Mchumba wangu anapenda kuvaa nguo zangu

Bavaria

JF-Expert Member
Jun 14, 2011
53,102
53,351
Habari za asubuhi wapendwa.
Nina mchumba wangu ambae anasoma chuo sasa, na mara nying hupenda kuja kushinda kwangu weekends. Sasa sijui ni nini, huyu mdada anapenda sana kuvaa nguo zangu na kushinda nazo au kulala nazo. Naombeni wana jf mnisaidie hapa, tatizo linaweza kuwa nini?
 
kaka huku nahisi utazinguliwa tu kama unavoona majibu ya hao hapo juu labda uendelee subiri uone, mi nadhani itakuwa labda anapenda au anafata ushauri wa kalumanzila, kama hana mambo ya kalumanzila mwache tu avae
 
Habari za asubuhi wapendwa.
Nina mchumba wangu ambae anasoma chuo sasa, na mara nying hupenda kuja kushinda kwangu weekends. Sasa sijui ni nini, huyu mdada anapenda sana kuvaa nguo zangu na kushinda nazo au kulala nazo. Naombeni wana jf mnisaidie hapa, tatizo linaweza kuwa nini?

Baadhi ya wadada huwa wana tabia hizi. Wengine hupenda kuvaa mashati au hata t-shirt za wapenzi wao na wengine ni mpaka boxer! Kama wewe mwenyewe haukwazi na jambo kama hilo, unaweza kulipotezea maana hakuna ubaya wowote wa yeye kuvaa nguo zako. Ila kama unakwazika, unaweza kutafuta namna ya kumfikishia ujumbe kwa namna ambayo hataweza kujisikia vibaya ili penzi lenu lisiyumbe kwa vitu vidogo vidogo kama hivi.
Kila la kheri mwana!
 
Ni mapenzi tu hakuna kingine,mimi mke wangu huwa anapenda kuvaa t shirt zangu na huwa naona sawa tu maana huleta mvuto zaidi wa mapenzi,kama wa kwako anavaa boxer pia si mbaya ni kwa kuwa anapenda kufanya hivyo na kukuonesha kuwa anakupenda na anajisikia raha kuzivaa.
 
Ile dawa ya kunasana kama tukio lililotokea Temeke huwa inatumiwa kwa kuvaa nguo ya mtu unayetaka kumkamatisha so mkuu kuwa macho hapo ukienda nje tu una nafasi kubwa sana ya kunasa.
 
Sio tatizo sana kuvaa nguo zako! ni katika kujiamini tu kuwa yoyote atakae kuja ghafla asipate cha kuuliza kwani si rahisi dadaako akavaa nguo zako.
Sasa kama wewe ni kicheche akitoka huyo unamleta mwingine nae anavaa au havai kazi kwako kaka.
 
kaka huku nahisi utazinguliwa tu kama unavoona majibu ya hao hapo juu labda uendelee subiri uone, mi nadhani itakuwa labda anapenda au anafata ushauri wa kalumanzila, kama hana mambo ya kalumanzila mwache tu avae

hapana mkuu, hili ni tatizo la kawaida kabisa, ni issue za kisaikolojia zaidi, they like kuvaa nguo zetu wakati mwingine bt ukimuuliza why hana jibu, huwa tu wanataman, mie alikuwa wazi one day akanambia anapenda the way they smell, as inakuwa like tumekumbatiana. trust me mkuu wanawake ni watu wanaojua kukariri sana harufu, so akivaa anahisi mmekumbatiana au mmekaa pamoja. there's nothing wrong mkuu.
 
Kaka hapo usimkataze hata kidogo, anakufeel mno!!!!!!!!!!!!!!!:majani7:hizo pia ni namna na kukukubali sana kamanda na kukupa hisia, wewe vipiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii bana????:majani7:
 
Hilo halina shida yoyote, maana niipatayo ni kwamba demu wako hujisikia huru akiwa na wewe...
 
mkuu mbona hilo la kawaida sana.....kwan huyu si wako sasa woga wa nini? anafua yeye na anavaa yy tatizo nini sasa hapo....tena kama vipi na wewe kamata bikin zake cku moja moja unavaa shaka hakuna ndo mapenzi hayo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom