BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,167
Kuna haja ya kumuuliza JK, huu utamaduni wa mafisadi waliokupua mabilioni ya mapesa ya walipa kodi na hatimaye kuzirudisha pesa hizo huku wakiendelea kuwa huru umetoka wapi!? Kwa nini wasirudishe mapesa hayo huku wakiwa lupango wakisubiri kufikishwa mahakamani?
Posted Date::3/1/2008
Mchumi ashauri fedha zilizoibwa BoT zirejeshwe na riba
Na Ally Sonda,Moshi
Mwananchi
WAKATI watuhumiwa wa ufisadi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakidaiwa kurejesha serikalini zaidi ya Sh50 bilioni za EPA, mfanyabishara maarufu wa mjini Moshi, Patrick Boisafi amesema lazima fedha hizo zinazorejeshwa zilipiwe riba.
Boisafi ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Kilimanjaro,amesema pamoja na kwamba serikali haijasema wazi kuwa mafisadi hao walizichukuaje fedha hizo kutoka BoT na hivyo kuamua kuzirejesha baada ya mchezo mchafu kubainika ni lazima watozwe riba ili thamani ya fedha iliyochotwa isipotee
Mwenyekiti huyo ambaye kitaaluma ni mchumi amesema thamani ya fedha inabadilika kila dakika na kwamba watuhumiwa walichukua fedha hizo muda mrefu uliopita wakiwa wanazitumia kwenye biashara zao na hivyo kuzalisha faidi kubwa.
"Nimesikia waliochota mabilioni BoT wameanza kurejesha fedha hizo, mimi sipingi huo urejeshaji, bali ninachotaka kieleweke ni kwamba fedha hizo wamekuwa nazo kwa muda mrefu,wamezalisha hivyo ni lazima wawekewe riba walipe," alisema Boisafi.
Vilevile, Boisafi amemwomba,Waziri wa Fedha na Mipango, Mustafa Mkulo, kuwataja hadharani mafisadi waliorejesha fedha hizo ili waeleweke kwa jamii ambayo alidai inaweza kufichua mali zilizofichwa na mafisadi hao.
"Sioni mantiki yoyote ya kuficha majina ya hao watuhumiwa, namwomba Waziri wa Fedha na Mipango, awataje hadharani wahusika, inawezekana ni watu tunawafahamu pamoja na mali anazomiki tukiwajua tutasaidia uchunguzi zaidi," alisema.
Alisema fedha za EPA ambazo ni zaidi ya Sh133m bilioni ni nyingi sana na hivyo si vema zikarejeshwa bila kuongezewa riba na wahusika.
Posted Date::3/1/2008
Mchumi ashauri fedha zilizoibwa BoT zirejeshwe na riba
Na Ally Sonda,Moshi
Mwananchi
WAKATI watuhumiwa wa ufisadi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wakidaiwa kurejesha serikalini zaidi ya Sh50 bilioni za EPA, mfanyabishara maarufu wa mjini Moshi, Patrick Boisafi amesema lazima fedha hizo zinazorejeshwa zilipiwe riba.
Boisafi ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Kilimanjaro,amesema pamoja na kwamba serikali haijasema wazi kuwa mafisadi hao walizichukuaje fedha hizo kutoka BoT na hivyo kuamua kuzirejesha baada ya mchezo mchafu kubainika ni lazima watozwe riba ili thamani ya fedha iliyochotwa isipotee
Mwenyekiti huyo ambaye kitaaluma ni mchumi amesema thamani ya fedha inabadilika kila dakika na kwamba watuhumiwa walichukua fedha hizo muda mrefu uliopita wakiwa wanazitumia kwenye biashara zao na hivyo kuzalisha faidi kubwa.
"Nimesikia waliochota mabilioni BoT wameanza kurejesha fedha hizo, mimi sipingi huo urejeshaji, bali ninachotaka kieleweke ni kwamba fedha hizo wamekuwa nazo kwa muda mrefu,wamezalisha hivyo ni lazima wawekewe riba walipe," alisema Boisafi.
Vilevile, Boisafi amemwomba,Waziri wa Fedha na Mipango, Mustafa Mkulo, kuwataja hadharani mafisadi waliorejesha fedha hizo ili waeleweke kwa jamii ambayo alidai inaweza kufichua mali zilizofichwa na mafisadi hao.
"Sioni mantiki yoyote ya kuficha majina ya hao watuhumiwa, namwomba Waziri wa Fedha na Mipango, awataje hadharani wahusika, inawezekana ni watu tunawafahamu pamoja na mali anazomiki tukiwajua tutasaidia uchunguzi zaidi," alisema.
Alisema fedha za EPA ambazo ni zaidi ya Sh133m bilioni ni nyingi sana na hivyo si vema zikarejeshwa bila kuongezewa riba na wahusika.