Mchovu Yosefu Sinde Warioba ana ajenda gani na vijana?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,468
911,172
Nimepitia mara wa kadhaa kuanzia jana yatokanayo na hoja za Waziri Mkuu Mstaafu Yosefu Sinde Warioba kwenye TBC1 jana akiwamwagia dongo vijana kuwa waache kulalamika juu ya uongozi uliopo...................hoja zake ambazo zilinifanya nianze kujiuliza ya kuwa hivi Sinde akiwa na miaka 35 Nyerere alipomteua kuwa Mwanasheria Mkuu hivi kigezo hakikuwa ni nepotism kweli maana sioni kama ni mtu mwenye busara hata chembe................................

hoja ya Sinde ni kuwa Nyerere alipokuwa Waziri mkuu wa kwanza akiwa na miaka 39 alikuwa kijana...........aliyemrithi pia Kawawa alikuwa ni kijana.................................na wengi wa mawaziri Wakuu ukiwaondoa Msuya na Malecela walikuwa vijana..........................kwa hiyo huo ndiyo ushahidi wake wa ya kuwa vijana wamekuwa wakiongoza nchi hii na kizazi hiki cha vijana kiache malalamiko...........


Hoja hizi zinanikumbusha profesa mmoja mwalimu wangu aliwahi kusema ukiacha wafanye maamuzi kwa niaba yako watakula pia kwa niaba yako..........

Kule ufaransa akina Boukassa na Leopald Senghor waliteuliwa kuwa wabunge kwenye Bunge la ufaransa.........................Mkoloni huyo alibuni utaratibu huo ili kuhalalisha uporaji wa mali katika makoloni yake......................kwa hoja ya kuwa acheni kulalamika mbona watu wenu kutoka kwenye makoloni tunakula nao meza moja hapa ulaya?.........................mbinu hizohizo hata Mwingereza alizitumia kwa akina banda wa malawi kuwa daktari wa malkia n.k..................

tatizo la kizazi cha vijana wa leo siyo kukosa uwakilishi ndani ya taswira ya uongozi ila wao wanashirikishwa vipi katika kuzitambua chachu za maendeleo na kuzipangilia chachu tajwa ikiwemo kutekeleza mipango ya maendeleo..................siyo kuwakilishwa katika High Table pekee...................hakutoshi kuwawezesha kuweka ugali na maharagwe kwenye meza ndani ya vibanda vyao vya nyasi...........................
 
Huyu mzee katushikia bango sana vijana bila kujua sababu,na wala siioni anachoongea....anataka vijana wa CCM na vijana upande wa upinzani tuungane tuwe wamoja bila kusema tuungane kwa namna gani,hoja yake haiweki wazi anakuwa kama anaogopa vile kuweka wazi mawazo yake....
 
Angetoa mfano wa Nape ningevunja TV au Radio yangu muda ule ule....ingekuwa ni dharau kubwa kwa Taifa,vijana na wananchi kwa ujumla....
Mkuu juzi nimesikia Hotuba flani ya Nyerere anasema nanukuu "Upumbavu uko kwa aina mbalimbali kama ambavyo kuna mtu mrefu na mwingine mfupi"
Kwa maana hii ya Nyerere naamini kiupumbavu Sinde ni mrefu kuliko Hashimu Zabiti.
 
Mkuu juzi nimesikia Hotuba flani ya Nyerere anasema nanukuu "Upumbavu uko kwa aina mbalimbali kama ambavyo kuna mtu mrefu na mwingine mfupi"
Kwa maana hii ya Nyerere naamini kiupumbavu Sinde ni mrefu kuliko Hashimu Zabiti.

Mkuu hiyo nami nilisikia na nilicheka sana lol!! Kweli Babu yetu wa Taifa na wengine baba wa taifa kwao aliona mbali sana.....
 
Nimepitia mara wa kadhaa kuanzia jana yatokanayo na hoja za Waziri Mkuu Mstaafu Yosefu Sinde Warioba kwenye TBC1 jana akiwamwagia dongo vijana kuwa waache kulalamika juu ya uongozi uliopo...................hoja zake ambazo zilinifanya nianze kujiuliza ya kuwa hivi Sinde akiwa na miaka 35 Nyerere alipomteua kuwa Mwanasheria Mkuu hivi kigezo hakikuwa ni nepotism kweli maana sioni kama ni mtu mwenye busara hata chembe................................

hoja ya Sinde ni kuwa Nyerere alipokuwa Waziri mkuu wa kwanza akiwa na miaka 39 alikuwa kijana...........aliyemrithi pia Kawawa alikuwa ni kijana.................................na wengi wa mawaziri Wakuu ukiwaondoa Msuya na Malecela walikuwa vijana..........................kwa hiyo huo ndiyo ushahidi wake wa ya kuwa vijana wamekuwa wakiongoza nchi hii na kizazi hiki cha vijana kiache malalamiko...........


Hoja hizi zinanikumbusha profesa mmoja mwalimu wangu aliwahi kusema ukiacha wafanye maamuzi kwa niaba yako watakula pia kwa niaba yako..........

Kule ufaransa akina Boukassa na Leopald Senghor waliteuliwa kuwa wabunge kwenye Bunge la ufaransa.........................Mkoloni huyo alibuni utaratibu huo ili kuhalalisha uporaji wa mali katika makoloni yake......................kwa hoja ya kuwa acheni kulalamika mbona watu wenu kutoka kwenye makoloni tunakula nao meza moja hapa ulaya?.........................mbinu hizohizo hata Mwingereza alizitumia kwa akina banda wa malawi kuwa daktari wa malkia n.k..................

tatizo la kizazi cha vijana wa leo siyo kukosa uwakilishi ndani ya taswira ya uongozi ila wao wanashirikishwa vipi katika kuzitambua chachu za maendeleo na kuzipangilia chachu tajwa ikiwemo kutekeleza mipango ya maendeleo..................siyo kuwakilishwa katika High Table pekee...................hakutoshi kuwawezesha kuweka ugali na maharagwe kwenye meza ndani ya vibanda vyao vya nyasi...........................[/QUOTE]

Kwanza omba radhi kwa kutukana watu wazima kama Warioba. ANGALIA RED QUOTE, sasa kama wewe kajana huzitambui chachu za maendeleo na huna mipango Jaji Warioba kasema uongo gani? Kwa hiyo unataka kufanyiwa spoon-feeding?
 
Huyu mzee katushikia bango sana vijana bila kujua sababu,na wala siioni anachoongea....anataka vijana wa CCM na vijana upande wa upinzani tuungane tuwe wamoja bila kusema tuungane kwa namna gani,hoja yake haiweki wazi anakuwa kama anaogopa vile kuweka wazi mawazo yake....

huyu babu ni mchovu sana sioni jingine.............................angelikuwa ana busara angeliendelea kula sembe yake ya bwerere ambayo nayo ni mfano wa kiubaguzi.......................inakuwaje viongozi wa ngazi za juu kitaifa wawe na pensheni yenye rutuba na wengineo wasiwe nayo..........
 
Kwanza omba radhi kwa kutukana watu wazima kama Warioba. ANGALIA RED QUOTE, sasa kama wewe kajana huzitambui chachu za maendeleo na huna mipango Jaji Warioba kasema uongo gani? Kwa hiyo unataka kufanyiwa spoon-feeding?

wewe wala hujanielewa........................vuijana hawataki spoon-feeding bali wanataka kushirikishwa katika kupanga na kusimamia maendeleo yao............hawataki wawekezaji kutoka nje na wao wawe wapagasi wao..........
 
Wakati wa uhuru wasomi wachache waliokuepo waliingizwa serikalini kuchukua nafasi za wakoloni waliokua wanaondoka. Nikiangalia hoja ya Warioba kuhusu vijana wa sasa,ningekua mtangazaji ningemwuliza yeye na wazee wenzake wamefanya nini kuwezesha vijana kuchukua madaraka? Wamesaidiaje kukuza na kurutubisha demokrasia ya vyama vingi?
 
Ahsante sana Ruta kwa kulileta hili suala la huyu mzee! Binafsi nmekuwa natafakari kauli zake toka jana, na pia hapa saiv namsoma kwenye Raia Mwema.. . Kwa umri wake na pia kama sehemu ya mjenzi wa mfumo wa nchi yetu, nmesononeshwa sana na mtazamo wa mzee.
Haikumpasa ye kuishi kutusema tu sie vijana, anatakiwa kwenda mbali zaidi na kutuonyesha ni namna gani mfumo (ambao yeye alikuwa sehemu wa kuujenga) unatakiwa kufanyiwa mapitio ili vijana wawe na nafasi ipi katika kujenga taifa lao kama wao enzi hzo walivyopata kujenga taifa lile la ndoto ya BABA! Mtu makini yeyote anatakiwa kuelewa kuwa vijana leo hii ni waathirika wa mfumo katika taifa lao, tumemomonyolewa ujasiri katika kupambana na mustakabali, tumeaminishwa katika siasa za kichovu na zisizo za kujitegemea. Mfumo umeharibu Elimu (kama chemchem ya nguvu za fikra), hivi mzee Sinde hayajui yote haya? Sawa anayajua, na anasema tusilalamike tupambane.... Ni kweli tunapambana ndio maana tunajenga hoja ni namna gani tupewe nafasi ya kuweka sawa ili uharibifu ambao sisi tumefanyiwa na mfumo walioujenga wao usiende kwa wanetu! Anachokisema Mzee Sinde ni sawa na kutarajia Nzi aliye kwenye chupa iliyofunikwa na mwenyewe, atoke bila kupiga kelele wala kujipiga kwenye kuta.... Eti anampigia kelele?! Huu ni uenda wazimu wa kizee!
Namna anavyoongea mzee Sinde, ni wazi kuwa anamengi sana kusema na anayajua ila kwa sababu za usalama wake anaamua kukimbilia kundi letu kwa kujua hamna kitu vijana tutafanya... Pia yeye amepoteza hadhi ya ushujaa aliyowahi kuwa nao, kwa vijana kusambaratika mbele ya macho yake huku na yeye akilalamika kuwa vijana wanamkumbusha majukumu yake!
 
Ni vyema Mzee warioba akajua hali ilivyo ndani ya nchi yetu..!utaongeleaje umoja wa vijana wakati vyombo vya dola vinafanya kazi ya kuiba na kujenga ufa..? kidini, kiumri nk
Lakin pia umoja wa vijana hauwezi kuwepo hadi wezi hawa ccm waondolewe kwanza!
 
Back
Top Bottom