Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Nimeiona hii kwenye gazeti la Tanzania Daima nikaona niwamwagie kwenye jamvi tuijadili .....hivi imekaaje vile.......................
Mchungaji: Kupanga uzazi ni kumkosea Mungu
na Danson Kaijage, Dodoma
MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelistic Asembless of God (EAGT) James Ibrahimu maarufu kwa jina la Majembe Makali amewataka Watanzania kuacha dhana potofu ya uzazi wa mpango inayohamasishwa na taasisi mbalimbali na serikali.
Akiwahubiria waumini wa kanisa hilo wakati wa ibada iliyofanyika kwenye kanisa la EAGT Siloam Ipagala, Dodoma mjini, alidai kitendo cha uzazi wa mpango ni kufuru mbele za Mungu.
Mchungaji Majembe Makali alisema pamoja na taasisi mbalimbali na serikali kuhamasisha aina hiyo ya uzazi ni tendo la aibu ndani ya nchi na jambo linaweza kusababisha laana kwa taifa.
Akihubiri kanisani hapo alisema inasikitisha kuona watu wanajiita walokole nao wanaingia katika mkumbo huo aliouita wa kishetani wa kutumia vidonge vya majira huku akifafanua kwamba uzazi wa mpango unatakiwa kufuatwa na wasiomwamini Mungu kwa maelezo kuwa ni mpango kutoka kuzimu.
Mchungaji huyo alikwenda mbali zaidi akidai kuwa mpango huo ni dalili za mtu kushindwa maisha kwa visingizio mbalimbali na kubainisha kuwa wote wanaofunga kizazi wanamkosea Mungu na kwa mtaji huo wanatakiwa kutubu kwa kumwekea Mungu mipaka ya uumbaji wake.
Kanisa la EAGT linapinga uzazi wa mpango na hata Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Dk. Moses Kulola huwahimiza washirika wake kuacha matumizi ya vidonge vya majira na njia zote za uzazi wa mpango.
Mchungaji: Kupanga uzazi ni kumkosea Mungu
na Danson Kaijage, Dodoma
Akiwahubiria waumini wa kanisa hilo wakati wa ibada iliyofanyika kwenye kanisa la EAGT Siloam Ipagala, Dodoma mjini, alidai kitendo cha uzazi wa mpango ni kufuru mbele za Mungu.
Mchungaji Majembe Makali alisema pamoja na taasisi mbalimbali na serikali kuhamasisha aina hiyo ya uzazi ni tendo la aibu ndani ya nchi na jambo linaweza kusababisha laana kwa taifa.
Akihubiri kanisani hapo alisema inasikitisha kuona watu wanajiita walokole nao wanaingia katika mkumbo huo aliouita wa kishetani wa kutumia vidonge vya majira huku akifafanua kwamba uzazi wa mpango unatakiwa kufuatwa na wasiomwamini Mungu kwa maelezo kuwa ni mpango kutoka kuzimu.
Mchungaji huyo alikwenda mbali zaidi akidai kuwa mpango huo ni dalili za mtu kushindwa maisha kwa visingizio mbalimbali na kubainisha kuwa wote wanaofunga kizazi wanamkosea Mungu na kwa mtaji huo wanatakiwa kutubu kwa kumwekea Mungu mipaka ya uumbaji wake.
Kanisa la EAGT linapinga uzazi wa mpango na hata Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Dk. Moses Kulola huwahimiza washirika wake kuacha matumizi ya vidonge vya majira na njia zote za uzazi wa mpango.