yaliyotolewa Jana Na Kamanda Kova kwamba Kuna Mtu anaedaiwa kuhusika Na utekaji Na shambulizi Hilo aliyejitokeza kujisalimisha ndani ya Kanisa linaloongozwa Mch Josephat Gwajima, pamoja Na utata uliosambaa juu ya matamshi hayo, nimebahatika hatimae kuongea na Mchungaji huyo..
Yeye mwenyewe Kwanza amekiri kusikia taarifa hizo Na pia maelfu ya watu miongoni mwao ni washirika NOa watu wengine nje ya Kanisa nao wamekuwa wakimtafuta ili kupata ukweli Wa matamshi hayo ya Polisi
Mchungaji huyo ambaye Kwa mtazamo ni mpole, mkimya Na mwenye maneno yaliyonyooka, akasema kwamba kuna taarifa aliletewa Na walinzi wa Kanisa kwamba kuna kijana mdogo tu alikuwa akidai yeye ndiye Kinara wa sakata Hilo la kumteka daktari huyo..Na walinzi Hao wakampeleka kituoni Na kumkabidhi huko.. Sasa cha Ajabu ni taarifa ya Jana ya jeshi la polisi juu ya uhusika wa tukio Hili..
Na yeye Kama kiongozi imemgharimu kuwaita Upya wale walinzi Na kupata kutoka kwao taarifa hiyo Na hatimae kesho kwenye Ibaada maalum ataelezea Mkasa wote ulivyokuwa ili jamii ielewe nini kilichojiri..
Nimepitia comment nyingi za watu humu kila Mtu akinadi Na kusema lake, wapo wanaotukana Na wapo wanalalamika Kwa namna wajuao.. Labda nitoe rai kwamba ni vema tuwe Na subira Na kupata Picha kamili hiyo kesho..
Mimi mwenyewe nitawahi mapema Na Kama kawaida ya TAMKO nitawajuza kila kitu..matusi kejeli si mahali pake nadhani kuna kamchezo kanaendelea ambako lazima kafichuliwe sasa.. Jambo Hili si Dogo linagusa masikio ya mataifa mengi Kwa sasa..
..
..
Kabla ya kesho Gwajima atakuwa ameulimbokiwa!!!