Mchumi ashauri fedha zilizoibwa BoT zirejeshwe na riba

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Kuna haja ya kumuuliza JK, huu utamaduni wa mafisadi waliokupua mabilioni ya mapesa ya walipa kodi na hatimaye kuzirudisha pesa hizo huku wakiendelea kuwa huru umetoka wapi!? Kwa nini wasirudishe mapesa hayo huku wakiwa lupango wakisubiri kufikishwa mahakamani?

Posted Date::3/1/2008
Mchumi ashauri fedha zilizoibwa BoT zirejeshwe na riba
Na Ally Sonda,Moshi
Mwananchi

WAKATI watuhumiwa wa ufisadi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakidaiwa kurejesha serikalini zaidi ya Sh50 bilioni za EPA, mfanyabishara maarufu wa mjini Moshi, Patrick Boisafi amesema lazima fedha hizo zinazorejeshwa zilipiwe riba.

Boisafi ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Kilimanjaro,amesema pamoja na kwamba serikali haijasema wazi kuwa mafisadi hao walizichukuaje fedha hizo kutoka BoT na hivyo kuamua kuzirejesha baada ya mchezo mchafu kubainika ni lazima watozwe riba ili thamani ya fedha iliyochotwa isipotee

Mwenyekiti huyo ambaye kitaaluma ni mchumi amesema thamani ya fedha inabadilika kila dakika na kwamba watuhumiwa walichukua fedha hizo muda mrefu uliopita wakiwa wanazitumia kwenye biashara zao na hivyo kuzalisha faidi kubwa.

"Nimesikia waliochota mabilioni BoT wameanza kurejesha fedha hizo, mimi sipingi huo urejeshaji, bali ninachotaka kieleweke ni kwamba fedha hizo wamekuwa nazo kwa muda mrefu,wamezalisha hivyo ni lazima wawekewe riba walipe," alisema Boisafi.

Vilevile, Boisafi amemwomba,Waziri wa Fedha na Mipango, Mustafa Mkulo, kuwataja hadharani mafisadi waliorejesha fedha hizo ili waeleweke kwa jamii ambayo alidai inaweza kufichua mali zilizofichwa na mafisadi hao.

"Sioni mantiki yoyote ya kuficha majina ya hao watuhumiwa, namwomba Waziri wa Fedha na Mipango, awataje hadharani wahusika, inawezekana ni watu tunawafahamu pamoja na mali anazomiki tukiwajua tutasaidia uchunguzi zaidi," alisema.

Alisema fedha za EPA ambazo ni zaidi ya Sh133m bilioni ni nyingi sana na hivyo si vema zikarejeshwa bila kuongezewa riba na wahusika.
 
Kuna haja ya kumuuliza JK, huu utamaduni wa mafisadi waliokupua mabilioni ya mapesa ya walipa kodi na hatimaye kuzirudisha pesa hizo huku wakiendelea kuwa huru umetoka wapi!? Kwa nini wasirudishe mapesa hayo huku wakiwa lupango wakisubiri kufikishwa mahakamani?

Posted Date::3/1/2008
Mchumi ashauri fedha zilizoibwa BoT zirejeshwe na riba
Na Ally Sonda,Moshi
Mwananchi

WAKATI watuhumiwa wa ufisadi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakidaiwa kurejesha serikalini zaidi ya Sh50 bilioni za EPA, mfanyabishara maarufu wa mjini Moshi, Patrick Boisafi amesema lazima fedha hizo zinazorejeshwa zilipiwe riba.

Boisafi ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Kilimanjaro,amesema pamoja na kwamba serikali haijasema wazi kuwa mafisadi hao walizichukuaje fedha hizo kutoka BoT na hivyo kuamua kuzirejesha baada ya mchezo mchafu kubainika ni lazima watozwe riba ili thamani ya fedha iliyochotwa isipotee

Mwenyekiti huyo ambaye kitaaluma ni mchumi amesema thamani ya fedha inabadilika kila dakika na kwamba watuhumiwa walichukua fedha hizo muda mrefu uliopita wakiwa wanazitumia kwenye biashara zao na hivyo kuzalisha faidi kubwa.

"Nimesikia waliochota mabilioni BoT wameanza kurejesha fedha hizo, mimi sipingi huo urejeshaji, bali ninachotaka kieleweke ni kwamba fedha hizo wamekuwa nazo kwa muda mrefu,wamezalisha hivyo ni lazima wawekewe riba walipe," alisema Boisafi.

Vilevile, Boisafi amemwomba,Waziri wa Fedha na Mipango, Mustafa Mkulo, kuwataja hadharani mafisadi waliorejesha fedha hizo ili waeleweke kwa jamii ambayo alidai inaweza kufichua mali zilizofichwa na mafisadi hao.

"Sioni mantiki yoyote ya kuficha majina ya hao watuhumiwa, namwomba Waziri wa Fedha na Mipango, awataje hadharani wahusika, inawezekana ni watu tunawafahamu pamoja na mali anazomiki�tukiwajua tutasaidia uchunguzi zaidi," alisema.

Alisema fedha za EPA ambazo ni zaidi ya Sh133m bilioni ni nyingi sana na hivyo si vema zikarejeshwa bila kuongezewa riba na wahusika.

That is very true hata mtu ambaye si mchumi anaweza kukwambia hii kitu. Kikawaida ukipewa pesa na benki lazima urudishe na RIBA. Na kwa hawa wezi sio riba tu bali wafike kwa pilato, hii itakuwa fundisho kwa watu wengine wanaopnda maisha mazuri na ya kulingishia wengine kwa kutumia pesa za wizi na ulaghai.
 
Hao walioiba hayo mapesa ni wateule, na ikiwa mteule huwezi kuwa treated kama wanavyokuwa treated wezi wengine. Wateule hapa bongo wanaundiwa TUME na kama wewe sio basi wanaku-MAHALU au wanaku-KIULA.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom