Mchumba wa mdogo wangu kazuiwa na ndugu zake kumuoa kwa kigezo cha dini tofauti ila mdogo wangu hajui

Mlundilwa Jr

JF-Expert Member
Dec 11, 2019
2,886
4,283
Habari wana jf
Kadri siku zinavyoenda nimekua naiangalia hii tamthilia anayoicheza mdogoangu hapa Duniani bado inaniweka njia panda

Iko hivi, mdogoangu alianzisha mahusiano na mwanaume ambaye kiukweli hakumjua vizuri na niseme tuu hata yule Boy hakumjua vizuri dogo kutokana na muonekano wake
Kiukweli dogo ni mweupe sana na Mungu kamjalia nywele za singasinga

Hali iliyopelekea jamaa amuhisi ni Mpemba au Mwarabu, basi bwana mahusiano yao yalikua ya siri sana hatimae wakapeana Mimba hapo ndipo harakati za kutaka kuchukuana ili wakaishi mume na mke zikaanza kwani jamaa alianza kuwashirikisha ndugu zake

Basi alipoenda kumtambulisha kwao familia ya jamaa ikamhoji mbona kama Mwarabu jamaa naye kwakutaka sifa akasema ndiyo

Basi naye mwenzangu na mie akaja na jamaa nyumbani ili kumtambulisha na mm binafsi sikujua kama dogo kapewa Mimba

Hatimaye siku ya kuja kumposa dogo tulishangaa jamaa na ndugu zake wanakuja na ostazi tena wakiwa wameambatana na watu wanaotokea huko Zanzibar wakiamini mwenzangu na mimi moja kwa moja ni muislam kitendo kilichofanya nihamaki na kujiuliza huyu dogo tayari kabadili Dini kumbe hapana bali wao walijua dogo ni muislamu

Ikabidi tuanze sisi akina kaka kujitambulisha ndipo wao wenyewe wakahamaki kumbe mkiristo? Basi ingawa hawakuonyesha dalili za moja kwa moja kushituka ikabidi waghairi kile walichojia na kusema basi mtaandika gharama za posa theni mtuletee

Basi walivyoenda kwao huko wakamshauri jamaa nenda kawaambie hadi Azae ndiyo tutatoa hiyo posa, basi bana siku zikaenda miezi ikasonga, hatimae dogo akajifungua

Wakamtuma tena jamaa nenda kawaambie kwanza mimi sina kazi pia Baba yangu alikufa ila ukweli nikwamba familia ilishamshauri usioe mwanamke Dini tofauti na wewe
Na ukiangalia mtu mwenyewe anatokea familia Duni

Sasa narudi kwa mwenzangu na mie ambaye ni mdogoangu yaani pamoja na danadana zote hizo bado yupo gizani akiamini ipo siku watamtolea posa. Ilihali familia ya jamaa ilishamuwekea x kutokana na Dini yake na anayejua hii siri ktk familia yetu ni mimi tuu

Na chaajabu anaenda kwa mwanaume kulala na kurejea hasubuhi nyumbani kwa Maza

Sasa wakuu najiuliza hivi hii character aliyopewa dogo itaisha vipi ktk hii tamthilia ya uhalisia

Nihayo wakuu yanayoendea huku Duniani.
 
1. ^Wakapeana mimba^

2. Je ulienda na ^jamaa^ -- wenzako na wewe -- maana unavyosimulia sasa, kaaa ulikuwepoooo!???


^Basi ingawa hawakuonesha dalili za moja kwa moja kushituka ikabidi waghairi kile walichojia na kusema basi mtaandika gharama za posa theni mtuletee.^

^Basi walivyoenda kwao huko wakamshauri jamaa nenda kawaambie hadi azae ndiyo tutatoa hiyo posa.^

^Wakamtuma tena jamaa nenda kawaambie kwanza mimi sina kazi pia Baba yangu alikufa ila ukweli nikwamba familia ilishamshauri usioe mwanamke Dini tofauti na wewe^


3. ^Tamthilia hii itaishi vipi?^ Hiyo comedy iishe mara ngapi, kimfano!???
 
2 . Naona dogo atakavyo telekezwa na jamaa .

3. Dgo ata pata mshtuko na kuhisi kma kapoteza direction ya life

4. Dgo ataanza kuwa cheap inshort yeyote atakae mtaka atampata as long as mwitaji awe mjanja mjanja na sound kibao

5. Atapigwa mimba ya pili

6. Punde tuu baada ya kutupa kichanga hicho ata jazwa ya tatu

7. To be continued
View attachment 1692374
 
Usipochukua hatua Kama Kaka tegemea kuletewa uncle wa pili hapo home, na dada aendelee kuishi home na watoto wake.

Dada anaenda huko akiamini ndoa ni suala la muda tu na tayari wameshatambulishana, wa kumtoa gizani ni wewe
 
Hebu uwaite wote mdogo wako na huyo mzinzi mwenzake na uwaambie ukweli juu ya upuuzi wanaoufanya. Natambua watachukia na kukusema wakiwa wawili lakini badae mdogo wako ataona umuhimu wako.
Unapokua mkubwa katika familia usiogope lawama hakikisha unaziba mapema kila penye nyufa.
 
2 . Naona dogo atakavyo telekezwa na jamaa .

3. Dgo ata pata mshtuko na kuhisi kma kapoteza direction ya life

4. Dgo ataanza kuwa cheap inshort yeyote atakae mtaka atampata as long as mwitaji awe mjanja mjanja na sound kibao

5. Atapigwa mimba ya pili

6. Punde tuu baada ya kutupa kichanga hicho ata jazwa ya tatu

7. To be continued
View attachment 1692374
Elewa mkuu, yeye hajui chochote kwani mahitaji ya mtoto wanamletea na kwa mwanaume anaenda kulala inshort familia upande wa kuume hawataki wao walijua wanaunganisha undugu na Wapemba chaajabu wanakuja kukuta dogo anatokea mazingira duni ila muonekano wake ulimbeba akawa anaonekana wa kishua
 
Hebu uwaite wote mdogo wako na huyo mzinzi mwenzake na uwaambie ukweli juu ya upuuzi wanaoufanya. Natambua watachukia na kukusema wakiwa wawili lakini badae mdogo wako ataona umuhimu wako.
Unapokua mkubwa katika familia usiogope lawama hakikisha unaziba mapema kila penye nyufa.
Yaani dogo hamsikilizi mtu, yeye anavyoona jamaa anamjali mtoto anaamini ipo siku atamchukua kumbe siyo familia imemuwekea x wanasema hawezi kuwapa makafiri posa
 
mshauri abadili dini
Yaani dogo alikua teyari kwa lolote ukiangalia na mimba aliyopewa na jamaa, ila familia ikamshauri asioe Mwanamke Dini tofauti na yeye, yaani mkuu hii character aliyopewa bwana mdogo yeye mwenyewe haielewi
 
Maji yaliyomwagika hayazoleki kwa sponchi/sponge
Kabisa mkuu ila yeye hajui tuu na kuna kipindi nilimwambia bi mkubwa hivi unajua kilichofanya wao wagaili kumchukua huyu mwanao chaajabu hajui
Na chaajabu alitaka kumuozesha mtu amabae hajui kazi anayofanya hapa mujini Darisalam
 
Usipochukua hatua Kama Kaka tegemea kuletewa uncle wa pili hapo home, na dada aendelee kuishi home na watoto wake.

Dada anaenda huko akiamini ndoa ni suala la muda tu na tayari wameshatambulishana, wa kumtoa gizani ni wewe
Mkuu bigup umenielewa
 
Kabisa mkuu ila yeye hajui tuu na kuna kipindi nilimwambia bi mkubwa hivi unajua kilichofanya wao wagaili kumchukua huyu mwanao chaajabu hajui
Na chaajabu alitaka kumuozesha mtu amabae hajui kazi anayofanya hapa mujini Darisalam
HILO NI KOSA KUBWA SANA
 
1. ^Wakapeana mimba^

2. Je ulienda na ^jamaa^ -- wenzako na wewe -- maana unavyosimulia sasa, kaaa ulikuwepoooo!???


^Basi ingawa hawakuonesha dalili za moja kwa moja kushituka ikabidi waghairi kile walichojia na kusema basi mtaandika gharama za posa theni mtuletee.^

^Basi walivyoenda kwao huko wakamshauri jamaa nenda kawaambie hadi azae ndiyo tutatoa hiyo posa.^

^Wakamtuma tena jamaa nenda kawaambie kwanza mimi sina kazi pia Baba yangu alikufa ila ukweli nikwamba familia ilishamshauri usioe mwanamke Dini tofauti na wewe^


3. ^Tamthilia hii itaishi vipi?^ Hiyo comedy iishe mara ngapi, kimfano!???
Jamaa alijaza mimba
 
Kwanini ulijipeleka wakujue wewe na ndio maana unahangaika, kama hukuona shida na mdogo wako angebadili dini.. ulishindwaje kumpa ushauri!!.. pole kwa kujua umesababisha haya matokeo na wenzako pia mlioyafanya..
 
Back
Top Bottom