Mchumba ninae taka kumuoa nimegundua anavuta bangi

alberttt

Member
Sep 30, 2016
50
120
Wadau naomben ushauri.....nimegundua kuwa mke wngu mtarajiwa anavuta bangi....nilikua sifahamu hapo mwanzo sababu alinificha....nimemfumania akivuta chumbani niliporudi toka kazin bila kumfahamisha.nipo dailema
 
black uhuru.jpg
 
Mara mchumba mara mke, which is which mkuu!!

BTW kwani kuna tatizo lolote hutokea akivuta?
 
Endelea nae, hilo sio jambo kubwa la kukufanya umwache. Ukitaka mkalishe tu vizuri na jadilianeni namna ya kumfanya apunguze.
 
Comments utakazopata humu kuhusiana na demu wako kuvuta bangi hazitakidhi.Miaka kadhaa ya humu Jf imenifundisha kuwa wengi humu ni wavuta bangi na hawatakushauri kinyume na kile wanachopenda.Fuata moyo wako.Je, unadhani unaweza kuvumilia kuishi na mvuta bangi for the rest of your life?TAFAKARI,CHUKUA HATUA STAHIKI.
 
Dosari umeitengeneza mwenyewe tangu mwanzo.
"Mchumba wangu... nimemfumania akivuta chumbani niliporudi toka kazini....".
Mchumba wako atakaa chumbani kwako?
Mchumba'ako anastahili kuishi kwa wazazi wake hadi utakapomuoa na kuwa mke.
Huyo uliyemkuta anavuta bhangi chumbani kwako ni hawara yako.
Mmomoyoko wa maadili uliokuta akiufanya yeye, umeufanya wewe pia kwa njia nyingine. Hilo la kwanza.
La pili sielewi kama una ujuzi wa kum-re hurb teja na akawa "mtoto mzuri" kufikia kuachana na hiyo tabia yake na kuwa mama familia bora.
M/Mungu hupenda kuwaepusha waja wake mapema kwa njia ya ndoto, hisia, fumanizi kama hilo nk nk.
Wasichana wenye nidhamu zao wameisha mtaani hadi uendelee kuwaza hatua za kuchukua dhidi ya hilo fisadi?
Kwa kuwa uliyemfumania akivuta bhangi chumbani kwako ni hawara yako, endelea naye kula maisha kwa kuwa ni mwanamke uliyemhodhi kwako kwa ajili ya starehe na starehe mojawapo ni hizo.
Utakapoamua kuoa utafuata taratibu za kuoa na utapata mke bora
 
Wadau naomben ushauri.....nimegundua kuwa mke wngu mtarajiwa anavuta bangi....nilikua sifahamu hapo mwanzo sababu alinificha....nimemfumania akivuta chumbani niliporudi toka kazin bila kumfahamisha.nipo dailema

Kwani aliyekuambia kuvuta ' Bangi / Bange ' ni dhambi nani? Kuna uhusiano gani wa Wewe kumuoa Yeye kama Yeye na hizo ' Sigara Bwege / Bange / Bangi ' anazovuta?
 
Wadau naomben ushauri.....nimegundua kuwa mke wngu mtarajiwa anavuta bangi....nilikua sifahamu hapo mwanzo sababu alinificha....nimemfumania akivuta chumbani niliporudi toka kazin bila kumfahamisha.nipo dailema
Muoe waambie wifi zake wamletee gunia la bangi kama zawadi ya Harusi atashtukia umeshajua mienendo yake usiyoipenda!
 
Ni kawaida sana kimsingi tumia hekima na busara kwake khs hilo suala litaisha. Ingelikua ngono sawa ila bangi si mbaya.
 
Back
Top Bottom