Mchumba wangu kanisaliti!! Niko kwenye maumivu makali naombeni ushauri

Huyo ulimkosea kuanzia mwanzo. Ulimuendea kistaarabu mno na ukawa mpole mno. Dalili mojawapo ni kukaa mwaka bila papuchi...

Wanawake hawapendi nice guys mkuu. Hata kama ni muoaji, be a man. Kuwa na misimamo. Usifuate matakwa yake muda wote, be a priority to yourself.

Muendeshe. Demand utmost respect. Usionyeshe kumuamini. Onyesha kuwa una options na sio kwamba yeye ndio kila kitu kwako. Mwambie kuwa she is highly replaceable hivyo akijiskia at any time anaweza kuondoka.

Mmiliki, lakini be confident. Usimfuatilie mawasiliano yake na nyendo zake. Na ukigundua kitu kwenye simu yake, usimwambie. Basically ingekuwa mahakamani tungesema whatever you find in her phone is inadmissible evidence.

Hakuna principle moja kwamba ukimpa mwanamke kitu flani atatulia. No man knows what women want. Neither do themselves. Neither does God, hata akasema tuishi nao kwa akili.

Hizo principles nilizokupa zitakukinga dhidi ya upuuzi wa hawa viumbe in the future. Your sanity is more important than sex and affection.

Huyo hata ukimsamehe, nakuasi usirudiane naye. Ameshakumark weakness yako. Alianza kukupush limits zako kidogo kidogo na ameshazisogeza sana. Hakufai tena.

Kila mtu ana namna yake ya kudeal na heartbreak. Do what a nigga's got to do.

Sent using Jamii Forums mobile app
Very nice comment hii ni ya mwaka 2019 bro though leo ni tarehe 13 january, mkuu umesema hkn anaejua wanawake lkn kwa heshima ya hii comment ww unawajuaa....

Awa viumbe ukiingia kichwa kichwa kulia na maskitiko avitakuacha salama, muhimu ni kuishi maisha yako, uwe mtu usiyetabirika, Kosa ambalo yeye ataliona dogo ww likuze, ambalo yy ataliona kubwa ww lifanye liwe dogo, mfanye aamini hata bila ww still utasimama tena ndani ya muda mfupi tu, na tena unaweza kuwa na mwingine....

Azitegemee akiri zako na sio ww utegemee zake, mpe nafsi, mshauri pale tu inapobidi sio kila mkiingia rum ww ni ushauri na nasihi km mko angaza, muongezee maalifa kidogo yale ambyo ww unayahitajii....mfanye kuwa rafiki na sio km ulivyo ww.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama unahisi ni mwanamke pekee wa maisha yako, rudiana naye. Na kama unahisi unaweza kupata mwanamke sahihi wa kumuoa basi piga chini na maisha yaendelee
 
Mkuu sio kila jambo linahitaji solution mambo kama hayo ni udhaifu wa kibinadamu tu.

Ila kumbuka dume la uhakika halimchungulii mkewe. Matatizo hayo utakutana naye almost kwa kila mwanamke.
 
Wakubwa zangu shikamooni, vijana wenzangu habari vipi?
Ndugu zangu, nipo serious sanaa katika ombi langu, nakuomba unipe muda wa kunisikiliza kidogo na unishauri kama inafaa.

Mimi ni kijana nina umri wa miaka 29, ni mwajiliwa serikalini idara ya Afya. Kuna binti nilianza nae uchumba 2017 mwanzoni yeye akiwa chuo flan cha afya, Mimi ni Mgogo yeye ni Mbulu ana miaka 24 sasa.

Tulianza mapenzi akiwa ameonesha msimamo wa kutoshiriki tendo lolote na mimi mpaka mwaka mmoja ulipopita ndo tukaanza kukutana kimwili. Ni binti ambae niliona huyu anafaa kuwa mke wangu kabisaa maana alikua ana msimamo sanaa hata kwa watu wengi waliokua wakimtongoza maana alikua ananionesha sms na calls zao, bas nikawa namshauri wajibu wewe ni mke wa mtu na unahitaji heshima, kiukweli nilijipa moyo hapa nimepata mke kweli kweli.

Basi akamaliza chuo 2017 mwishoni nikamtaftia ajira ya kujishikiza mahali flani mkoa wa Mwanza. Sasa nikawa nimeongea na mtu mmoja awe anafatilia nyendo zake wakati mimi nipo mbali.

Alipotimiza miezi miwili kazini nikapata taarifa kuna kabwana mdogo ka umri wa miaka 22 - 24 kanatembea nae hapo hapo alipopanga chumba, sikutaka kuamini, ikanibidi siku moja nifanye kusadiri kwenda kumtembelea kimya kimya bila taarifa, nikafika akanipokea vizuri. Ilipofika usiku nikamwambia sasa mpenzi unaweza kunihakikishia huku huna mchezo wowote mchafu wa kimahusiano? Akanijibu hapana kabisa mpenzi wangu naomba uniamini.

Nikamuuliza, Je, unaweza kunipa simu yako nikague chochote? Akapata kigugumizi sanaaaaa, nikamuuliza Unanipenda na unajiamini? Akajibu ndio, nikamwambia bas naomba simu yako, akapata kigugumizi kizito sanaaa.

Basi ikanibidi nichukue simu yake nipitie sms na whatsap, aseee niliyoyakuta ni mazito mnooooooo wallahi Nimepata simanzi kubwa sanaaa, ikanibidi niondoke usiku huo huo kwenda kutafta Lodge nikalala na kesho nikaondoka kurudi kazini.

Mchumba wangu huyu nilikua nimeshafahamiana na ndugu zake baadhi na mama yake mzazi alikua ananijua kwa picha tu na alikua tayari karidhia niwewe mkwe wake kabla hata sijaenda kujitambulisha maana matendo niliyomfanyia mwane ni mwanaume mwenye malengo mazuri wazi wazi. Kinachoniuma zaidi ni kwamba nimetumia muda mwingi sanaaa kumjenga kiimani, kumjenga juu ya tabia za wanaume wenye tamaa, kiukweli niliamini huyu mwanamke sasa hakuna atakae weza kumshawishi maana hata mimi binafsi nilikua nimebadilika sanaaa kitabia sikuwa nnahamu na michepuko tena niliona sasa huu ni muda wa kutulia na mwanamke mmoja sina haja ya kutanga tanga na dunia ya leo.

Ndugu zangu niko serious sanaaa, naombeni ushauri cha kufanya, mwanamke huyu alikua anatembea na kijana wa mwenye nyumba tena kwa kulala nae chumbani kwake karibu kila wiki.

Mwanamke alionesha sanaaa kunipenda tulikua tunawasiliana kila siku zaidi ya mara 5 kila siku ya Mungu. Leo naona dunia imenigeuka, nina maumivu makali sanaaaa, niliplan nije kumtambulisha kwetu mwaka huu December, na kwao ningeenda kujitambulisha November ili mwakani Mungu akijaalia tufunge Ndoa. Wakuu, niko gizani, nina msongo wa mawazo, mimi ni jasiri sanaaa lakini nakuomba wewe ndugu yangu ushauri wako katika hili, nakuomba usinitukane wala kunikejeli maana utaniongezea majonzi makubwa.

Naamini thread yangu hii itawafunza na wengine watakao kumbwa na mkasa kama wangu.
ASANTE kwa Muda wako

Sent using Jamii Forums mobile app
We nawe kuna makabila hata huitaji kujitia unapenda kupindukia utaishia kuumia tu, Manyara, Singida, Dodoma, Arusha (exl Maasai na Meru), Ruvuma, Mbeya, Songwe, Kagera, Tabora, Morogoro, Mtwara, Tanga, Dar, Pwani, Songwe usithubutu kujifanya unapenda sana utajikuta unapata magonjwa ya BP mapema sana.
Hafu usipende kusoma sms za simu ya mpenzi wako, labda kama ulimtoa bikra hapo atakuwa huru sana kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vijana mnataka presha za bure kwa kweli. Mtu na mgodi wake mwenyewe alafu unamchunga na kuchunguza....wewe wagegede tuu usiweke moyo wako kwa mwanamke ...utakuja kufa mapema.
Hawa wanawake ukiwapenda utaishia lia wewe bora mara mia uwagegede uwaache walie wao
 
Nakushukuru sanaa Brazaa, umenipa Courage ya Ajabu, najisikia faraja Moyoni.
Natamani hata tufahamiane Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Pia brother hata ukioana naye hutamuamini kamwe, na hata ukijifanyisha kumuamini bado hutamuamini. Je, angefanya haya tayari mpo kwenye ndoa? Yaani kama umemsaidia hayo yote, umempa msingi wa maisha na bado akakusaliti maana yake hafai. Kwa nini uingie kwenye ndoa na mwanamke ambaye humuamini? Kwani kuanza upya ni kosa? Umeyajua haya kwa sababu pia ulipanga uyajue na sasa umeyajua. Naamini unaweza kuanza upya na umejifunza na huwezi kurudia kosa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makosa yako ni:
1.kukagua simu yake,
2.kumtrack mienendo yake(aligundua ndio maana akakuaminisha kuwa kawakataa wote wanaomtongoza)
3.kukaa nae mbali
4.kumuonyesha unampenda sana,
5.kumletea ulokole,

NB: Asilimia kubwa wanawake wa hilo kabila(sio wote) ni warembo ila ni maharage ya mbeya yaani maji Mara moja NA wewe umetokea kabila ambalo asilimia kubwa(sio wote) ni malimbukeni wa wanawake warembo eg. MC CHILL

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakazia hapa. Tatizo lake kubwa ni namba 3, 4 , 5 na hiyo NB.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom