Kamati Kuu ya CHADEMA imetoa rasmi orodha ya wagombea wa nafasi mbalimbali katika kanda zake zote 10 baada ya mchujo mkali.
Kati ya Orodha hiyo mvuto mkubwa ni nafasi ya Uenyekiti kanda ya Kaskazini ambako kuna mtifuano mkubwa kati ya wabunge wake wawili machachari Godbless Lema na Joseph Selasini.
Kanda nyingine yenye mvutano mkubwa ni kanda ya Serengeti ambako mafahali wawili wabunge John Suguta Heche na Esther Matiko wanawania nafasi ya Uenyekiti.
Kanda nyingine inayotizamwa na mashabiki wa siasa nchini ni Kanda ya Kati ambapo Alhonce Mbassa na Lazaro Nyalandu wanachuana kugombea Uenyekiti
Kanda ya Kusini nako si haba kwani wababe wawili wa siasa za kusini Suleiman Mathew na Cecil Mwambe wanachuana kugombea uenyekiti.
Hata hivyo Kanda ya Pwani inayotizamwa kama Kanda Kiongozi Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Tluway Sumaye amepita bila kupingwa kugombea Uenyekiti hiyo ikionekana kama heshima kubwa kwake.
Ikumbukwe kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA washindi wote wa nafasi ya Uenyekiti wa Kanda moja kwa moja watahesabika kama wajumbe wa Kamati Kuu.
Kati ya Orodha hiyo mvuto mkubwa ni nafasi ya Uenyekiti kanda ya Kaskazini ambako kuna mtifuano mkubwa kati ya wabunge wake wawili machachari Godbless Lema na Joseph Selasini.
Kanda nyingine yenye mvutano mkubwa ni kanda ya Serengeti ambako mafahali wawili wabunge John Suguta Heche na Esther Matiko wanawania nafasi ya Uenyekiti.
Kanda nyingine inayotizamwa na mashabiki wa siasa nchini ni Kanda ya Kati ambapo Alhonce Mbassa na Lazaro Nyalandu wanachuana kugombea Uenyekiti
Kanda ya Kusini nako si haba kwani wababe wawili wa siasa za kusini Suleiman Mathew na Cecil Mwambe wanachuana kugombea uenyekiti.
Hata hivyo Kanda ya Pwani inayotizamwa kama Kanda Kiongozi Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Tluway Sumaye amepita bila kupingwa kugombea Uenyekiti hiyo ikionekana kama heshima kubwa kwake.
Ikumbukwe kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA washindi wote wa nafasi ya Uenyekiti wa Kanda moja kwa moja watahesabika kama wajumbe wa Kamati Kuu.