Mchumba wangu kanisaliti!! Niko kwenye maumivu makali naombeni ushauri

Samahani ndugu yangu kama nitakosea utaniambia.
Nimekusomasoma hata kwenye thread nyingine kuhusu Kuwashambulia wanaopata shida na kuhitaji msaada wetu na unatumia Eti kitunguu Swaumu kimekolea Mara unakuwa mtaalam wa lugha bila kujali maumivu ya mhusika.
Umeelewa mada why usijikite kushauri au ukapita kimya.Unaona fahari gani kumuongezea maumivu MTU ambaye wala hajasema baya lolote.
Nakusihi sana naomba uwe mwelewa na muungwana
Usitafute sifa kwenye maumivu ya watu .
Au kama mada zinakukera bora ukapita kimya.
Aksante.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu akubariki sanaaa ndugu yangu kutumia fursa hii kuelimisha wengine, suo kila jambo linalomkuta mwenzio ulichukulie Negatively kimzaha mzaha, kuujua udhaifu wa mwenzako haukufanyi wewe kuwa mkamilifu. STAY BLESSED

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana Dogo, mapenzi ndivyo yalivyo hivo. Kama unampenda msamehe na mtoe huko aliko mlete karibu uishi nae mpaka hasira na maumivu yatakapokwisha. Kumbukuka "Kosa moja haliachi mke"

Hata ukiwa nae karibu naomba usipende kumkaguakagua sana wala kutaka kujua mambo mengi maana "Ukimchunguza sana bata humli"

Unatakiwa kuishi na mwanamke kwa akili sana, ni wadhaifu sana hawa. Kitendo cha mwanamke kuishi mbali na wewe lazima agongwe kwasababu ww ni " Fimbo ya mbali haiui nyoka"

Huyo mchumba wako ni lakuvunda halina ubani. ila kama ukijitahidi kumweka karibu vizur basi hakiki unamtimizia mahitaji yake ya kimwili na kifedha yaani "penye udhia penyeza rupia"

Ila ukimuacha na kuamua aende basi yule dogo mwenye miaka 24 mtoto wa mwenye nyumba yeye ataona kapata na ataendelea kujisitili maana "ganda la mua la jana chungu kaona kivuli"

ila kingine wewe ni mwanaume shababi, usiwe nyoronyoro pambana maana ungekuwa mjanja wa mademu la usingelialia. si unajua "Mgaaga na upwa hali wali mkavu" eeee

na kama hutaki kabisa kuonana nae tena jikaze kiume tafuta demu mwingine na ishi nae kwa akili na kumbuka busara zangu. na usimkumbuke kabisa wa zamani ww deal na huyo mpya utaempata maana "Mla mla leo mla jana kala nini"


Sent using Jamii Forums mobile app
Shukurani Sir, nimekupata vizuri bro wangu, alot of blessings to u

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nikupe pole sana na katika mapenzi hayo yapo katika kujifunza. Luck enough umejua before hujaoa.

Ushauri wangu kung'uta mavumbi songa mbele no need to come back even if u fall in love at the maximum. Lakini pia ukiweza badili namba ya simu au block namba yake. Kiujumla mpotezee kabisa. Kuna wanawake wengi wenye hitaji la kuolewa na wametulia.

Mi nilipitia kwenye tatizo kama lako ila sikuumia sana na mwisho wa siku niwaendea wazazi wake nikawambia ukweli na nikawambia huwa sirudii matapishi nikasonga mbele kiume.

Remember mwanaume ni Lulu isiyoisha thamani yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sanaa MrRegion, nalifanyia kazi shauri lako, thanks

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Broo unaroho mbaya sana aisee kumbuka ajamuowa ameshafanya ivyoo siku jamaa akiamuowa alafu akaamishwa kikazi na demu akiwa amebaki aliposaivi na ana kazi atafanyaje. Mtu ambaye si mwaminifu ata umvute karibu yako atakuliza tu.

Kisa kidogo rafiki yangu alikuwa na demu wake na walizaa kabisa sababu ya kazi walikuwa wanakaa mbali wilaya tofauti baada ya mda kidogo jamaa alisikia mkewe anatiwa na bodaboda na boss wake pia alipita jamaa akafanya uchunguzi kweli akambamba alipiga sana ila bdaye alimuamisha wakaa wilaya moja na ndoa wakafunga aisee yaliyofata ni hadithi maana mwanamke alikuwa anatoka apoapo nyumbani ikafikia akawa anatoka na boss wake tena. Jamaa akaamishwa kikazi mwanamke ndyo ikawa analeta hadi nyumbani . Ile ndoa haikudumi ilikaa miaka mi3 tu ikavunjika ila mwanaume alipata hasara maana waligawana viwanja walikuwa washanunua vitatu na gari likauzwa saivi anaanza upya kujipanga kwaiyo awe makini na hawa viumbe
Pole sana Dogo, mapenzi ndivyo yalivyo hivo. Kama unampenda msamehe na mtoe huko aliko mlete karibu uishi nae mpaka hasira na maumivu yatakapokwisha. Kumbukuka "Kosa moja haliachi mke"

Hata ukiwa nae karibu naomba usipende kumkaguakagua sana wala kutaka kujua mambo mengi maana "Ukimchunguza sana bata humli"

Unatakiwa kuishi na mwanamke kwa akili sana, ni wadhaifu sana hawa. Kitendo cha mwanamke kuishi mbali na wewe lazima agongwe kwasababu ww ni " Fimbo ya mbali haiui nyoka"

Huyo mchumba wako ni lakuvunda halina ubani. ila kama ukijitahidi kumweka karibu vizur basi hakiki unamtimizia mahitaji yake ya kimwili na kifedha yaani "penye udhia penyeza rupia"

Ila ukimuacha na kuamua aende basi yule dogo mwenye miaka 24 mtoto wa mwenye nyumba yeye ataona kapata na ataendelea kujisitili maana "ganda la mua la jana chungu kaona kivuli"

ila kingine wewe ni mwanaume shababi, usiwe nyoronyoro pambana maana ungekuwa mjanja wa mademu la usingelialia. si unajua "Mgaaga na upwa hali wali mkavu" eeee

na kama hutaki kabisa kuonana nae tena jikaze kiume tafuta demu mwingine na ishi nae kwa akili na kumbuka busara zangu. na usimkumbuke kabisa wa zamani ww deal na huyo mpya utaempata maana "Mla mla leo mla jana kala nini"


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Very nice comment hii ni ya mwaka 2019 bro though leo ni tarehe 13 january, mkuu umesema hkn anaejua wanawake lkn kwa heshima ya hii comment ww unawajuaa....

Awa viumbe ukiingia kichwa kichwa kulia na maskitiko avitakuacha salama, muhimu ni kuishi maisha yako, uwe mtu usiyetabirika, Kosa ambalo yeye ataliona dogo ww likuze, ambalo yy ataliona kubwa ww lifanye liwe dogo, mfanye aamini hata bila ww still utasimama tena ndani ya muda mfupi tu, na tena unaweza kuwa na mwingine....

Azitegemee akiri zako na sio ww utegemee zake, mpe nafsi, mshauri pale tu inapobidi sio kila mkiingia rum ww ni ushauri na nasihi km mko angaza, muongezee maalifa kidogo yale ambyo ww unayahitajii....mfanye kuwa rafiki na sio km ulivyo ww.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Naam mkuu. Tuko pamoja. Wanaoelewa hili wala hawapatagi tabu. Mahusiano yanakuwa smooth. Mwanamke anajikeep in check mwenyewe. Anakuwa on her toes.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sanaa MrRegion, nalifanyia kazi shauri lako, thanks

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanaume bro tunapitia makubwa ila tuliumbwa majasiri sana katika kupambana. Nakushauri tafuta mwingine maana naamini kuna mtu yupo kwaajili yako na utafrahia uhusiano wenu Mpya kuliko kuhangaika na Malaya huyo ambae hata umsamehe atakusumbua sana na hutafurahia uwepo wako hapa duniani.

Bro plz kimbia sana huyo ni shetani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua ni vizuri kufahamu kwanini mwenzako amekupenda japo ni ngumu sana. Nilichogundua huyo bibie ulikuwa unamtimizia mahitaji ya kifedha zaidi kuliko ya kimapenzi ndio maana alipopata hyo kazi akaona huna umuhimu kwa kiasi kubwa km zamani so akapata mtaalam wa kukata kiu yake ya kimapenzi. Anyway achana naye huyo vumilia tu yatapita. But next time ukipata mtu mwingine usirudie kosa. HAKIKISHA UNAKATA KIU KWELI KWELI!
Download playlist moja ya reggae inaitwa Lovers Reggae rhythm 2014 uuguze machungu vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahah Lovers Riddim
 
Wakubwa zangu shikamooni, vijana wenzangu habari vipi?
Ndugu zangu, nipo serious sanaa katika ombi langu, nakuomba unipe muda wa kunisikiliza kidogo na unishauri kama inafaa.

Mimi ni kijana nina umri wa miaka 29, ni mwajiliwa serikalini idara ya Afya. Kuna binti nilianza nae uchumba 2017 mwanzoni yeye akiwa chuo flan cha afya, Mimi ni Mgogo yeye ni Mbulu ana miaka 24 sasa.

Tulianza mapenzi akiwa ameonesha msimamo wa kutoshiriki tendo lolote na mimi mpaka mwaka mmoja ulipopita ndo tukaanza kukutana kimwili. Ni binti ambae niliona huyu anafaa kuwa mke wangu kabisaa maana alikua ana msimamo sanaa hata kwa watu wengi waliokua wakimtongoza maana alikua ananionesha sms na calls zao, bas nikawa namshauri wajibu wewe ni mke wa mtu na unahitaji heshima, kiukweli nilijipa moyo hapa nimepata mke kweli kweli.

Basi akamaliza chuo 2017 mwishoni nikamtaftia ajira ya kujishikiza mahali flani mkoa wa Mwanza. Sasa nikawa nimeongea na mtu mmoja awe anafatilia nyendo zake wakati mimi nipo mbali.

Alipotimiza miezi miwili kazini nikapata taarifa kuna kabwana mdogo ka umri wa miaka 22 - 24 kanatembea nae hapo hapo alipopanga chumba, sikutaka kuamini, ikanibidi siku moja nifanye kusadiri kwenda kumtembelea kimya kimya bila taarifa, nikafika akanipokea vizuri. Ilipofika usiku nikamwambia sasa mpenzi unaweza kunihakikishia huku huna mchezo wowote mchafu wa kimahusiano? Akanijibu hapana kabisa mpenzi wangu naomba uniamini.

Nikamuuliza, Je, unaweza kunipa simu yako nikague chochote? Akapata kigugumizi sanaaaaa, nikamuuliza Unanipenda na unajiamini? Akajibu ndio, nikamwambia bas naomba simu yako, akapata kigugumizi kizito sanaaa.

Basi ikanibidi nichukue simu yake nipitie sms na whatsap, aseee niliyoyakuta ni mazito mnooooooo wallahi Nimepata simanzi kubwa sanaaa, ikanibidi niondoke usiku huo huo kwenda kutafta Lodge nikalala na kesho nikaondoka kurudi kazini.

Mchumba wangu huyu nilikua nimeshafahamiana na ndugu zake baadhi na mama yake mzazi alikua ananijua kwa picha tu na alikua tayari karidhia niwewe mkwe wake kabla hata sijaenda kujitambulisha maana matendo niliyomfanyia mwane ni mwanaume mwenye malengo mazuri wazi wazi. Kinachoniuma zaidi ni kwamba nimetumia muda mwingi sanaaa kumjenga kiimani, kumjenga juu ya tabia za wanaume wenye tamaa, kiukweli niliamini huyu mwanamke sasa hakuna atakae weza kumshawishi maana hata mimi binafsi nilikua nimebadilika sanaaa kitabia sikuwa nnahamu na michepuko tena niliona sasa huu ni muda wa kutulia na mwanamke mmoja sina haja ya kutanga tanga na dunia ya leo.

Ndugu zangu niko serious sanaaa, naombeni ushauri cha kufanya, mwanamke huyu alikua anatembea na kijana wa mwenye nyumba tena kwa kulala nae chumbani kwake karibu kila wiki.

Mwanamke alionesha sanaaa kunipenda tulikua tunawasiliana kila siku zaidi ya mara 5 kila siku ya Mungu. Leo naona dunia imenigeuka, nina maumivu makali sanaaaa, niliplan nije kumtambulisha kwetu mwaka huu December, na kwao ningeenda kujitambulisha November ili mwakani Mungu akijaalia tufunge Ndoa. Wakuu, niko gizani, nina msongo wa mawazo, mimi ni jasiri sanaaa lakini nakuomba wewe ndugu yangu ushauri wako katika hili, nakuomba usinitukane wala kunikejeli maana utaniongezea majonzi makubwa.

Naamini thread yangu hii itawafunza na wengine watakao kumbwa na mkasa kama wangu.
ASANTE kwa Muda wako

Sent using Jamii Forums mobile app

Kinachowauwa watu kwa stroke ni expectation hasa zinapoenda oposite so ukikosea kuamini m2 kwa 100%
Kwenye maisha hakikisha v2 viwili havikupati ili ubaki salama
(1)hakikisha humwamini binadamu awaye yote kwa 100%
(2)hakikisha hakuna m2 anayekuamini kwa 100%
Then utaishi kwa amani
 
Huyo ulimkosea kuanzia mwanzo. Ulimuendea kistaarabu mno na ukawa mpole mno. Dalili mojawapo ni kukaa mwaka bila papuchi...

Wanawake hawapendi nice guys mkuu. Hata kama ni muoaji, be a man. Kuwa na misimamo. Usifuate matakwa yake muda wote, be a priority to yourself.

Muendeshe. Demand utmost respect. Usionyeshe kumuamini. Onyesha kuwa una options na sio kwamba yeye ndio kila kitu kwako. Mwambie kuwa she is highly replaceable hivyo akijiskia at any time anaweza kuondoka.

Mmiliki, lakini be confident. Usimfuatilie mawasiliano yake na nyendo zake. Na ukigundua kitu kwenye simu yake, usimwambie. Basically ingekuwa mahakamani tungesema whatever you find in her phone is inadmissible evidence.

Hakuna principle moja kwamba ukimpa mwanamke kitu flani atatulia. No man knows what women want. Neither do themselves. Neither does God, hata akasema tuishi nao kwa akili.

Hizo principles nilizokupa zitakukinga dhidi ya upuuzi wa hawa viumbe in the future. Your sanity is more important than sex and affection.

Huyo hata ukimsamehe, nakuasi usirudiane naye. Ameshakumark weakness yako. Alianza kukupush limits zako kidogo kidogo na ameshazisogeza sana. Hakufai tena.

Kila mtu ana namna yake ya kudeal na heartbreak. Do what a nigga's got to do.

Sent using Jamii Forums mobile app

hii iko sawa
 
Huyo ulimkosea kuanzia mwanzo. Ulimuendea kistaarabu mno na ukawa mpole mno. Dalili mojawapo ni kukaa mwaka bila papuchi...

Wanawake hawapendi nice guys mkuu. Hata kama ni muoaji, be a man. Kuwa na misimamo. Usifuate matakwa yake muda wote, be a priority to yourself.

Muendeshe. Demand utmost respect. Usionyeshe kumuamini. Onyesha kuwa una options na sio kwamba yeye ndio kila kitu kwako. Mwambie kuwa she is highly replaceable hivyo akijiskia at any time anaweza kuondoka.

Mmiliki, lakini be confident. Usimfuatilie mawasiliano yake na nyendo zake. Na ukigundua kitu kwenye simu yake, usimwambie. Basically ingekuwa mahakamani tungesema whatever you find in her phone is inadmissible evidence.

Hakuna principle moja kwamba ukimpa mwanamke kitu flani atatulia. No man knows what women want. Neither do themselves. Neither does God, hata akasema tuishi nao kwa akili.

Hizo principles nilizokupa zitakukinga dhidi ya upuuzi wa hawa viumbe in the future. Your sanity is more important than sex and affection.

Huyo hata ukimsamehe, nakuasi usirudiane naye. Ameshakumark weakness yako. Alianza kukupush limits zako kidogo kidogo na ameshazisogeza sana. Hakufai tena.

Kila mtu ana namna yake ya kudeal na heartbreak. Do what a nigga's got to do.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeandika vitu vya msingi sana na hivi ndivyo tunapaswa kujua kuhusu wanawake

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

30 Reactions
Reply
Back
Top Bottom