Mchungaji Getrude Rwakatare amrithi marehemu Salome Mbatia

Kithuku

JF-Expert Member
Nov 19, 2006
1,395
207
Na Said Mwishehe

MCHUNGAJI Dkt. Getrude Rwakatare, ameteuliwa kuwa Mbunge wa Viti Maalumu kupitia CCM kuziba pengo la aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bibi Salome Mbatia, aliyekufa kwenye ajali ya gari.

Taarifa zilizopatikana jana jioni Dar es Salaam kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) zilithibitisha kuteuliwa kwa Mchungaji Rwakatare.

Akizungumza na Majira, mmoja wa maofisa wa NEC, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema Mchungaji Rwakatare aliteuliwa kushika wadhifa huo na tayari chama chake kimefahamishwa kuhusiana na uteuzi huo.

"Tumeshaandika barua kwa CCM kuwafahamisha uteuzi wa Mchungaji huyo kushika wadhifa huo. Hivyo kisheria NEC haina ulazima wa kutangaza jina lake kwa wananchi, bali chama chake ndicho kinaweza kufanya hivyo, baada ya kuwapa barua," alisema ofisa huyo.

Naye Ofisa Habari wa NEC, Bw. Bathlomew Wandi, alipoulizwa kuhusiana na uteuzi huo, alisema ni kweli Mchungaji Rwakatare, ameteuliwa na tayari barua ya kukitaarifu chama chake imeshakwenda.

"Taarifa nilizonazo ni kwamba tayari CCM wameandikiwa barua ya uteuzi huo, lakini ni vema mkapata maelezo zaidi kutoka kwa viongozi wa CCM kwani ndio wenye jukumu la kumtangaza mtu wao, kutokana na kuchaguliwa kwake," alisema Bw. Wandi.

Mwaka 2005, Dkt. Rwakatare aliingia katika kinyang'anyiro cha kupata nafasi hiyo kupitia mkoa wa Morogoro, lakini alishindwa; na sasa ameingia kwa utaratibu wa mlolongo wa nafasi walizopata mwaka huo.

Kuingia kwa Mchungaji huyo bungeni kwa tiketi ya CCM kunafanana na jinsi alivyoingia Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dkt. Christine Ishengoma, ambaye naye aliteuliwa kushika nafasi hiyo, baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa viti maalumu kupitia Jumuiya ya Vijana wa CCM, marehemu Amina Chifupa.

Kutokana na uteuzi huo, Dkt. Rwakatare anatarajiwa kuapishwa katika Mkutano wa 10 wa Bunge unaotarajiwa kufanyika Dodoma kuanzia Januari 29 mwakani.


Dkt. Rwakatare ambaye ni Mchungaji wa Kanisa na Assemblies of God Mikocheni, anamiliki shule na vyuo vya St. Mary's na kituo cha redio cha Praise Power Radio.

Source: Majira.

Kumbe akifa mtu anateuliwa aliyefuata kwa kura uchaguzi uliopita? Hivi wadau sheria ndivyo inavyosema au huu ni utaratibu wa CCM? Kwa mtaji huu wale katika viti maalumu wanaoamini "vipapai" watavisaka kwa udi na uvumba!
 
Huyu hivi kateuliwa na Rais pia au?
Huwa nina wasiwasi na huyu mama kujiita mchungaji. Sina uhakika kama ni wale wanaokula kuku kw mrija kuptia migongo ya mashirika ya dini maana nimejua huyu mama ana pesa kuliko serikali. Sasa sijui naye atahojiwa alizipaje.....kesho twaweza kusikia kuwa ndio pia amekuwa naibu wa waziri wa marehemu Mbatia. Naomba wajomba mfanyie uchunguzi wa background yake.
 
:confused: Mmmh! Mi yangu macho, maana data nilizosikia kuhusu huyu mama zilinishtua sana, tatizo sijui kama ni kweli au ni uzushi! Kama mtu ana data za uhakika atueleze zaidi, lakini kulikuwa na minong'ono kwamba alikuwa kwenye list mojawapo!
 
Sasa sijui uchungaji atauacha? maana uchungaji ni kazi ya ki utume!

I am confused!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
 
Kama Angekuwa Anaacha Uchungaji, Basi Angeshafanya Hivyo Zamani Wakati Anagombea Kiti Hicho Kupitia Viti Maalum, Ambapo Sasa Kakilamba Bwererere..cheche..

Dini Ni Deal, Mishule Na Miradi Mingi Ya Huyu Mama Inatisha Kuamini Kuwa Ni Muumini Wa Mungu, Na Kama Ni Hivyo Kwenye Siasa Anatafuta Nini????? Watanzania Tunaatiwa Pilipili Mdomoni Na Tunalazimishwa Kuila Wakati Tuna Uhuru Wa Kukataa Kuila Kwani Tunajua Wazi Kwamba Ni Chungu.
 
Jamani kelele za nini leo? Hizi hadithi kama zina mantiki zilipaswa kutoka siku nyingi tangu amegombea siyo mpaka mtu apate ndo yaibuke.

Dini ni kwa ajili ya watu kama ilivyo siasa kwa ajili ya watu.
Mbona Papa ni Raisi wa Vatican? Ndiyo si anaongoza serikali inayotambulika duniani, mpaka ana mabalozi?
 
Kumbe akifa mtu anateuliwa aliyefuata kwa kura uchaguzi uliopita? Hivi wadau sheria ndivyo inavyosema au huu ni utaratibu wa CCM? Kwa mtaji huu wale katika viti maalumu wanaoamini "vipapai" watavisaka kwa udi na uvumba!

Ndiyo manake,
Hii ni kwa kesi ya viti maalum tu na siyo vya majimboni.

Kama ni kwenye jimbo Process zinaanza upya huwezi kuwekwa eti kisa ulizidiwa kura kidogo.
 
hata mimi nina dukuduku ya kujua kulikoni na huyu mama maana yanayoongelewa juu yake yanatisha sana. ebu tuendelee kusikiliza data toka kwa wengine. ila ya mMungu tunampa Mungu na ya kaisari tunampa kaizari.
 
huwezi kutumikia mabwana wawili...HAKUJIFUNZA KWA YALIYOMKUTA KAKOBE KUKIMBIWA NA WAUMINI ALIVYOJIUNGA NA SIASA ...

NDIO MAANA MAKANISA NA BAADHI YA DINI NYINGINE HAYARUHUSU WATUMISHI WAO KUJIUNGA NA ACTIVE PILITICS
 
Pamoja na yote itabidi kazi ya uchungaji wa kondoo wa BWANA aiache ili awe ndani ya siasa maana hivyo vitu haviendi pamoja.
Hebu angalieni hii,jukwaani kama mbunge atahimiza vijana matumizi ya kondom kujikinga na ukimwi kama sera za chama chake zinavyosema. Lakini msimamo wake madhabahuni utakuwa tofauti kabisa,je ataeleweka? labda uwe na malengo tofauti katika kuwania kwake ubunge,vinginevyo aache kimoja.
 
Hongera mama Rwakatare. Hayo ya siasa na kanisa, wanajua waumini wake. Kama walimruhusu agombee ina maana wanaona sawa.

Kuhusu mambo mabaya ya huyu mama, leteni data zake vinginevyo mimi miaka na miaka kila Mtanzania aliyefanikiwa kunakuwa na maneno ya chini chini. Huabaki najiuliza ni kwanini? Ni wivu? Au ni kwamba ili ufanikiwe Tanzania ni lazima humo njiani utatenda maovu mengi.

Binafsi sina jibu, lakini mimi ningependa tuanze kuwasifu Watanzania wenzetu wanaofanikiwa through kazi.

Kwa mazingira ya TZ huenda ni ngumu sana kuwa clean 100%.
 
Kuna mwimbaji mmoja wa injili aliwahi kuimba "DINI NA SIASA NI KAMA MAFUTA NA MAJI" Nisaidien jamani wanaa jambo haya mabo yanakuwaje, I'm wondering...!

Na huku kuteuliwa inakuwaje,wanatumia vigezo gani kumteua mtu, please wana sisiem naomba mnisaidie

Kweli aliyenacho huongezewa,asiyenacho hunyanganywa kabisaaa..
 
Kujiunga kwa Dr. Lwakatare kwenye siasa tena sisiem, na sasa ubunge.mmmh Yesu aliwafananisha wanasiasa na mbwa mwitu sio maneno yangu ila fuatilia maneno ya Huyu pastor kuhusu sisiem na siasa.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=G0dqLxJ1TzI[/ame]
 
Inasemekana huyu mama ni mshirika mkubwa katika biashara ya mihadarati. Haya kazi kwenu.
 
Inasemekana huyu mama ni mshirika mkubwa katika biashara ya mihadarati. Haya kazi kwenu.

Mmmhhhhh!!!! mimi sijui.

NInachojua mimi huyu mama katuamsha Watanzania kwenye mambo ya shule. Ule ujinga wa kupeleka watoto wadogo Kenya na Uganda sasa umeisha.

Kwa sehemu kubwa huyu mama kachangia kwa kuanzisha shule zake ambazo zina quality ya kutosha. Katoa ajira kwa Watanzania na si ajabu analipa kodi ya kutosha. Hivyo ndivyo vichwa tunavyotaka Tanzania na wala sio wale wajinga waliojaa kila sehemu Tanzania wanaokumbatia wageni kwa cost ya Watanzania.

Mimi ninamsifu kwa hilo maana nina uhakika nalo, sina uhakika na hayo ya madawa ya kulevya.
 
Kuna mwimbaji mmoja wa injili aliwahi kuimba "DINI NA SIASA NI KAMA MAFUTA NA MAJI" Nisaidien jamani wanaa jambo haya mabo yanakuwaje, I'm wondering...!

Na huku kuteuliwa inakuwaje,wanatumia vigezo gani kumteua mtu, please wana sisiem naomba mnisaidie

Kweli aliyenacho huongezewa,asiyenacho hunyanganywa kabisaaa..

Huyo aliyeimba hayo anaitwa Faustin Munishi. Nadhani sihitaji kuendelea kueleza mambo yake, kwani wengi kwenye forum hii wanaelewa kuwa huyu jamaa sasa hivi yuko kwenye siasa chafu sana zinazofanana sana na wendawazimu hasa. Ni wanafiki tu hawa jamaa. Au pengine background zao, tabia walizokuwa nazo kabla hawajaanza usanii wa kutangaza "wameokoka" na kujipachika "uchungaji" na "uaskofu", tabia hizo zinawarudia upya njaa inapoisha! Wataalamu wa saikolojia, najua wako wengi kwenye hii forum, wanaweza kutueleza nadharia hizi kama zipo. Yaani aliyekuwa tapeli, malaya, teja nk mambo yakamwendea mrama huko, anapojisalimisha kanisani kutafuta faraja, akiipata bora asipate zaidi ya hiyo faraja, kwani akipata fedha na umaarufu mambo yake yote ya zamani anayarudia kwa kasi. Tumeyaona haya kwa Munishi, Rose Muhando, na wengine. Sina ushahidi wowote dhidi ya Mama Lwakatare, sijui aliingiaje kwenye fani hiyo ya uchungaji, ambapo ya kwake inaendana na ujasiriamali na siasa kwa pamoja. Hata hivyo, historia imeshatufundisha kuwa na mashaka na watu wa aina hii, kwa hiyo ana kazi kubwa ya kutuondolea mashaka haya.

Kuna wakati najiuliza, hivi wale binadamu wenye nia na imani ya dhati kabisa kwa Mungu, kimbilio lao liko wapi? Maana viongozi wa dini mambo yao hata hayafai kusema. Yanatisha yaani. Pengine sasa ni ule wakati wa kila mtu kusimama kivyake na Mungu wake akisubiria hukumu yake bila kutegemea mafundisho kutoka kwa mtu yeyote. Makanisa yatabaki kama social gatherings tu ambako watu wanaenda kusalimiana na kusikiliza kwaya, kama huku Ulaya. Kanisa ninalohudhuria hapa kuna zamu za kuandaa kahawa kwa ajili ya wanaohudhuria misa jumapili. Na wakati wa kutoka, mlangoni tunagawiwa vipeperushi vinavyotangaza jinsi ya kuwapata "singles" wanaosali hapo. Huyo aliyebuni mradi huo naona amefanikiwa, maana ni miongoni mwa makanisa machache yenye misa 3 zinazojaa watu!

Sijui bwana!
 
Huyo aliyeimba hayo anaitwa Faustin Munishi. Nadhani sihitaji kuendelea kueleza mambo yake, kwani wengi kwenye forum hii wanaelewa kuwa huyu jamaa sasa hivi yuko kwenye siasa chafu sana zinazofanana sana na wendawazimu hasa. Ni wanafiki tu hawa jamaa. Au pengine background zao, tabia walizokuwa nazo kabla hawajaanza usanii wa kutangaza "wameokoka" na kujipachika "uchungaji" na "uaskofu", tabia hizo zinawarudia upya njaa inapoisha! Wataalamu wa saikolojia, najua wako wengi kwenye hii forum, wanaweza kutueleza nadharia hizi kama zipo. Yaani aliyekuwa tapeli, malaya, teja nk mambo yakamwendea mrama huko, anapojisalimisha kanisani kutafuta faraja, akiipata bora asipate zaidi ya hiyo faraja, kwani akipata fedha na umaarufu mambo yake yote ya zamani anayarudia kwa kasi. Tumeyaona haya kwa Munishi, Rose Muhando, na wengine. Sina ushahidi wowote dhidi ya Mama Lwakatare, sijui aliingiaje kwenye fani hiyo ya uchungaji, ambapo ya kwake inaendana na ujasiriamali na siasa kwa pamoja. Hata hivyo, historia imeshatufundisha kuwa na mashaka na watu wa aina hii, kwa hiyo ana kazi kubwa ya kutuondolea mashaka haya.

Kuna wakati najiuliza, hivi wale binadamu wenye nia na imani ya dhati kabisa kwa Mungu, kimbilio lao liko wapi? Maana viongozi wa dini mambo yao hata hayafai kusema. Yanatisha yaani. Pengine sasa ni ule wakati wa kila mtu kusimama kivyake na Mungu wake akisubiria hukumu yake bila kutegemea mafundisho kutoka kwa mtu yeyote. Makanisa yatabaki kama social gatherings tu ambako watu wanaenda kusalimiana na kusikiliza kwaya, kama huku Ulaya. Kanisa ninalohudhuria hapa kuna zamu za kuandaa kahawa kwa ajili ya wanaohudhuria misa jumapili. Na wakati wa kutoka, mlangoni tunagawiwa vipeperushi vinavyotangaza jinsi ya kuwapata "singles" wanaosali hapo. Huyo aliyebuni mradi huo naona amefanikiwa, maana ni miongoni mwa makanisa machache yenye misa 3 zinazojaa watu!

Sijui bwana!

Mkuu, fuata wanachokuhubiria, usichungulie wao wanafanya nini.
 
Mmmhhhhh!!!! mimi sijui.
NInachojua mimi huyu mama katuamsha Watanzania kwenye mambo ya shule. Ule ujinga wa kupeleka watoto wadogo Kenya na Uganda sasa
umeisha kwasehemu kubwa huyu mama kachangia kwa kuanzisha shule zake ambazo zina quality ya kutosha. Katoa ajira kwa Watanzania na si ajabu analipa kodi ya kutosha. Hivyo ndivyo vichwa tunavyotaka Tanzania na wala sio wale wajinga waliojaa kila sehemu Tanzania wanaokumbatia wageni kwa cost ya Watanzania.

Mimi ninamsifu kwa hilo maana nina uhakika nalo, sina uhakika na hayo ya madawa ya kulevya.

Yaa, ni kweli mtanzania huwezi kusikia vitu kama hivyo. Hiyo ni biashara yenye siri kubwa sana. Ukistaajabu ya mussa utaona ya firauni.
 
Kujiunga kwa Dr. Lwakatare kwenye siasa tena sisiem, na sasa ubunge.mmmh Yesu aliwafananisha wanasiasa na mbwa mwitu sio maneno yangu ila fuatilia maneno ya Huyu pastor kuhusu sisiem na siasa.

http://www.youtube.com/watch?v=G0dqLxJ1TzI

Anaimba vizuri, (yaani uzuri wa sauti na kupiga vyombo), lakini naona sasa amechanganyikiwa. Simwelewi anaposema kama waislamu wa Zanzibar wamechoka na CCM waachwe waiondoe, je anasemaje kuhusu wa dini nyingine?

Kama wakristo wa bara wamechoka na CCM lakini waislamu hawajachoka nayo, anasemaje? Au kinyume chake, waislamu wa bara wamechoka na CCM lakini wakristo hawajachoka nayo, itakuwaje? Si ndio udini huu jamani? Huku ni kugawanya watu kwa misingi ya udini, ameangalia akaona Zanzibar waislamu ni wengi, kwa hiyo akitumia neno hilo atapata ufuasi.

Huko Zanzibar kama kuna kinachowachosha watu, kimewachosha wote bila kujali dini zao, hata bara pia ndio maana vyama vya upinzani vina wanachama wakristo, waislamu na wengine. Na isitoshe wanaotawala wanawakilisha composition ya umma, bara kuna waislamu na wakristo kwenye uongozi wa ngazi zote, na Zanzibar kuna waislamu wengi zaidi kwenye uongozi kuliko dini nyingine kwa sababu population yao ndivyo ilivyo. Huyu mtu ni balaa.

Mtu wa namna hii ni hatari sana, kwa sababu baadae ataanza kuangalia tena ni watu wa kabila gani walio wengi, ataanza kusema "wanyamwezi wamechoka na chama fulani", "watanganyika WEUSI wamechoka na chama fulani" nk! Mwangalie kwanza, hata aibu hana!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom